Mapema siku ya Alhamisi tarehe 23 Septemba watu wa Colombia waliamka na taarifa ya habari hii: Siku iliyopita, ndege 30 na helikopta 27 za jeshi la Anga la Colombia zilivamia kambi ambamo Víctor Julio Suárez, ambaye anajulikana zaidi kama Jorge Briceño or Mono Jojoy, mmoja wa viongozi wa juu wa Majeshi ya Ukombozi wa Colombia (FARC), alikuwa amejificha pamoja na dazeni za wapiganaji gorila karibu na La Macarena, Meta. Suarez, mwenye umri wa miaka 57, aliuwawa katika kile kilichoitwa “Operesheni Sodoma”, kama ambavyo Rais Juan Manuel Santos alivyothibisha [es] kutokea mjini New york, ambako alikuwa akihudhuria mkutano wa Baraza la umoja wa mataifa. Askari watano wa majeshi ya Usalama walijeruhiwa na mbwa wa kike wa polisi aliuwawa [es].
Viongozi wengine wa juu wa wapiganaji hao gorila inawezekana kuwa walikamatwa ndani ya kambi hiyo yenye ukubwa wa mita za mraba 30 – ambayo inataarifiwa kuwa [es] ilikuwa na [es] mahandaki ya kuishi chini ya ardhi – na majeshi ya ulinzi ya Colombia (ambayo yalijumuisha zaidi wanajeshi wa jeshi la Colombia pamoja na Jeshi la Polisi la Taifa ambalo lilitua baada ya mapigano kumalizika) yanawafanyia utambulizi wakati makala hii ikiwa inaandikwa. Mnamo majira ya mchana siku ya Alhamisi vyanzo visivyo rasmi vilidai kuwa kiongozi wa FARC Henry Castellanos, Romaña, naye pia aliuwawa [es] katika operesheni hiyo.
Mono Jojoy, ambaye alitoswa na mdukizi, alikuwa akichukuliwa kama kiongozi wa upande wenye siasa kali katika jeshi la FARC na alikuwa kamanda wa Kanda wa Mashariki. Aliaminika kama “mmoja wa wapiganaji gorila mwenye uchu wa damu” [es],kulikuwa na hati 62 za kuamrisha kukamatwa kwake, aliwahi kuhukumiwa mara 5, na Marekani ilikwishaomba kukamatwa na kusafirishwa kwa mtu huyo kwenda Marekani kujibu tuhuma zinazohusiana na usafirishaji madawa ya kulevya, na iliahidi kutoa zawadi kwa kukamatwa kwake.
Utata uliibuka pale ambapo El Tiempo, gazeti la kila siku lenye wasomaji wengi zaidi nchini humo (ambalo linamilikiwa kwa kiasi na familia ya Rais Juan Manuel Santos’ ), lilipotuma mfululizo wa twita kuhusu habari hii:
Vigilantes de parqueadero en Corferias: ‘Hay que pedir la tarde libre para celebrar la muerte de Jojoy’
¿Cómo están celebrando en sus oficinas o donde se encuentren la muerte de Jojoy?
Para los ofendidos por la pregunta de celebración, disculpas. Mejor pregunta es: ¿Cómo reaccionan por la muerte de Jojoy?
Watumiaji wa Twita walijibu mara moja jumbe hizo za twita. Miguel Olaya (@juglardelzipa) alisema:
por ahora no nos han dado el día libre en la universidad de los andes. @eltiempocom debería denunciarlos por no ser patriotas.
Mtumiaji mwenye jila la @PAPerezA alilikosoa gazeti hilo::
Que ignorancia y amarillismo!! Salvajes!! […]
Agnes Dantés (@Agnes_Dantes) alifanya mzaha:
Ayy esos de @eltiempocom son muy jocosos. Pero bueh… bien por ellos que no nos engañan con falsa imparcialidad y profesionalismo
Kwa kejeli, Clo Calao(@cloquis) aliandika:
Hay unos desplazados al frente de mi casa pidiendo limosna, les voy a preguntar a ellos como celebran la muerte de #jojoy #eltiempostyle
Adriana (@Adridice) aliandika maoni kuhusu ombi la msamaha lililotumwa na El Tiempo:
las disculpas del @eltiempocom dejan mucho que desear “a los que se sientan ofendidos” que amarillismo, están peor que el espacio
Wengine walilitania jina la operesheni, ambalo kwa mujibu wa Waziri wa Ulinzi Rodrigo Rivera lilichaguliwa [es] kwa sababu “kiini cha uovu kilikuwa pale. Na tulihitaji msaada kutoka mbinguni.” Orlando (@DanielitoBang) alisema:
Alejandro Ordóñez abrirá investigación contra Rodrigo Rivera y la cúpula militar por usar el aberrante nombre de Sodoma en esta operación.
Ramírez Jaramillo (@egolaxista):
La película de la Operación Sodoma será clasificada R, porque su nombre es sugestivo
Kwa mzaha tu, Miguel Olaya (@juglardelzipa) aliandika:
en el ministerio de defensa organizan focus groups para decidir el nombre de las operaciones.
Alvaro Sáenz (@AlvarettoS):
:o que el mono jojoy murió de sodomía? #toomuchinformation
Maoni mengine katika twita yanashabihi masuala yaliyopo katika siasa za Colombia. Manuel Carreño (@Popcultura) alielekeza ujumbe wake kwa wale wanaoipinga serikali ya sasa na ile iliyopita:
Amigo antiuribista: alegrarte por esta noticia no te vuelve de derecha: solo demuestra que te alegras por la muerte de cafres como ese.
Lakini Juan C. Rodríguez (@JCRodriguezMD) hadhani kwamba matokeo ya operesheni hii ni ishara ya kuwa serikali imefanikiwa:
El éxito de un gobierno no se mide por número de bajas, sino por el bienestar de su población. En eso si seguiremos muy mal.
Mtumiaji wa twita @Vulturno alisema:
Sin duda es el logro más grande de las FFMM, con todo y que les tocó matarlo de lejos y con sevicia
Daniel Arango (@stultaviro) alielezea mafanikio ya operesheni hii yanamaanisha nini kwa watu wa Colombia:
Qué buena bofetada a los que andaban anunciando y celebrando el fracaso de la Seguridad Democrática.
Katika ujumbe wake wa twita, Alejandro Gaviria (@agaviriau) anahusisha [kifo hicho] na dhana ya haki:
No es la muerte lo que alegra a la mayoría de la gente: es la idea o la sensación de justicia.
Lakini Orlando (@DanielitoBang) anafikiri kuwa haki haikutekelezwa vilivyo:
Qué rabia que mueran tipejos como ese. Se siente cierta sensación de justicia, pero el miserable en realidad murió impune.
“El Chiflamicas” (@elchiflamicas) aliandika:
Si no mataban al Mono Jojoy se les hubiera escapado por algún aeropuerto.
Alieth Acosta (@_InTheMood) alikosoa shinikizo [lililojitokeza] la kuonyesha uzalendo:
Si no pongo una bandera de Colombia en mi nick de bb soy terrorista entonces? Esas bobadas.
“La Morenita” (@lapetitebrune) alisema:
El día en que celebremos la vida, en vez de la muerte, ese día sí habrá esperanza para nosotros.
Makala nyingine zinazohusiana na hii:
- Colombia: FARC leader “Sureshot” is Confirmed Dead (30 May 2008)
- Colombia: Reward for FARC Guerrilla for Killing His Commander (21 March 2008)
- Colombia: The Unsettling Conflict with Ecuador and Venezuela (5 March 2008) [related special coverage]