PICHA: Maandamano ya Pamoja ya Watu wa Shia Nchini kote Pakistan Yamalizika Kwa Amani.

Maandamano ya mshikamano ya watu wa Shia yaliyoendeshwa kwenye takribani majiji 100 katika maeneo mbalimbali ya Pakistan hatimaye yamefikia tamati. Maandamano yalichochewa mara baada ya milipuko ya mabomu iliyowaua watu zaidi ya 100 wa jamii ya Hazara ya Shia katika jiji lililopo Kusini Magharibi mwa jiji la Quetta mnamo Januari 10, 2013.

Milipuko hiyo ya mabomu iliweka kumbukumbu ya miongoni mwa siku mbaya ya umwagaji damu katika historia ya jimbo la kusini Magharibi la Balochistan. Wanachama wa kikundi cha kijeshi kilichofutwa cha Laskher-e-Jhangvi walidai kuhusika na ukatili huo.
Kufuatia mashambulizi hayo, watu wa jamii ya Hazara wa kutoka Quetta walikutana katika barabara ya Alamdar na kisha kuanzisha maandamano ya amani ya kukaa mahali pamoja na kuishinikiza serikali kusikiliza madai yao. Wakati picha zao zikisambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii zikiwaonesha wakiwa wamekaa huku wakinyeshewa na mvua iliyoambatana na barafu sambamba na majeneza ya ndugu zao, maandamano ya mshikamano kwa mtindo wa maandamano ya amani ya kukusanyika sehemu moja yalisambaa kama moto katika sehemu mbalimbali za nchi. Watu wa Pakistan kutoka katika makundi makuu ya dini pamoja na makabila yaliungana kupinga ugaidi katika jina la Uislam

Waandamanaji katika jiji la Quetta walikuwa na agenda moja tu:

“Jiji la Quetta liwekwe chini ya uangalizi wa Jeshi na iwe kama sheria ya utawala.”

Iliichukua serikali siku nne kujadili jambo hili; hatimaye ilituma ujumbe kuashiria kusitishwa kwa maandamano ya siku nne ya kukaa mahali pamoja. Zaidi, ndugu wa marehemu walikataa kuzika miili ya ndugu zao waliofariki mpaka pale madai yao yatakapotatuliwa. Kwa kuwa maandamano yameshasitiswa, waliofariki sasa wanazikwa.

Raia walipanga maandamano ya kuishinikiza serikali kutatua madai yao katika maeneo yote ya nchi ya Pakistan. Maandamano yalifanyikia katika barabara kuu za treni na katika barabra kuu za magari. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, maandamano yalianzishwa kwenye zaidi ya majiji 100 na katika miji kadhaa. Maandamano pia yalianzishwa katika jiji la Skardu, ambapo jotoridi wakati wa usiku lilifikia nyuzijoto hasi 14. Lengo lilikuwa rahisi:

Kubaliana na matakwa ya waandamanaji wa Quetta.

Kinachofuata ni muonekano katika picha wa baadhi ya maandamano katika miji mikuu ya Pakistan:

Karachi

Protest infront of Bilawal House against Shia Killing.

Maandamano mbele ya nyumba ya Bilawal ya kupinga mauaji ya Shia. Chanzo: ‏@ArsalanMKhan

Protest infront of Bilawal House against Shia Killing. Source: FacebookSyed Sabih Abbass Rizvi</a>. Copyight: Used with author's permission

Maandamano mbele ya nyumba ya Bilawal ya kupinga mauaji ya Shia. Haki miliki: FacebookSyed Sabih Abbass Rizvi. Used with permission

Protest at Karachi Press Club.

Maandamano katika klabu ya vyombo vya habari ya KarachiProtest at Karachi Press Club. Chanzo: @‏faisalkapadia

A child during a protest near Numaish Chowrangi.

Mtoto wakati wa maandamano ya mshikamano wa waShia karibu na Numaish Chowrangi. Chanzo: @arifaBatool

Ifuatayo ni video maandamano ya Numaish, Karachi.

Hyderabad

Protest near Hyderabad Bypass.

Maandamanno karibu na barabara ndogo ya Hyderabad. Chanzo: ‏@ImZeesh

Lahore

#WeAreAllHazara protests in Lahore.

# Sisi sote ni waandamanaji wa Hazara katika Lahore. Muda: saa nane usiku. Chanzo: ‏@XumarShirazi

Protest infront of Governor House Lahore. Time: 11:30 pm.

Maandamano mbele ya nyumba ya Gavana wa Lahore. Muda: 5:30 usiku. Chanzo: Qurrat-ul -in Haider (‏@mojesma)

A young Shia girl asking her "Sunni Brothers" to join the protest.

Msichana mdogo wa Shia akiwaomba “kaka zake wa Sunni” kujiunga na maandamano. Chanzo: ‏@annyzaidi

Sit in continues all night.

Maandamano ya kukusanyika sehemu moja yaendelea usiku kucha. Chanzo: FaceBookTaimour Mubashar

Islamabad

Women and children during a peaceful sit-in.

Wanawake na watoto wakati wa maandamano ya pamoja ya kuishinikiza serikali kusikiliza matakwa yao. Chanzo: ‏@Zulfi25

Trying their best to fight the cold climate.

Wanajitahidi kwa kadiri wawezavyo kukabiliana na hali ya hewa ya baridi kali. Chanzo: ‏@Mehr_Shah

Peshawar

A youngster participates in the protest.

Mtoto mdogo akishiriki katika maandamano. Chanzo: ‏@Khushal

Peshawar Sit-in.

Maandamano ya Peshawar. Chanzo: Hassan Turi (‏@spin_ghar)

Quetta

People sitting in Quetta with the cadaver of their loved ones.

Watu wakiwa wamekaa na maiti za wapendwa wao huko Quetta. Chanzo: Humayoun Behzad (‏@behzadjee)

Hunger strike organized by Hazara Development Party (HDP) in Quetta.

Maandamano makubwa yaliyoanzishwa na Chama cha Maendeleo cha Hazara (HDP) huko Quetta. Chanzo: Humayoun Behzad (‏@behzadjee)

People sitting firm. Night temperature in Quetta stays below zero degree centigrade.

Watu wakiwa imara. Jotoridi wakati wa usiku huko Quetta likiwa bado ni chini ya nyuzijoto sifuri. Chanzo: Humayoun Behzad (‏@behzadjee)

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.