Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania

Photo of the clashes, uploaded by Abo Bakr Ahmado on his Facebook

Picha ya mapigano, iliyowekwa na Abo Bakr Ahmado kwenye ukurasa wake wa Facebook

Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara kwenye makampuni ya machimbo ya madini katika nchi za Kiarabu (ARMICO). Wafanyakazii hao waliandamana kuelekea kwenye makao makuu ya utawala wa jimbo hilo, majengo ya mmoja wapo wa makampuni ya wakandarasi, pamoja na majengo ya kituo cha redio ya taifa. Jeshi [ar] liliingilia kati kudhibiti hali hiyo na kuyatawanya maandamano hayo.

Mwanaharakati Magdy Ahmed alitwiti kuhusu kutoroka kwa gavana wa Tiris Zemmour baada ya wafanyakazi kuandamana [ar]:

@mejdmr :والي ولاية زويرات الجنرال ول باهية و الوالي المساعد وشرطة المدينة يفرون أمام غضب عمال الجرنالية الذين اقتحمو مبني الولاية والإذاعة الجهوية

@mejdmr: Gavana, Ould Bahia, naibu gavana na polisi walikimbia baada ya kushuhudia hasira ya wafanyakazi hao kwa siku moja walipovamia ofisi ya gavana na kituo cha redio ya taifa.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.