Cuba: Ukweli wa Sanchez Kutiwa Mbaroni Waibuka

Kukamatwa, kupigwa na kuachiwa huru kulikofuata kwa wanablogu Yoaní Sánchez, Claudia Cadelo na Orlando Luis Pardo kulikofanywa na majeshi ya usalama ya Cuba tarehe 6 Novemba, kunapata matangazo mengi katika vyombo vikubwa vya habari na katika ulimwwengu wa blogu pamoja na ule wa Twita. Yoani ameandika (es) kuhusu tukio hilo kwenye blogu yake, Generación Y, na blogu za Kiingereza kama vile Babalú Blog, Repeating Islands pamoja na Uncommon Sense zinafuatilia habari hiyo. Mahojiano ya sauti (es) na Sanches kuhusu tukio hilo yamepandishwa kwenye YouTube.

Anza mazungumzo

Mwandishi, tafadhali jiandikishe »

Miongozo

  • Tafadhali wape heshima watumiaji wengine. Maoni yenye lugha ya chuki, matusi na mashambulizi binafsi hayataruhusiwa.