Ushiriki Mkubwa wa Umma katika Mafunzo ya Tetemeko la Ardhi Nchini Mexico

Mnamo Septemba 19, 1985, kwenye maeneo ya kati, Kusini na Magharibi mwa Mexico, hususani kwenye Wilaya ya Shirikisho, yalikumbwa na tetemeko kubwa, linalosemekana kuwa baya zaidi katika historia ya Mexico inayojulikana. Wakikumbuka miaka 29 tangu tukio hilo litokee, Katibu wa Ulinzi wa raia wa Wilaya ya Shirikisho aliandaa mafunzo ya tetemeko, kwa ajili ya kuwasaidia watu kujua namna ya kuchukua hatua yanapotokea matukio kama haya. Watu walishiriki kwa kiasi kikubwa, katika jiji kuu la nchi hiyo pamoja na majiji mengine.

Tulifanya mazoezi ya uokoaji katika tukio ya tetemeko, tukikumbuka kile kilichotokea mwaka 1985 huko Mexico City.

Majengo yanayokadiriwa kuwa 17,000 yalifanyiwa uokozi wakati wa mafunzo hao.

Serikali ya Yucatán inayoongozwa na Rolando Zapata iliendesha mafunzo hayo kwenye ikulu ya nchi hiyo.

Tlalnepantla anashiriki mafunzo makubwa ya kupambana na matukio ya tetemeko la ardhi yaliyoongzwa na na serikali ya Mexico.

Mafunzo hayo yalikuwa si tu kuwakumbuka wahanga wa tetemeko la ardhi, bali kushughulikia jamii na taratibu za kirasimu za uendeshaji wa shughuli za serikali.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.