Israel Yaanza Operesheni ya Ardhini Gaza

Israel begins ground operations on Gaza. iFalasteen shares this photograph from Gaza on Twitter

Israel imeanza operesheni ya ardhini Gaza. iFalasteen anatuma picha hii kutoka Gaza kwenye mtandao wa Twita

Vikosi vya kijeshi vya Israeli vimeanza kuingia Gaza, baada ya siku 10 za mapigano zilizochukua maisha ya Wapalestina 200. M-Israeli mmoja aliuawa kwa shambulio la roketi kwenye eneo la Palestina. Hatua hiyo inakuja baada ya Hamas, kikundi kinachoitawala Gaza, kukataa pendekezo la kumaliza mapigano lililotolewa na Misri.

Tovah Lazaroff, mwandishi wa Boston aliye katikati ya mgogoro wa Israel na Palestina, anatwiti:

Ni rasmi sasa kutoka kwenye ofisi ya Waziri Mkuu wa Israel, vikosi vya jeshi vimeanza kuingia Gaza

Anaongeza:

Ofisi ya Waziri Mkuu: Baraza la Mawaziri limeidhinisha operesheni ya ardhini baada ua Israeli kukubaliana na pendekezo la Misri la kusitisha mapigano. Hamas ilikataa mapendekezo hayo

Ardhini huko Gaza, iFalasteen anasema:

Mabomu kila mahali hapa Gaza, hakuna umeme na kuna mwanga mkali wa milipuko na mabomu…

Mabomu yanapigwa mfululizo na hakuna pa kukimbilia…Mungu tu atailinda Gaza

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.