Shule 2,715 Kuunganishwa na Mtandao wa Intaneti Nairobi

Shule 2,715 jijini Nairobi, Kenya hivi karibuni zitaunganishwa na mtandao wa intaneti wa bure:

Wanachi Group [kampuni] imefikia makubaliano ya kutekeleza mradi wa thamani ya Dola za Marekani milioni 3 (Takribani KSh milioni 270) na kaunti ya Nairobi, ili kuunganisha shule 2,715 jijini Nairobi na mtandao wa intaneti.

Mradi huo ulizinduliwa leo na ifikapo mwezi Juni mwaka huu (ndio, ndani ya miezi mitatu), shule 245 za mfano zinatarajiwa kuwa zimeunganishwa tayari. Baada ya hapo, mradi huo utatathiminiwa na awamu ya pili itaanza ndani ya miaka mitatu hadi mitano.

“Pamoja na mtandao wa bure wa intaneti, kampuni hiyo itaipatia kila shule vifaa vya kidijitali kwa ajili ya kuunganisha televisheni kwa ajili ya matumizi ya kupata maudhui ya elimu kwa njia ya sauti kwa faida ya wanafunzi. Watoto wa shule za awali watapata vifaa hivyo pia ikiwa ni pamoja na televisheni ndogo,” ilisema taarifa ya kampuni hiyo ya Wananchi.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.