Je, Madaraka ni Matamu Kiasi cha Watawala wa Afrika Kushindwa Kuyaachia?

Gershom Ndhlovu anaangalia sababu za kwa nini watawala wa Afrika hawataki kuachia madaraka:

Kumekuwepo na tetesi, dondoo na hata uvumi kuhusu afya au basi udhaifu wa afya ya Rais wa Zambia Michael Chilufya Sata, aliye madarakani tangu Septemba 2011. Tetesi hizi zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii kiasi kwamba serikali ya chama chake cha Patriotic Front (PF) imekuwa ikifanya jitihada za kuzidhibiti au hata kuzizima kabisa tetesi hizo.

Serikali haijajibu tetesi hizi ukiacha matamko ya mstari mmoja yanayokanusa habari kuhusu hali ya afya ya mkuu huyo wa nchi mwenye miaka 76 ambaye vile vile ni mwanasiasa wa siku nyingi.

Hata hivyo, Sata mwenyewe alipoonekana hadharani kwneye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Mei Mosi kupokea heshima kutoka kwa wafanyakazi nchini humo, na kukaa kwa muda mfupi hapo, na kutoa hotuba fupi ya dakika moja kabla ya kuingia kwenye msafara wake kurudi ikulu, watu wengi walianza kuamini kuwa Rais si mzima.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.