Watu wasiopungua watatu walikufa na kati ya watu 25 na 30 wamenaswa baada ya kuanguka kwa mgodi ulikuwa unaendeshwa kinyume cha sheria katika idara ya Cauca, kusini magharibi mwa Colombia, kama ilivyoripotiwa [es] na vyombo vya habari mnamo Alhamisi, Mei 1.
HSBNoticias aliarifu kwenye mtandao wa Twita:
[FOTOS] [+18] Se lleva a cabo el rescate de 25 a 30 mineros atrapados en una mina del #Cauca ➜http://t.co/Cm0XpWdYFq pic.twitter.com/6xpfKFDLS4
— HSBNOTICIAS (@HSBNOTICIAS) Mayo 1, 2014
[PICHA] juhudi za uokoaji kuwatafuta wachimbaji 25 hadi 30 walionaswa katika mgodi katika idara ya Cauca.