Leo ni Juni 4, maadhimisho ya 26 ya maandamano ya kudai demokrasia ya Tiananmen mwaka 1989.
Katika miaka ya hivi karibuni, baadhi ya tarakimu zimepotea kwenye mtandao wa Intaneti nchini China kwa sababu ya udhibiti wa taarifa. Tarakimu hizi ni 64, 89 na 535 —zenye kuunganisha kupata Mei 35, namna maarufu yakukumbuka siku ya Juni 4. Tarakimu hizo hazitafutiki kwenye tovuti za kutafutia taarifa na haziwezi kuonekana kwenye mitandao ya kijamii.
Mchora katuni za kisiasa Biantailajiao, kupitia mtandao wa twita, alionesha namna hiyo ya kijinga ya kujaribu kufuta historia:
如果可以做到,他們會毫不猶豫讓這一天從日曆上徹底消失 pic.twitter.com/5ERnYBn63o
— 变态辣椒 (@remonwangxt) June 3, 2015
Kama inawezekana, wanaweza kuifuta kabisa tarehe hii kwenye kalenda.