Matamshi Matano ya Kushangaza Kufuatia Kuanguka kwa Ndege MH17 Nchini Ukraine

So much for "knowing that feel," when it comes to polemics surrounding the downed Malaysian airliner. Images mixed by Kevin Rothrock.

Kuna namna nyingi “kujua mtu anavyojisikia,” ukifuatilia matamshi yanayotolewa baada ya kutunguliwa kwa ndege ya Malaysia. Picha zimechanganywa na Kevin Rothrock.

Maafisa, wanasiasa na waandishi maarufu wa Kirusi walikuwa wepesi kutoa maoni kuhusiana na ajali ya Ndege ya Malaysia MH17, iliyoanguka Mashariki mwa Ukraine siku ya Alhamisi, Julai 17. Mamlaka za Kyiv, Moscow, na Donetsk zimekuwa zikishutumiana, kubebeshana lawama kwa kutunguliwa kwa ndege hiyo ya abiria na kuua watu wote karibu 300 waliokuwemo ndani yake. Wakati hisia zikiendelea kuongezeka, matamko machache yaliyotolewa na watu mashuhuri mjini Moscow na Donetsk yamevutia hisia ya watumiaji wa Intaneti mtandaoni. 

1. Katika hili, hatukufanya.

Waziri Mkuu aliyejitangaza mwenyewe wa Jamhuri ya watu wa Donetsk, Aleksandr Boroday, hakuwa na uhakika kuhusiana na uhusika wa waasi katika tukio hili:

Bahati mbaya, hii ni nukuu ya siku. [Maneno yanasomeka, “Kama ni kweli ni ndege ya abiria, basi haikuwa sisi,” Alexandr Boroday.]

2. Ina maana yoyote kujua nani alifanya kitendo hiki?

Leonid Kalashnikov, naibu mwakilishi wa kamati ya Bunge la Urusi ya mambo ya kimataifa, aliiambia TV Rain haikuwa na maana yoyote kujua nani wa kumlaumu kwa kuiangusha ndege hiyo:

“Вам что, легче станет, если узнаете, кто сбил самолет?”

“Nini, utajisikia nafuu kaa utamjua aliyeiangusha ndege hiyo?”

3. Uovu wa hali ya juu

Akiwa ameumizwa na kile waasi wa Urusi na ‘waendesha propaganda’ wa Ukraine walichokirudia mara kwa mara hisia zile zile (kwamba walikosoa serza ya Urusi kwa Ukraine), Konstantin Rykov wa chama tawala cha siasa Urusi alikuwa na haya ya kusema:

Katika nyakati kama hizi ni wazi kuna watu wanatarajia kitu na wanacho wanachokitaka…wapigania uhuru wetu na wapiga propaganda wa Ukraine wanashindania kile kile…

4. Ni rahisi: hakuna wa kumlaumu

Mkuu wa shirika la Russia TodayMargarita Simonyan alionyesha namna janga hilo lilivyo na faida kwa wa-Soviet wasio na akili:

Kw amuda mrefu nimekuwa nikifanyia kazi taarifa kadhaa za habari zinazotokea, na nimehitimisha kuwa siamini kabisa namna watu wanavyojaribu kuunganisha matukio kujengea hoja imani zao. Lkaini ninaamini kuwa Usoviet ina matatizo. 

5. Waasi? Waasi gani?

Mwisho lakini si kwa uzito ni mwitikio wa Vladimir Putin mwenyewe, aliyeliambia shirika la habari la ITAR-TASS kwamba Kyiv inawajibika kwa anga la Ukraine mashariki inayodhibitiwa na waasi.

“Безусловно, государство, над территорией которого это произошло, несет ответственность за эту страшную трагедию. […] Этой трагедии не произошло бы, если бы на этой земле был мир, не были бы возобновлены боевые действия на юго-востоке Украины”

“Kwa hakika, nchi ambayo mpaka wake ndiko tukio hili limetokea inawajibika kwa janga hili […] Janga hili lisingetokea kama pangekuwa na amani kwenye nchi hiyo, kama mapigano yasingeibuka tena Kusini Mashariki mwa Ukraine.”

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.