Wajibu wa Kisayansi katika Mawasiliano

Katika mfululizo mpya wa Cosmos, Víctor R. Ruíz anaonyesha jinsi ambavyo kutafuta maarifa ya kisayansi limekuwa ni jukumu la kijamii na kisayansi katika nyanja za umma:

Kabla na wakati huo, makampuni binafsi na serikali yalikuwa na ajenda ambazo daima hazikuwa zikiambatana na maslaha mapana ya jamii. Makampuni ya mafuta yaliendelea kuhusiana na wanasayansi kwa malipo yenye kutia shaka. Nchi zinaendelea kufadhili maendeleo ya silaha za hali ya juu. Na wakati mwingine, mipaka kati ya maslahi binafsi na ya umma haiko wazi. Kama nilivyoeleza katika mazungumzo yangu ya Naukas Bilbao mwaka jana, Shirika la Usalama wa Taifa (NSA) huajiri theluthi tatu ya wataalamu wa hisabati kote duniani. Nyaraka zilizofichuliwa na Edward Snowden zinaonyesha kwamba wametekeleza na hata kuhujumu teknolojia ya mtandao kwa upelelezi wa ngazi za kimataifa, si kwa minajili ya kupambana na ugaidi kama kama ambavyo imekuwa ikifanyika kwa upelelezi wa kibiashara.

Víctor anahitimisha kutoka maoni yake hayo ya kisayansi:

Maneno matupu ya mwanasayansi wazimu yanaweza kuonekana kama hadithi, lakini mabomu yaliyoanguka Hiroshima na Nagasaki hayakutengenezwa na majeshi ovu. Hatuwezi kugeuza shavu la pili na kujifanya kwamba si wanasayansi wala wahandisi huendeleza teknolojia ambazo baadaye hutumika kwa minajili ya kupeleleza mabilioni ya wananchi au kuua raia kwa vifaa vya udhibiti. Leo, kama jana, ni wajibu wetu wote kuzungumza juu ya shauku ya elimu na kukosoa ushirikiano wa wanasayansi katika miradi ambayo hutishia jamii yetu.

Makala yaliyoainishwa yalishirikishwa katika blogu ya kwanza ya #LunesDeBlogsGV [Blogu za Jumatatu kwenye GV] Mei 5, 2014.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.