Mnamo Septemba 19, 1985, kwenye maeneo ya kati, Kusini na Magharibi mwa Mexico, hususani kwenye Wilaya ya Shirikisho, yalikumbwa na tetemeko kubwa, linalosemekana kuwa baya zaidi katika historia ya Mexico inayojulikana. Wakikumbuka miaka 29 tangu tukio hilo litokee, Katibu wa Ulinzi wa raia wa Wilaya ya Shirikisho aliandaa mafunzo ya tetemeko, kwa ajili ya kuwasaidia watu kujua namna ya kuchukua hatua yanapotokea matukio kama haya. Watu walishiriki kwa kiasi kikubwa, katika jiji kuu la nchi hiyo pamoja na majiji mengine.
Realizamos con éxito el simulacro de evacuación por sismo, recordando el ocurrido en 1985, en la ciudad de México. pic.twitter.com/wQUM6h5Zpd
— UTTAB (@UTTAB) septiembre 19, 2014
Tulifanya mazoezi ya uokoaji katika tukio ya tetemeko, tukikumbuka kile kilichotokea mwaka 1985 huko Mexico City.
Estiman que 17 mil edificios fueron evacuados por simulacro http://t.co/4bfislAT6R pic.twitter.com/ls9WPrgkUM
— Metrópoli (@Univ_Metropoli) septiembre 19, 2014
Majengo yanayokadiriwa kuwa 17,000 yalifanyiwa uokozi wakati wa mafunzo hao.
El @GobYucatan de @RolandoZapataB ha realizado simulacro histórico en Palacio. pic.twitter.com/CNVfBqrhx7
— YUCATAN AL MINUTO (@YUCATANALMINUTO) septiembre 19, 2014
Serikali ya Yucatán inayoongozwa na Rolando Zapata iliendesha mafunzo hayo kwenye ikulu ya nchi hiyo.
Tlalnepantla se une al Mega Simulacro Sísmico organizado en el Estado de México @Pablo_Basanez pic.twitter.com/CZxA9661v2
— Edgardo Garza (@egygarza) septiembre 19, 2014
Tlalnepantla anashiriki mafunzo makubwa ya kupambana na matukio ya tetemeko la ardhi yaliyoongzwa na na serikali ya Mexico.
El #simulacro no sólo es honor a las víctimas del terremoto, también lo es de la #sociedad vs la burocracia pic.twitter.com/8NjQ4xbrD1
— Venancio Queupumil (@VQ_Cabrera) septiembre 19, 2014
Mafunzo hayo yalikuwa si tu kuwakumbuka wahanga wa tetemeko la ardhi, bali kushughulikia jamii na taratibu za kirasimu za uendeshaji wa shughuli za serikali.