Le Potentiel anaandika kwamba [fr] tathmini ya Uvunjaji wa Haki za Binadamu nchini DRC Kongo iliyofanywa na Rais wa Ufaransa Hollande haikuchukuliwa kijuu juu na serikali ya Kongo wakati ambapo Mkutano wa nchi zizungumzazo Kifaransa ndio kwanza umeanza mjini Kinshasa, DRC. SErikali hizi mbili zinaonekana kutofautiana sana kuhusu mambo kama kifo cha mtetezi wa Haki za Binadamu Ndg Chebeya, tume ya taifa ya uchaguzi na uhitaji wa kamati itakayosimamia masuala ya haki za binadamu.