Rais wa Iran, Mahmud Ahmadinejad, aliwasili nchini Venezuela siku ya Jumapili, tarehe 8 Januari, katika siku yake ya kwanza ya ziara itakayoendelea kwenye nchi za Nicaragua, Cuba na Ecuador. Ziara yake imechochea miitikio mikali kwenye mitandao ya kijamii, ambapo watumiaji wanahoji ikiwa uwepo wake huko unaweza kuwa na faida yoyote kwa taifa hilo.
Kwenye Twita, baadhi wanakosoa kuwepo kwa Ahmadinejad na mapokezi aliyopewa na serikali ya Venezuela. Luis Carlos Díaz (@LuisCarlos) [es] anaandika:
Dice mucho del Ministerio de la Mujer su no-pronunciamiento sobre la visita de Ahmadineyad
Mwanablogu Carlos Bauza (@CarlosBauza) [es] anapendekeza kwamba ziara ya Ahmadinejad inaweza kuathiri uchaguzi ujao wa Urais nchini Venezuela, wakati Garcilaso Pumar (@garcilasop) [es] anaandika kwenye twita:
Mahmud Ahmadinejad es un tirano retrogrado, asesino y misógino. Chávez es un imbécil que le ilusiona ser todo eso. #Coneldebidorespeto
Wengine wanatumia alama ya #FueraAhmadinejadDeVzlakumtaka Rais huyo wa Iran aondoke nchini humo. Mtumiaji @PericoRipeado24, kwa mfano, anakosoa mtazamo wa Ahmadinejad kuhusu haki:
#FueraAhmadinejadDeVzla Porque tu justicia se ve en la horca, cuando tu pueblo roba es para comer
Wakati huo huo, watumiaji wa mtandao wanaomwunga mkono Rais Chavez walituma ujumbe kwenye twita kumpokea Ahmadinejad:
Basem Tajeldine (@BasemTajeldine): Merece un reconocimiento la valentía d Ahmadineyad al visitar Vzla, Cuba, Nicarg y Ecu, antes “patio trasero” d USA, hoy paises soberanos
Justo Bustamante Ch. (@JustoBustamante): BIENVENIDO MAHMUD AHMADINEJAD PRESIDENTE REPÚBLICA ISLAMICA DE IRÁN Lider de la Revolución Iraní. LOS REVOLUCIONARIOS VENEZOLANOS te saludan
Carlos R. Franco (@CarlosRFrancoM): Camarada Mahmud Ahmadinejad bienvenido a la tierra de Bolívar, patria libre, soberana y socialista… ¡Que chillen los escuálidos!
Hii ni ziara ya tano ya Ahmadinejad nchini Caracas. Baada ya kutania kuhusu “mabomu ya atomiki“, ziara yake iliisha siku ya Jumatatu, Januari 9 kwa kutia saini mfululizo wa makubaliano mengi ya pamoja, ikijumuisha Mkataba wa Makubaliano ya ushirikiano wa kiteknolojia kwa kuwafunza wataalamu katika elimu ya tabia za chembechembe ndogondogo na utengenezaji wa vifaa vinavyotokana na chembechembe hizo na kubadilishana walimu katika fani hii.