ISIS Yashambulikia Kwa Mara Nyingine Msikiti wa Shia Nchini Saudi Arabia

kwenye dawati lakuthibitisha habari la Global Voices, mradi unaoendeshwa kwa ushirikiano kati ya Meedan Checkdesk, zana ya mtandaoni ya kufuatilia habari, na Global Voices Online, Joey Ayoub anaonesha miitikio ya awali kabisa kuhusu kupigwa bomu kwa msikiti wa pili wa Shia huko Dammam, Jimbo la Mashariki mwa Saudi Arabia, siku ya Ijumaa.

Watu watatu wameuawa kwenye shambulio hilo la kujitoa mhanga, na Walayat Najd, tawi la ISIS nchini Saudi Arabia, limedai kuhusika, na watu kumi wamejeruhiwa.

Mnamo Mei 22, mtu aliyekuwa na bomu alijilipua kwenye msikiti wenye watu wengi huko Al Qadih, kwenye jimbo la Qatif, na kuua watu wasiopungua 21, ikiwani pamoja na mtoto, na kujeruhi wengine 120, kwenye shambulio baya kuwahi kuonekana katika kipindi cha miaka kumi nchini Saudi Arabia.

Mwezi Novemba, watu nane waliuawa huko Al Ahsa, kwenye jimbo la Mashariki, baada ya wanamgambo kushambulia kituo cha kijamii kinachomilikiwa na Shia, mahali ambapo sherehe ya kidini ilikuwa ikiendelea.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.