Below are posts about citizen media in Bangla. Don't miss Global Voices বাংলা ভার্সন, where Global Voices posts are translated into Bangla! Read about our Lingua project to learn more about how Global Voices content is being translated into other languages.

Habari kuhusu Kibangla

Bangladesh: Jengo Laporomoka, Mamia Wauawa kwenye Vifusi

  29 Aprili 2013

Janga jingine tena la kiwanda nchini Bangladesh, safari hii jengo la ghorofa tisa lilianguka na kuua zaidi ya watu 142 na watu wengine karibu elfu moja kujeruhiwa. Watu wengine wengi bado wamenaswa kwenye kifusi na harakati za kuwaokoa bado zinaendelea. tukio hili linatokana na uzembe wa baadhi ya watu kwani utawala wa kiwanda hiki uliwashinikiza watu kuendelea kufanya kazi katika jengo ambalo halikuwa salama.

Serikali ya Bangladeshi Yawafuatilia Wanablogu, Yawatuhumu Kuukashfu Uislam.

  28 Aprili 2013

Kadri mapambano makali kati ya wanaharakati wa Kiislamu na serikali yanavyoendelea kusababisha migongano ya kidini nchini Bangladesh, Mamlaka ya Mawasiliano ya nchi hiyo imechukua hatua ya kuwanyamazisha wanablogu wanaoonekana wapinzani wa Uislamu na serikali. Asif mshindi wa tuzo ya mwanablogu bora amekuwa akilengwa na hatua hizo kwa siku za hivi karibuni.

Bangladeshi: Raia Wakutana Kudai Haki Itendeke

  17 Februari 2013

Kidogo kidogo, makutano ya Shahbag katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka yamefurika watu wenye lengo la kutaka haki kufuatia ukatili uliofanywa mnamo mwaka 1971 wakati wa harakati za vita vya kutafuta uhuru pamoja na kudai hukumu ya kifo kwa wahalifu wa vita.Drop by drop, the Shahbag intersection in Bangladesh's capital city Dhaka has become an ocean of people, demanding justice for the atrocities committed during the country's 1971 liberation war and death penalty for war criminals.

Bangladeshi: Msichana Mwingine Mzawa Abakwa na Kisha Kuuliwa.

  2 Januari 2013

Kwa mara nyingine msichana mzawa ameuawa nchini Bangladesh baada ya kubakwa kikatili. Mhanga huyo, Khomaching Marma (14) alikuwa mwanafunzi wa darasa la nane. Ubakaji huu wa kikatili uliosababisha mauaji kwa mara nyingine tena umeamsha hasira na ghadhabu nchini kote. Watumiaji wa mtandao pia wanapinga vikali vitendo hivyo.

Watoto wa Mitaani Bangladesh Wakabiliwa na Unyanyasaji

  13 Novemba 2012

Jumla ya watoto wa mitaani nchini Bangladeshi wanakadiriwa kufikia 400,000. Karibu nusu ya idadi hiyo wanaishi katika Jiji la Dhaka. Asilimia kubwa ya watoto hao ni wasichana. Wasichana hao wa mitaani huishi katika mazingira yenye hatari nyingi hasa unyanyasaji na dhuluma nyingine.

Bangladeshi: Ku-twita na kublogu tetemeko la ardhi

  5 Agosti 2008

Tetemeko la ardhi la wastani lilitikisa jiji la Dhaka siku ya tarehe 27 Julai mnamo muda wa saa 00:51 kwa saa za Bangladeshi (+6 GMT). Russell John anaripoti katika blogu yake: Nilikuwa nimelala kwenye kitanda changu huku nikongea kwa simu na rafiki yangu, na ghafla nikahisi kitanda kikitetemeka. Ndani ya...

Kuhusu habari zetu za Kibangla

bn