Waandishi wa kimataifa Wakashifu Israeli kwa Kuendelea kwa Ujenzi wa Makazi

Waandishi kumi na sita wa kimataifa ambao walishiriki katika Tamasha la Wapalestina la Fasihi, lililofanyika katika miji kadhaa Palestina kuanzia Mei 31 hadi Juni 5, walitoa taarifa kukashifu Israeli kwa kuendelea kwa ujenzi wa makazi na kupongeza juhudi za kususia kampeni ya Boycott Divest and Sanction (BDS). Taarifa, kupitia mtandao wa Facebook, inasema:

“Baada ya kushuhudia kibinafsi ukosefu wa haki kwa watu wa Palestina katika maeneo yaliyonyakuliwa na Israeli, ni kwa huzuni kubwa na kusikitishwa kwamba sisi – waandishi wa kimataifa na wasanii tuliotia saini hapa chini – twakumbuka idhini ya Benjamin Netanyahu ya wiki hii ya vitengo vingine vipya vya makazi haramu 1500 katika Ukanda wa Magharibi. Hii ni hasa ya kusikitisha kwa wakati ambao Wapalestina wameunda serikali ya umoja ambayo imetambuliwa na jumuiya ya kimataifa.

Makazi ya Israeli katika maeneo ya nchi nyingine kwa muda mrefu yametajwa kuwa kinyume cha sheria za kimataifa. Na makazi ya Israel kwenye maeneo ya Palestina ni kinyume cha sheria, na imetangazwa hivyo na jumuiya ya kimataifa kupitia maazimio mbalimbali ya Umoja wa Mataifa.

Makazi ya ziada yanaweza kuonekana tu kama kitendo cha uchokozi, kuonyesha kupuuza si tu kwa haki za binadamu na kiraia ya watu wa Palestina, lakini kwa sheria za kimataifa.

Tunapongeza juhudi isiyo na vurugu ya kampeni ya BDS (www.bdsmovement.net) na kuonyesha mshikamano wetu na mahitaji yake kwamba Israeli inapaswa kuzingatia maagizo ya sheria za kimataifa kwa:

1. Kukomesha ujenzi wa makazi na ukoloni wa ardhi yote ya Kiarabu na kubomolewa kwa Ukuta
2. Kutambua haki za msingi za raia wa Kiarabu na Palestina wa Israeli kwa usawa kamili; na
3. Kuheshimu, kulinda na kukuza haki za wakimbizi wa Kipalestina kurudi makwao na kwa mali yao kama ilivyoainishwa katika azimio la Umoja wa Mataifa 194

Kwa hivyo twatoa wito kwa serikali ya Israeli kuheshimu sheria za kimataifa na kugeuza idhini ya nyongeza ya makazi elfu moja na katika West Bank.

Sisi zaidi twatoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kufanya kazi kushawishi Israeli kuzingatia kanuni za msingi za sheria za kimataifa.

Imetiwa Saini na:

Sharif Abdel Khouddous
Susan Abdulhawa
Teju Cole
Nathan Hamilton
Nathalie Handal
Brigid Keenan
Sabrina Mahfouz
Michael Ondaatje
Ed Pavlic
Eliza Robertson
Sapphire
Kamila Shamsie
Ahdaf Soueif
Linda Spalding
Janne Teller
Haifa Zangana

Juni 6, 2014.”

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.