Ndege ya Malaysia Haijulikani Ilipo Ikiwa na Abiria 239

Malaysian Airline. Flickr photo by planegeezer (CC License)

Ndege ya Shirika la Ndege ya Malaysia. Picha ya Flickr na planegeezer (CC License)

Siku ya Jumamosi ya Machi 8, mashirika ya habari duniani kote yaliripoti kuwa ndege ya Shirika la ndege la Malaysia iliyokuwa angani kuelekea China imepotea. Ndege hiyo MH370 ilikuwa ikitokea Kuala Lumpur kwenda Beijing ilipoteza mawasiliano na waongoza ndege, ambapo shirika la ndege pamoja na mamlaka zinazohusika zikishindwa kufahamu kwa hakika iliko ndege hiyo. Ilikuwa na abiria 227 na wafanyakazi 12 wa ndege 

Kwa mujibu wa gazeti la The Guardian, ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na kifaa cha kuongozea ndege ikiwa kwenye anga la Vietnam. 

Shirika la ndege hiyo limekuwa likiandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kutoa habari kuhusu mwenendo wa mambo, ikiwa ni pamoja na tamko lililotolewa na Mkurugenzi wake Mkuu  Ahmad Jauhari Yahya: 

Tunasikitika sana kuwa tumepoteza mawasiliano yote na ndege namba MH370 iliruka kutoka Kuala Lumpur saa 6.41 usiku wa manane ikielekea Beijing. 

Ndege hiyo ilikuwa itue kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Beijing saa 12.30 asubuhi kwa saa za Beijing. 

Kituo cha Kuongozea ndege cha Subang  kilitoa taarifa kuwa kimepoteza mawasiliano saa 8.40 usiku (kwa saa za Malaysia) leo. 

Ndege MH370 ilikuwa aina ya Boeing B777-200.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba jumla ya watu 239 na wafanyakazi -hiyo ikiwa ni abiria 227 (watoto 2), na wafanyakazi 12. Abiria walikuwa wa mataifa 13 tofauti. 

Shirika la Ndege la Malaysia kwa sasa linafanya kazi kwa karibu na mamlaka ambao wanaendelea na zoezi la utafutaji na uokoaji kujaribu kujua ndege hiyo iko wapi.

Timu yetu kwa sasa inawapigia simu warithi wa abiria na wafanyakazi.

Taarifa nyingine kwa vyombo vya habari iliyotolewa na shirika hilo la ndege limemtambua rubani wa ndege hiyo kuwa ni Captain Zaharie Ahmad Shah, ambaye ana  masaa 18,365 ya kurusha ndege kwenye mkanda wake. 

Kwenye mtandao wa Twita, watu wengi wameonyesha wasiwasi na hofu: 

Kuna taarifa kuwa ndege ya Malaysia imeanguka lakini hakuna taarifa rasmi za kuthibitisha hilo

Ndege ya Shirika la ndege la Malaysia iliyopotea ndicho hasa kinachonifanya niogope kusafiri kwa ndege

Naweza kujiapiza kuwa ndege ya Shirika la Ndege la Malaysia haijaanguka na watu 239 walio kwenye ndege hiyo wako salama na wanaendelea vizuri

Habari za kusikitisha kuhusiana na tasnia ya usafiri wa anga na wale waliokuwepo kwenye ndege hiyo! Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Uingereza (BBC), Shirika la Ndege la Malaysia limepoteza mawasiliano na ndege yao iliyokuwa ikisafiri kuelekea Beijing

Tukio hilo limemfanya Waziri Mkuu wa Malaysia, Najib Razak kujibu kupitia mtandao wa Twita:  

Mawazo na maombi yangu yako na familia za wanaosafiri na ndege #MH370. Tumeagiza hatua zote zinazowezekana zichukuliwe

Shirika la Habari la Reuters sasa limeripoti kuwa ndege hiyo ilianguka kwneye Bahari za China Kusini, hata hivyo, hakuna tangazo rasmi lililotolewa wakati wa kuandikwa kwa makala haya.  

1 maoni

  • Kiungo cha makala haya kutokea kwenye tovuti nyingine: Ndege ya Malaysia Haijulikani Ilipo Ikiwa na Abiria 239 | TravelSquare

    […] Ndege ya Malaysia Haijulikani Ilipo Ikiwa na Abiria 239 Ndege ya Shirika la Ndege ya Malaysia. Picha ya Flickr na planegeezer (CC License) Siku ya Jumamosi ya Machi 8, mashirika ya habari duniani kote yaliripoti kuwa ndege ya Shirika la ndege la Malaysia iliyokuwa angani kuelekea China imepotea. Ndege hiyo MH370 ilikuwa ikitokea Kuala Lumpur kwenda Beijing ilipoteza mawasiliano na waongoza ndege, ambapo shirika la ndege pamoja na mamlaka zinazohusika zikishindwa kufahamu kwa hakika iliko ndege hiyo. Ilikuwa na abiria 227 na wafanyakazi 12 wa ndege  Kwa mujibu wa gazeti la The Guardian, ndege hiyo ilipoteza mawasiliano na kifaa cha kuongozea ndege ikiwa kwenye anga la Vietnam.  Shirika la ndege hiyo limekuwa likiandika kwenye ukurasa wake wa Facebook kutoa habari kuhusu mwenendo wa mambo, ikiwa ni pamoja na tamko lililotolewa na Mkurugenzi wake Mkuu  Ahmad Jauhari Yahya:  Tunasikitika sana kuwa tumepoteza mawasiliano yote na ndege namba MH370 iliruka kutoka Kuala Lumpur saa 6.41 usiku wa manane ikielekea Beijing.  Ndege hiyo ilikuwa itue kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Beijing saa 12.30 asubuhi kwa saa za Beijing.  Kituo cha Kuongozea ndege cha Subang  kilitoa taarifa kuwa kimepoteza mawasiliano saa 8.40 usiku (kwa saa za Malaysia) leo.  Ndege MH370 ilikuwa aina ya Boeing B777-200. Ndege hiyo ilikuwa imebeba jumla ya watu 239 na wafanyaka… Kusoma makala kamili  »  http://sw.globalvoicesonline.org/2014/03/ndege-ya-malaysia-haijulikani-ilipo-ikiwa-na-abiria-239/ […]

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.