Uvumbuzi: Kompyuta Inayotumia Nishati ya Jua Nchini Mali

Limmorgal, a low power PC made in Mali via Tech of Africa with permission

Limmorgal, Kompyuta inayoendeshwa kwa nishati ya jua iliyotengezwa nchini Mali na Kampuni ya Tech of Africa kwa ruhusa

Kama sehemu ya mfululizo wetu juu ya teknolojia na ugunduzi unaofanyika Afrika, hivi karibuni tulionyesha Mashine ya Kuchapishia picha zenye umbo halisi yaani 3D iliyotengenezwa kutokana na taka pepe nchini Togo na mashine ya kukagua usahihi wa maneno katika lugha ya spell ki-Bambara . Leo, tunawaletea kompyuta ya kwanza kutumia umeme mdogo iliyotengenezwa nchini Mali. Kompyuta hiyo inayoitwa Limmorgal (ikiwa na maana ya kikokotozi kwa lugha ya ki-Peul) ni zao la bongo za vikundi viwili vya raia wa Mali, Jumuiya ya Intaneti Mali (ISOC Mali) na Intelec 3. Mamadou Iam Diallo, rais wa ISOC Mali, anaeleza mahitaji wanayohitaji kuyatatua kwa kutumia kompyuta hiyo akiongea na Blogu ya Bamako[fr]:

Nous avons conçu cette machine pour contribuer à la réduction du fossé numérique, mais également à la vulgarisation de l’outil informatique surtout en milieu scolaire. Limmorgal est aussi un ordinateur adapté à l’alimentation par l’énergie solaire grâce à sa faible consommation d’énergie.

Tulibuni kompyuta hii kusaidia kupunguza pengo kati ya walio mtandaoni na wale wasiomudu huduma za kidijitali, lakini pia  upanuzi wa matumizi ya kompyuta mashuleni. Limmorgal ni kompyuta ilitengenezwa mahususi kutumia umeme wa nishati ya jua na inatumia nishati kidogo sana (Watt 24 tu zinahitajika).

Sifa za kompyuta hiyo ni kama ifuatavyo :

  • Mfumo wa Ufanyaji kazi (Operating system): Ubuntu (zana huru) 
  • Uwezo wa kutafuta ni 1.4 G Hertz
  • 1GB RAM
  • Bei : 171000 Fcfa (Tsh 650,000 hivi)

2 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.