PICHA: Makanisa Yanalia Nchini Misri

Mtetezi wa haki za wanawake nchini Misri Dalia Aziada aliposti twiti hii  baada ya makanisa kadhaa ya wakristo kuteketezwa katika maeneo mbalimbali nchini Misri kufuatia operesheni ya kikatili  iliyofanywa na jeshi Agosti 14 2013, iliyokusudia kuwatoa wafuasi wa chama cha Udugu wa Ki-islamu kutoka makao ya makambi katika mji mkuu wa Cairo, ambapo wamekuwa wakidai kurejeshwa madarakani kwa rais Morsi kwa wiki kadhaa.

Operesheni hiyo ya kuwaondoa wafuasi hao ilisababisha vifo vya watu wasiopungua 638 kwa mujibu wa serikali ya Misri. Msemaji wa chama cha Udugu wa ki-Islamu amesema watu 2,000 waliuawa katika “mauaji hayo ya halaiki”.

Makumi kadhaa waliuawa mnamo Agosti 16, wakati wafuasi wa Udugu wa ki-Islamu walipokuwa wakipambana na vikosi vya usalama katika “Siku ya hasira.”

 Soma zaidi katika Habari zetu MaalumUmwagaji wa damu nchini Misri.

 

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.