Misri: Maandamano ya Kukomesha Udhalilishaji wa Kijinsia Yavamiwa

Maandamano yaliyokusudia kudai kusitishwa kwa vitendo vya kubughudhiwa yaligeuka kuwa shubiri baada ya wanawake waliokuwa wanahusika nayo kushambuliwa na kikundi cha wanaume wenye hasira katika viwanja vya Tahrir leo (June 8, 2012). Watu walioshuhudia tukio hilo walielezea maoni yao kupitia twita.
Mwandishi wa habari aliyeshuhudia tukio hilo Sarah El Deeb, anaelezea kilichotokea kupitia twiti hii:

@seldeeb: Udhalilishaji kwenye maandamano hayo ulifanywa na wanaume wengi –lengo lilikuwa kuyavunja, kuwatukana na kuwadhalilisha washiriki

@seldeeb: Wanaume waliokuwa kwenye maandamano walijihami dhidi ya wavamizi lakini idadi yao ilikuwa kubwa na baadhi ya wanawake walibanwa

@seldeeb: Watu kwenye eneo la tukio walifanywa kituko na wavamizi hao na wengine wakafunga maduka yao kwa sababu ya hali kuonekana kutokuwa shwari. Mwishowe duka moja likatoa hifadhi

@seldeeb: Baadhi ya mashuhuda wanasema watu waliozunguka maandamano hayo walikuwa wakiwatukana wasichana waliokuwa wanaandamana kabla mapigano hajayaanza

May your hand be severed. No to sexual harassment, reads a sign held at the protest. Photograph by Sarah El Deeb

Mikono yenu ikatwe. Tunasema hapana kwa udhalilishaji wa kijinsia, linasomeka bango moja kwenye maandamano. Picha imewekwa kwenye mtandao wa twita na Sarah El Deeb


Taarifa za udhalilishaji wa kijinsia zimeendelea kumiminika kwenye miezi kadhaa za maandamano. Amira Howeidy anaonyesha muktadha:

@amirahoweidy: kuwadhalilisha kijinsia waandamanaji wa kike kulivyoanza kutokea wakati wa chama cha NDP cha Mubarak tangu mwaka 2005

Turk4Syria anauliza kama kuna mtu amewekwa ndani kwa kuwadhalilisha wanawake na Mohamed Yahia anajibu:

@MohammedY: @Turk4Syria hakuna aliyekamatwa. Imepangiliwa kiufundi kiasi kwamba wengi wanahisi ghasia hizi zilianzishwa na wale walio madarakani kuwatisha waandamanaji wa kike

Sherine Thabet anapendekeza[ar]:

@sherinethabet: ‬‏ الجملة اللي بقولها في كل حتة مع اي حد، المتحرش مش هايسمع الكلام، المتحرش مش هاتقدر توعيه، المتحرش لازم يكش، لازم المجتمع ينبذه، بس
Sentensi ninayoirudia kila mahali ninapoongea na kila mtu ni: wadhalilishaji hawatasikiliza tena. Wadhalilishaji hawataelimika. Wanapaswa kutoweka na njia pekee ya kufanya hivyo ni pale jamii itakapowakataa. Ndivyo inavyopaswa kuwa.

Na Deena Adel anahitimisha:

@deena_adel: Je, tunaweza kutumia hali hii ya kuongezeka kwa hasira baada ya udhalilishaji huu ili kuchukua hatua za kupambana nao?

Miitikio zaidi inapatikana kupitia alama hii
#EndSH kwenye mtandao wa twita.

1 maoni

jiunge na Mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.