Mkuu wa Upelelezi wa Jeshi la Sudani Kusini Akana Jaribio Mapinduzi ya Kijeshi

Mkuu wa upelelezi wa jeshi nchini Sudani Kusini amekana kuwa kulikuwa na jaribio la mapinduzi ya kijeshi tarehe 15 Desemba, 2013.

PaanLuel Wel anaripoti:

Taarifa kutoka Juba zinasema mkuu wa upelelezo wa jeshi, Jenerali Mac Paul Kuol Awar, ametupilia mbali madai ya jaribio la kijeshi la Desemba 15, 2013. Mac Paul alitwa na serikali kutoa ushahidi dhidi ya mahabusu wanne wa kisiasa (Pagan, Oyai, Majak na Gatkuoth) waliopandishwa kizimbani wakijibu mashitaka ya uhaini.

Kimsingi, Mkurugenzi wa upelelezi wa kijeshi, aliyeitwa kuyapa nguvu madai ya serikali kuwa kulikuwa na mapinduzi, alikuwa imara kudai hapakuwa na kitu kama hicho. Badala yake, alisema, palitokea hali ya kutokuelewana miongoni mwa wanajeshi wa Tiger Battalion, ambao hawakudhibitiwa mpaka kutokuelewana huko kukaeneza uasi nchini kote.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.