Swali: Wapiganaji Wangapi wa Jihadi Wana Historia ya Jeshi?

Kwa kutumia dondoo kutoka kwenye ripoti ya Der Spiegel kuhusu watu walionyuma ya muundo wa ISIS, mwanablogu wa Palestina Iyad El-Baghdadi anatwiti:

Baada ya habari ya Spiegel kuhusu watu walio nyuma ya uongozi wa ISIS – nimejiuliza wapiganaji wa Jihadi wangapi wana historia ya jeshi?

Der Spiegel anamtaja Iraqi Samir Abd Muhammad al-Khlifawi, aliyeuawa huko Tal Rifaat in Syria mwezi Januari 2014, kuwa ndiye “moyo” wa ISIS, tawi la Al Qaeda ambalo limekuwa na udhibiti wa nchi kama Iraq na Syria, wakiacha hofu, vifo na uharibifu sehemu mbalimbali. Inasema kwamba al-Khlifawi alikuwa kornel wa zamani kwenye kitengo cha ujasusi katika jeshi la ulinzi wa anga enzi za utawala wa Saddam Hussein.

El-Baghdadi anaongeza:

Kamandi kuu ya ISIS ina mafisa wa zamani wa Jeshi la Iraq; nchini Libya maafisa wa zamani wa jeshi la Gaddafi ndio wanaunga mkono ugaidi huu…

Anaeleza:

ISIS nchini Misri (Sinai) pia ina maafisa kadhaa wa zamani wa jeshi la Misri; Mkuu wa Ansar Bayt al Maqdis ni komandoo wa zamani wa jeshi la Misri


Hakiki taarifa hizi:

Tusaidie kufuatilia na kuhakiki habari hizi kuhusu wakuu wa ISIS wenye histori ya jeshi kwenye dawati letu la kuhakiki utaarifa la Global Voices hapa.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.