Habari kuhusu Bahrain

Rafiki Yangu Anateswa kwa Ku-blogu

GV Utetezi  5 Oktoba 2013

Safy ni mtu wa kawaida aliyewahi kufanya kazi kama afisa wa Teknohama mpaka aliposhuhudia rafiki yake akipigwa risasi na polisi wa kutuliza ghasia wakati wa majuma ya mwanzo ya mapinduzi. Hakuweza kuendelea kuwa "mtu wa kawaida" baada ya tukio hilo.

Bahrain: ‘Kususia michezo ya Olimpiki’

  11 Aprili 2013

Wa-Bahraini wengi wanatoa mwito wa kususuia michezo ya Olympics. Kwanza, mwana wa mfalme, ambaye amekuwa akituhumiwa kwa kujihusisha na utesaji wa wanariadha, anahudhuria michezo hiyo. Pili, sehemu kubwa ya timu ya nchi hiyo imetengenezwa na wanariadha wa ki-Afrika.

Mwaka Mpya na Mienendo ya Zamani Nchini Bahrain

  8 Januari 2013

Wakati nchi mbalimbali ulimwenguni kote zikiukaribisha mwaka mpya kwa fataki na shamrashamra, serikali ya Bahraini iliandaa utaratibu wa aina yake kwa waandamanaji nchini humo. kwa bahati, watumiaji wa mtandao wa intaneti walikuwa tayari, kuonesha na kuweka kumbukumbu ya baadhi ya matukio kwa ajili ya kushuhudiwa na sehemu nyingine yote ya ulimwengu.

Hakuna Usalama kwa Waandishi wa Kiraia Nchini Bahrain

  1 Januari 2013

Baada ya video ya "kibao" cha polisi wa Bahrain kusambaa sana mtandaoni, Waziri wa Mambo ya Ndani alitoa tamko akiomba kuwa yeyote aliyepiga picha tukio hilo aliripoti haraka kwa mamlaka zinazohusika. Siku mbili baadae, na kinyume na kauli hiyo, watu wengi walishangazwa na kukamatwa kwa mpiga picha.

Uarabuni: Sera ya Romney kwa Mashariki ya Kati Yaibua Mjadala

  8 Oktoba 2012

Hotuba ya Mgombea urais wa Marekani kupitia chama cha Republican Bw. Mitt Romney iliyoelezea sera yake ya nje imeibua mjadala mzito miongoni mwa raia wa mtandaoni leo hasa wale watokao katika nchi za ki-Arabuni. Twiti zinazohoji sera ya mambo ya nje ya Marekani kwa Mashariki ya Kati ziliendelea wakati ambao Romney, anayepeperusha bendera ya chama cha Republican, alipozungumza katika Chuo cha Jeshi cha Virginia. Endapo atachaguliwa, Romney ameahidi kuwa na sera rafiki za mambo ya nje, tofauti na mwelekeo usiotabirika wa sera za Obama wakati huu ambapo mabadiliko ya kisiasa yanaendelea kulikumba eneo la Mashariki ya Kati.

Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011