Christian Bwaya
24 jumbe, alijiunga 2009-05-18
Ni mwanafunzi wa Baolojia, mpenzi wa lugha ya kiswahili. Muda wangu za ziada huutumia kusoma na kuandika. Ninayo blogu niitayo Jielewe (http://bwaya.blogspot.com) ambapo hujadili pamoja na masuala mengine falsafa, sayansi, dini na saikolojia. Nafikiri kutumia sehemu kubwa ya maisha yangu kuandika na kujitolea kwa ajili ya jamii yangu na ndio maana nikajiunga na Lingua Swahili.
Deogratias Simba
27 jumbe, alijiunga 2008-07-29
Ni mpenzi wa lugha ya Kiswahili. Licha ya kuwa ni mhariri na mwandishi wa vitabu, mimi pia ni mfasiri. Nafasiri maandiko kutoka lugha ya Kiingereza kuja Kiswahili na kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Pia ni mwanablogu: http://simbadeo.wordpress.com Ndiyo kusema kuwa ninapenda kuperuzi kwenye kurasa za mtandaoni ili kuilisha akili kwa habari mbalimbali zinazojiri huku na huko duniani. Ni raia wa Tanzania na mkaazi wa Dar es Salaam. Karibu.



