Mapendekezo Yanapokelewa kwa Ajili ya Mwezi wa Historia Nyeupe 2015

Likiwa limeandaliwa na blogu ya Africa is a Country [Afrika ni Nchi], tukio la Mwezi wa Historia Nyeupe linajongea mwezi ujao:

Mwezi Machi mwaka jana ndio ulikuwa mwezi wa uzinduzi wa zoezi hilo kwenye blogu hii, na bila kupuliza sana mavuvuzela yetu kw akujisifu, ule kwa hakika ulikuwa ni mwezi mzuri. Tunaahidi kufanya kama tulivyofanya kipindi hicho.

Tutakuwa na mambo kama ngozi ya Kathleen Bomani kutoka Human Skin, Filadefia ya miaka ya 1880 na tutakuwa na mambo mengi, kama vile utawala wa kikatili wa Uingereza kwenye miaka ya 1950 nchini Kenya na hata wakati ule serikali ya Afrika Kusini ilipotuma ujumbe kwenda Marekani kutafuta kujua namna “kuweka nafasi za mahotelini/ndege” kunavyofanyika.

Kama ungependa kushiriki, unatakiwa:

Wasiliana nasi kwa editorial [at] africasacountry [dot] com na tufahamishe kile unachotaka tukiandikie. Angalia kile tulichokiandika mwaka jana kupata wazo la kile tunachokitafuta.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.