Namna Huduma ya Kuhamisha Fedha kwa Njia ya Simu Ilivyobadili Maisha ya Wakenya

M-Pesa payment till at a restaurant in Kenya. Photo released under Creative Commons by Wikipedia user Raidarmax.

Mahali pa kufanyia malipo ya M-Pesa kwenye hoteli nchini Kenya. Oicha imetolewa chini ya leseni ya Creative Commons na mtumiaji wa Wikipedia Raidarmax.

Mwezi Machi 2014 yatakuwa ni maadhimisho ya miaka saba tangu M-Pesa, huduma ya kufanya miamala ya kifedha kwa njia ya simu na huduma ndogo za kibenki, ilipoanzishwa Kenya na kampuni ya simu za mkononi iitwayo Safaricom. M-Pesa inafanya kazi kama benki; watumiaji wa huduma hiyo huhifadhi fedha kwenye simu zao na kutoa fedha kupitia wakala au duka la Safaricom kwa kuonyesha kitambulisho na namba ya simu.

Safaricom ilikuwa kampuni ya kwanza nchini Kenya kutoa huduma ya miamala ya kibenki. Inabaki kuwa  kampuni iliyotawala biashara hiyo hata leo, wakati kukiwa na makapuni kama Airtel, Orange na Yu ambayo pia yanatoa huduma kama hiyo.  Katika kusherehekea miaka saba ya huduma hiyo, Safaricom iliwahamasisha wa-Kenya kwenye mtandao wa Twita kutumia alama habari ya #BeforeMPESA [Kabla ya MPESA] kueleza namna huduma hiyo ilivyobadili maisha.

Hapa unaweza kusoma maoni yaliyojitokeza mara nyingi:

1. M-Pesa imewapa Wakenya mbadala wa kutunza fedha zao kwa usalama:

Kabla ya Mpesa

Kabla ya Mpesa: Namna watu walivyokuwa wakitunza fedha zao kwa usalama

2. Kenyans can now pay for almost anything through M-Pesa, even church offerings [sadaka] and electricity bills:

Ninaweza kulipa sadaka kwa urahisi nikiwa sebuleni kwangu, bila kulazimika kwenye kanisani

Hivi ndivyo nilivyokuwa nilisafiri kwenda benki kulipa bili yangu ya umeme

Kufupisha masimulizi huduma hii imefanya maisha yangu kuwa rahisi tangu nijiunge na Mpesa

Ukitoka kuzunguka, ukaishiwa na mafuta….unatembea mwendo mfupi tu unalipa na Mpesa

Baada ya kupata chakula na rafiki yako wa kike na kisha unakumbuka uliacha pochi yako nyumbani

Malipo ya mahari ilikuwa kazi…baada ya Mpesa sasa ni rahisi

Baadhi ya watu walizimia kwenye mistari mirefu benki wakati wa kufungua shule kwa sababu ya kuchoka kusubiri

Namna nilivyokuwa nikisubiri kutumiwa hawala ya fedha kwa njia ya posta

Kabla ya Mpesa na baada ya miaka saba ya Mpesa

3. M-Pesa inaweza kupatikana kwa simu yoyote:

@kebiwot Miaka saba ya MPESA lakini simu zina miaka 20

Bado, si kila mmoja anaifurahia M-Pesa

Baadhi ya Wakenya walitumia maadhimisho hayo kuonyesha hasira zao kwa M-Pesa na kuwakosoa wale wanaoisifia huduma hiyo:

Na hadithi hizi za kusadikika za MPESA

Namna Safaricom wanavyokuita kuja kukumaliza….

Samuel Gikuru alikuwa na wasiwasi na nia ya Safaricom na hata akaituhumu kampuni hiyo kuiba wazo la Mkenya alibuni huduma hiyo:

Hivi ni mimi pekeyangu au na mwingine amegundua kuwa Safaricom inafanya kila inachoweza kwa makusudi mazima kuua Vipaji vya kiteknolojia vinavyoibukia Kenya? Kuna hadithi inasimulia namna Mkenya alivyoibiwa wazo lake lenye thamani ya dola bilioni moja ambalo leo ndio limekuwa M-Psa. Kijana huyo mwenye akili inasemekana aliwaendea wakubwa wa Safaricom na wakamkatalia kuwa wazo lake lisingetekelezeka na ajabu miezi kadhaa baadae wakazindua huduma hiyo. Hiyo ndiyo hadithi iliyo kwenye midomo ya Wakenya wote. Hata hivyo, kitabu kipya kinadai kuwa mwajiriwa mwandamizi wa Vodafone ndiye aliyebuni M-Pesa mwaka 2003. Wakenya ni kama hawafaidiki na ubunifu wa M-Pesa ambao ndio unaiweka Kenya kwenye ramani ya dunia kama kituo cha ubunifu.

….Ukiwa na MPESA, faragha yako hailindiw. Kwa kutumia hela kidogo mpaka hata shilingi 10, mtu yeyote anaweza kukutambu kama mmiliki wa lini ya simu, kama namba yako imesajiliwa kwa huduma hiyo, kirahisi tu. Kama vile haitoshi watekaji wanaweza kutumia husuma hii kudai fedha. Ili kuhakikisha kuwa hawakamatwi au kuingia mtegoni kirahisi, wanafungua akaunti kwa kutumia kitambulisho bandia ambacho kinaweza kutengenezwa kinyume cha sheria pale kwenye mtaa wa River road Nairobi. Safaricom haifanyi chochote kuhakiki usahihi wa namba za kitambulisho.

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.