Habari kuhusu Kichina
Maandamano ya Taiwan ya #KupingaBunge, Yatafsiriwa
Mamia ya watafsiri wamejipanga kupitia mtandao wa facebook kutafsiri habari kuhusu maandamano ya raia wanaojikusanya kwenye Bunge la nchi hiyo kupinga hatua ya chama tawala nchini humo kupitisha mkataba wa kibiashara wenye utata na nchi ya China.
Mwandishi Mwandamizi wa Kichina Akosolewa kwa Kujifungulia Marekani
"...anachotaka tu ni mwanae awe na mtindo wa kawaida wa maisha, kitu ambacho hakina uhusiano na uzalendo. Labda, hili ndilo tatizo ambalo serikali yapaswa kulitafakari..."
Hong Kong: Pinga Biashara ya Pembe za Ndovu
Muungano wa watu binafsi na Asasi Zisizo za Serikali zinazoguswa na tatizo la ujangili wa tembo, Hong Kong kwa Tembo, uliandamana Oktoba 4, wakiitaka Hong Kong kuteketeza hifadhi yake ya tani 25 za pembe za ndovu.
Barua ya Wazi ya Kushinikiza Kuachiwa Huru kwa Mwanasheria
Mnamo Julai 23, 2013, zaidi ya raia 400 wa China wamesaini barua ya kushinikiza serikali ya China kumuachia huru Xu Zhiyong, ambaye ni mwanasheria mashuhuri na mpigania haki aliyekamatwa mnamo Julai 16 baada ya kushinikiza kuachiwa kwa wanaharakati pamoja na kuratibu kampeni dhidi ya uovu unaofanywa na serikali. MRADI WA...
Maandamano Yasitisha Ujenzi wa Mtambo wa Nyuklia Kusini mwa China
Kufuatia siku tatu mfululizo za maandamano, inaonekana kuwa serikali ya Manispaa ya Heshan katika jiji la Jiangmen imesitisha mpango wake wa ujenzi wa mtambo mkubwa wa nishati ya Nyuklia. Baadhi ya watu wanaamini kuwa ushindi huu ni wa muda mfupi tu. Wana wasiwasi kuwa, mradi huu unaweza kuibukia sehemu nyingine karibu na Delta ya mto Pearl, Kusini mwa China mahali palipo na idadi kubwa sana ya watu.
China Yawaamrisha Vijana Kuwatembelea Wazazi Wao
Wiki hii, China imeanza kutumia sheria mpya inayowataka watoto waliokwisha fikia umri wa kujitegemea kuwa na mazoea ya kuwatembelea wazazi wao, hali iliyopelekea sheria hii kudhihakiwa na watumiaji wa tovuti ya jukwaa maarufu la wanablogu la China lijulikanalo kama Sina Weibo.
Maisha Binafsi ya Watawala Wapya wa China
Shirika la Habari la Xinhua lilichapisha[zh] mfululizo wa wasifu wa maisha binafsi ya watawala wa juu China, ikiwa ni pamoja na picha za familia zao, ambazo ni nadra sana katika vyombo vya habari vya China. Hatua hiyo imechukuliwa na wengi kama dalili nyingine kuwa utawala mpya wa China unaweza ukawa...
Italia Yalaumiwa kwa Ukiukaji wa Haki za Wakimbizi wa Kiafrika
Februari 23, Mahakama ya Haki za Binadamu ya Ulaya huko Strasbourg ilikuja na hukumu ya kihistoria kwamba Italia imevujna Tamko la Ulaya la Haki za Binadamu kwa kuwazuia na kuwarudisha wakimbizi wa ki-Eritrea na Somalia kwenda Libya. Abdoulaye Bah anaripoti.
China: Pato la Taifa Linaongezeka, Matumizi Katika Huduma za Jamii je?
Tunaendelea kusikia kuwa uchumi wa China unaendelea kukua; je matumizi ya huduma za jamii yameongezeka? Akiba binafsi zinabaki kwenye benki, anaandika mwanablogu mmoja: kutokea hospitali mpaka shuleni mpaka malipo ya uzeeni, China haiwezi kujilinganisha.
China: Kashfa ya Wizi wa Kitaaluma Uliofanywa na Wang Hui, Mtazamo wa Kimataifa
Kuna kashfa ya wizi wa kitaaluma iliyoibuka mwezi Machi katika duru za kitaaluma za Kichina pale Profesa wa Fasihi wa Chuo Kikuu cha Nanjing, Wang Binbin, alipotuhumu kwamba kazi ya uzamizi ya Wang Hui kuhusu Lu Xun – Kugomea Kukata Tamaa – ina aya kadhaa ambavyo vimenukuliwa moja kwa moja...