Misri: Waandamanaji Watuma Ujumbe Dhidi ya Udhalilishaji wa Kijinsia.

Nchini Misri, udhalilishaji wa kijinsia ni tatizo kubwa, na ndilo jambo linaloongozwa kupingwa na Wamisri. Maandamano yalifanywa na vijana wadogo wa Misri, wasichana kwa wavulana katika mji mdogo wa Nasr jijini Cairo mnamo tarehe 4 Julai kwa lengo la kutuma ujumbe kupinga udhalilishaji wa kijinsia.

Tangu mapinduzi yalipofanyika, Wamisri wanaotumia mtandao wa intaneti na wasiotumia mtandao wa intaneti wamekuwa wakisimama imara kupinga udhalilishaji wa kijinsia pamoja na machafuko yatokanayo na kutokujali usawa wa binadamu. Mwezi Juni matembezi ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia yalishambuliwa. Haikujalisha, harakati za kukabiliana na udhalilishaji huo zinaendelea.

Malengo ya maandamano ya Julai 4 yalilenga kuweka msimamo kuhusu kupinga udhalilishaji wa kijinsia na kudai usalama wa mitaa kwa wote. Maged Tawfiles alikuwepo kwenye tukio na alipiga picha zifuatazo (picha zote zimetumika kwa ruhusa):


“Uhuru wangu ni utu wangu”


“Mwanamke yeyote wa Misri ana haki ya kutembea kwa uhuru”


“Sihitaji kuchukia kwa mimi kuwa msichana”


“Natamani kama ungeacha kuangalia mwili wangu”


“Nahitaji kuendesha baiskeli bila kudhalilishwa”


“Sidhalilishi ili na dada yangu asidhalilishwe”


“Jitambue mwenyewe, sio mavazi yangu”


“Mtaa siyo wako, uhuru wangu siyo wako”

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.