Highway Africa 2014 Yasogeza Mbele Tarehe ya Mwisho ya Kujiandikisha

Tarehe ya mwisho ya kujiandikisha kwa ajili ya Mkutano wa 18 wa mwaka wa Highway Africaimesogezwa mbele mpaka Ijumaa, Agosti 08 2014:

Kutokana na kuongezeka kwa shauku ya watu kuhudhuria mkutano wa mwaka wa 18 wa Highway Africa, tarehe ya mwisho ya kujiandikisha imesogezwa mbele mpaka Ijumaa, 08 Agosti 2014.

Mkutano huo mkubwa wa mwaka wa Waandishi wa Kiafrika unafanyika kwenye Chuo Kikuu cha Rhodes, Grahamstown, Afrika Kusini, kuanzia Septemba 7 – 8 2014.

Mkutano huo ukiwa na kauli mbiu, “Mitandao ya Kijamii – kutoka pembezoni mpaka kwenye vyombo vikuu”, utakuwa ukichambua namna mitandao ya kijamii ilivyoathiri maeneo yote ya maisha yetu katka kipindi cha miaka 10 iliyopita.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.