<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Fri, 06 Nov 2009 13:29:03 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Irani: Vuguvugu la Kijani Laupinga Utawala Tena</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:29:03 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Farsi]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Iran]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Protest]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=552</guid>
		<description><![CDATA[Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba uliendesha maandamano makubwa ambapo maandamano hayo yalikabiliwa na matumizi makubwa ya nguvu ya kuyazuia yaliyofanywa na vikosi vya usalma. Kama ambavyo sasa inatarajiwa, uandishi wa habari wa kiraia nchini Irani haukukosa kitu kwani ulirekodi 'historia' hiyo kupitia simu zao za mikononi. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/hamid-tehrani/">Hamid Tehrani</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/iran-green-movement-defies-regime-again/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/13aban.jpg" class="alignleft" width="200" height="269" /><br />
Upande wa upinzani wa Vuguvugu la Kijani nchini Irani mnamo tarehe 4 Novemba mwaka huu (13 ya Abani) <a href="http://www.guardian.co.uk/world/blog/2009/nov/04/iran-student-day-protests">uliendesha</a> maandamano makubwa ya mitaani, baada ya kutumia fursa ya maandamano rasmi yaliyoendeshwa siku hiyo ya kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 30 ya ukaliaji wa Ubalozi wa Marekani jijini Teherani.  Maandamano hayo ya upinzani yalikabiliwa na matumizi ya nguvu kupita kiasi ya kuyavunja yaliyofanywa na vikosi vya usalama.</p>
<p>Kama ambavyo sasa imekuwa jambo la kutarajiwa, vyombo vya habari vya kiraia vya Irani vilirekodi &#8216;historia&#39; hiyo kupitia simu zao za mkononi.</p>
<p>Waandamanaji jijini Teherani walikanyagakanyaga picha ya Kiongozi Mkuu wa Kidini nchini humo, Ayatollah Ali Khamenei, kitendo ambacho wala kisingefikiriwa miezi michache tu iliyopita. </p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/ROBiaGs7OYo&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/ROBiaGs7OYo&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Ujumbe kwa Obama: Ama uko upande wetu au uko upande wao.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/x-yLLZ3JGfM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/x-yLLZ3JGfM&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Kiongozi wa upinzani, Mehdi Karoubi, akiwa katikati ya watu.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/UuGNPxkIXU4&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/UuGNPxkIXU4&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
<p>Vikosi vya Usalama vikishambulia waandamanaji.</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/AIiAopKXE7w&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/AIiAopKXE7w&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/irani-vuguvugu-la-kijani-laupinga-utawala-tena/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Amerika ya Kati: Kasi Kubwa ya Ueneaji wa Jangwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:24:23 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Chile]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Environment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=556</guid>
		<description><![CDATA[Ueneaji wa jangwa unasambaa kimyakimya lakini kwa kasi kubwa mahali pengi duniani na Amerika ya Kati haijaweza kukwepa hali hii iliyo na athari mbaya za kutisha. Wakati ambapo majangwa ni maumbo ya asili, ueneaji wa jangwa ni mchakato wa kuharibika kwa nyanda za ardhi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa na uharibifu unaofanywa na binadamu. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/belen-bogado/">Belen Bogado</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/  '>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Pengine maneno ueneaji jangwa yanaweza kusikika sawa na jangwa, lakini kuna tofauti kubwa ya msingi kati ya maneno hayo: wakati ambapo majangwa ni moja kati ya maumbo mazuri ya kipekee ya asili, ueneaji jangwa ni mchakato wa kuharibika ambako kanda za ardhi hupitia baada ya kuathiriwa vibaya na mabadiliko ya hali ya hewa, shughuli za binadamu na majanga ya asili mpaka hatimaye zinageuka na kuwa majangwa.</p>
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 410px"><img alt="Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons." src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/desertification.jpg" title="desertification" width="400" height="258" /><p class="wp-caption-text">Picha na Macnolete na inatumika chini ya leseni ya Creative Commons.</p></div>
<p>Ingawa athari ya mabadiliko ya hali ya hewa katika ueneaji jangwa bado haijaeleweka vema, yaani kwa mujibu wa GreenFacts, inafahamika kwamba <a href="http://www.greenfacts.org/en/desertification/index.htm">viwango vya juu vya joto vinavyotokana na kuongezeka kwa viwango vya dioksidii ya kaboni kunaweza kuwa na athari mbaya kutokana na kuongezeka kwa upotevu wa maji kutoka ardhini na kupungua kwa viwango vya mvua katika maeneo yenye ukame</a>. Wakati huohuo ueneaji jangwa nao huchangia katika mabadiliko ya hali ya hewa kwa kuruhusu kaboni iliyohifadhiwa kwenye mimea ya maeneo yenye ukame na udongo kurushwa kwenye anga.</p>
<p>Ueneaji jangwa unazidi kuwa na athari mahali pote duniani. Kwa sasa hivi ueneaji huo unaathiri mavuno, unasababisha kupanda kwa bei za vyakula vilivyopo, na katika baadhi ya maeneo, hata wanyama wanakufa. Watu wanalazimika kuhamia maeneo mengine ya mbali na nyumbani kwao, kama anavyoeleza mwanablogu Miguel Angel Alvarado anayetokea El Salvador <a href="http://www.ecoportal.net/content/view/full/61308/">kuhusu mpango wa kuhamisha makazi ya rais kwa sababu ya ueneaji jangwa[es]</a>:</p>
<blockquote><p>El traslado de casa presidencial, del Barrio san Jacinto al local en donde estaba el Ministerio de Relaciones exteriores, según informes extrajudiciales, obedece a la prevención del ejecutivo ante un posible hundimiento del suelo generado por cárcavas en este sector.</p></blockquote>
<div class="translation">Kwa mujibu wa nyaraka zisizo rasmi kisheria, kuhamishwa kwa makazi ya rais kutoka maeneo ya San Jacinto kwenda ilipokuwa Wizara ya Mambo ya Nje hapo awali, ilikuwa ni hatua ya kujihami iliyofanywa na mhimili wa dola ili kuepuka kutitia kwa ardhi kutokana na makorongo yaliyotokea pale.</div>
<p>Bara lililoathiriwa zaidi ni Afrika, na jambo hili linaweza kuonekana zaidi nchini Kenya, ambapo moja ya sekta zinazoweza kupata athari kubwa za ueneaji jangwa na ukame ni wasichana. Pale maji yaliyohifadhiwa kwenye matenki yalipokuwa yametumika yote katika Nyumba ya Watoto Yatima ya Dago Dala Hera huko Magharibi mwa Kenya, akina mama wanaojitolea na watoto wanalazimika kuteka maji yasiyo salama kutoka katika mto ulio karibu kwa ajili ya kupikia na kunywa. <a href="http://us.oneworld.net/article/367320-africa-famine-deepens-drought-worst-decades">“Kwenda mtoni kuteka maji peke yao nyakati za jioni kunawaweka wasichana katika hatari ya kukumbana na wanaume wanaoweza kuwanyanyasa kingono,”</a> alisema Edwin Odoyo, ambaye mama yake anayeitwa Pamela ndiye aliyeanzisha makazi hayo ya watoto yatima.</p>
<p>Ingawa ueneaji jangwa una athari kubwa zaidi barani Afrika, hali ya mazingira ya Amerika ya Kati nayo inapitia mabadiliko makubwa, kama ilivyojadiliwa siku za karibuni katika Mkutano wa Tisa wa Kongamano kuelekea Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kukabili Ueneaji Jangwa uliofanyika jijini Buenos Aires, Ajentina. Mtaalamu wa Kiitaliano, Massimo Candelori, aliyekuwa mwakilishi wa Mkataba wa Kukabili Uenejaji Jangwa, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=esp&#038;idnews=3422">alisema katika mahojiano na  Tierramerica</a> kwamba hali ilivyo Amerika ya Kati inatisha kwa kuzingatia kwamba hakuna taarifa za kutosha kuhusu kiwango cha ueneaji jangwa katika eneo hilo. “Hatuna takwimu za sasa hivi. Moja ya lengo lililojadiliwa katika Mkutano wa Tisa lilikuwa ni kupata viashirio vinavyoturuhusu kuelewa vizuri zaidi hali halisi &#8230; takwimu tulizonazo mpaka sasa ni zile za miaka kumi iliyopita,” alisema Candelori.</p>
<p>Katika nchi za Amerika ya Kati ambapo kilimo na ufugaji ni moja ya sekta kuu za uchumi, ueneaji jangwa unaweza kuwa wa kimyakimya, lakini wenye madhara makubwa kama mnyama hatari mwindaji. Walau <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">asilimia 25 ya sehemu ya eneo zima</a> tayari imeharibiwa na wakati huohuo watu wanazidi kuwa na wasiwasi juu ya suala hili, kama inavyojionyesha katika blogu mbalimbali. </p>
<p><em>Eco Briefings [pt]</em>, blogu ya KiBrazili, inaonyesha kwamba <a href="http://ecobriefings.com/2009/10/05/desertificao/">WaBrazili waishio Kaskazini Mashariki mwa nchi wanashuhudia ueneaji wa kasi sana wa jangwa[pt]</a>:</p>
<blockquote><p>Mais um alerta está ligado. Temos pouco tempo para corrigir as coisas. (…)</p>
<p>No Brasil a desertificação tem avançado na caatinga, e zonas do polígono da seca no Nordeste e Norte de Minas Gerais, e também em Estados que antes não tinham áreas secas ou desertificadas como o Rio Grande do Sul. O Rio Amazonas viveu já uma grande seca a pouco tempo, grande com mortandade de peixes.</p></blockquote>
<div class="translation">Kiitia hatari kingine kinanguruma. Tuna muda mfupi sana wa kurekebisha mambo (…)</p>
<p>Nchini Brazili, ueneaji jangwa umeongezeka sana katika Caatinga, katika ukanda wa maeneo kame Kaskazini Mashariki na Kaskazini mwa jimbo la Minas Gerais, na vilevile katika majimbo ambayo hayakukumbwa na ukame wala ueneaji jangwa hapo kabla kama vile Rio Grande do Sul. Mto Amazon umepitia ukame mkubwa kabisa katika kipindi kifupi kilichopita, jambo lililosababisha samaki kufa kwa idadi kubwa.</p></div>
<p>Ajentina nayo ina maeneo kadhaa yaliyoathiriwa. Katika mkoa wa Valles Aridos, Kaskazini Mashariki, ambapo shughuli kuu ya kiuchumi ni ufugaji kondoo, inakadiriwa kwamba <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/11/04/latin-america-the-rapid-spread-of-desertification/www.inta.gov.ar/salta/info/documentos/Desertificaci%C3%B3n.pdf">katika miaka 100 iliyopita, walau watu 180,000 walilazimika kuhama. [es] (katika mfumo wa .pdf)</a>. Kusini mwa nchi ya Ajentina nako hakujapona na ueneaji jangwa. Mwanablogu Ailen Romero, anaandika maoni katika blogu inayoitwa <em>Geoperspectivas [es]</em> <a href="http://geoperspectivas.blogspot.com/2009/06/dia-mundial-de-la-desertificacion-2009.html">kwamba katika mkoa wa Patagonia, juhudi za serikali za kukabili ueneaji jangwa bado hazitoshi</a>:</p>
<blockquote><p>En la Patagonia, la amplitud del problema es de tal magnitud que ha comenzado a adquirir estado público. Pocos ignoran el tema, pero pocos tienen la posibilidad de actuar de alguna forma o con el conocimiento para hacerlo. El problema de la desertificación en el caso de la Patagonia supera a los planes que se han elaborado para combatirlo. Es por eso que no deben ahorrarse esfuerzos, ni limitar la imaginación de soluciones alternativas.”Si la geografía es la manifestación de la sociedad en el espacio físico, un espacio físico deteriorado refleja una sociedad deteriorada” afirman del Valle y Coronato(investigadores del Centro Nacional Patagónico)</p></blockquote>
<div class="translation">Katika Patagonia, ukali wa tatizo ni mkubwa kiasi kwamba umma wote umetambua tatizo hilo. Ni watu wachache tu ndiyo wanaolipuuza na ni wachache tu walio na nafasi au maarifa ya kufanya juhudi kulikabili. Tatizo la ueneaji jangwa huko Patagonia unazidi mipango iliyokwishaainishwa kulikabili. Ndiyo sababu kila juhudi haina budi kufanywa, wala kusiwe na mipaka katika kufikiria ufumbuzi mwingine wowote. ‘Kama Jiografia ni kielelezo cha jamii katika nafasi halisia, kuharibika kwa nafasi halisia huko kunaakisi kuharibika kwa jamii, wanasema  Valle na Coronato (watafiti kutoka katika Kituo cha Taifa cha Patagonia).</div>
<p>Huko Chile, ambapo <a href="http://www.conaf.cl/?seccion_id=8ad00d8dd61d22aa152575a1e5c08e58&#038;unidad=0&#038;PHPSESSID=db19e79870c9e01418e62b8576a26daf">takribani asilimia 62 ya eneo la taifa tayari imeathiriwa na ueneaji jangwa [es]</a>, mwanablogu Alfredo Erlwein alieleza wasiwasi kupitia katika blogu inayoitwa <em>El Ciudadano [es]</em>(Raia) kuhusu jinsi gani watu <a href="http://www.elciudadano.cl/2009/03/26/desertificacion-y-sequia-el-gran-problema-ambiental-de-chile-y-el-mundo/">wasiyo na maarifa ya kutosha kuhusu ueneaji jangwa</a>.</p>
<blockquote><p>
Efectivamente la desertificación es el problema ambiental más grave de Chile y muy poco conocido. Existen grandes zonas, como en la costa de la octava región, donde la erosión severa supera el 50% de la superficie: esto es que literalmente más de la mitad de los suelos se ha perdido por completo. En esas zonas se encuentran cárcavas de más de 50 metros de profundidad. Una tasa normal de formación de suelo puede ser de 0.2 cm por año, lo que evidencia la gravedad del asunto.</p></blockquote>
<div class="translation">Ueneaji jangwa kwa hakika ni tatizo kubwa kabisa lakini lisilofahamika miongoni mwa matatizo ya kimazingira nchini Chile. Kuna maeneo makubwa, kama vile pwani ya Nane ya Mkoa, ambapo mmomonyoko mkali wa udongo unazidi asilimia 50 ya ardhi: hii ina maana kwamba zaidi ya nusu ya ardhi imepotea, huo ndiyo ukweli. Katika maeneo hayo kuna makorongo yenye kina cha mpaka mita 50. Kiwango cha kawaida cha utengenezekaji ardhi ni kama sm 0.2 kwa mwaka, huo ndiyo uthibitisho wa ukali wa tatizo lililopo.</div>
<p>Kwa mujibu wa mtaalamu Mwitaliano Candelori, <a href="http://www.tierramerica.info/nota.php?lang=eng&#038;idnews=3207">kutumia udongo katika soko la Kaboni kutasaidia kupambana na ueneaji jangwa</a>; jambo hili pengine litaamuliwa katika Kongamano litakalofanyika jijini Copenhagen. Tayari kongamano hilo limeanza kuhesabiwa siku na ulimwengu unalisubiri kwa hamu.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/amerika-ya-kati-kasi-kubwa-ya-ueneaji-wa-jangwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kutambulisha Sauti Zinazotishwa</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 13:08:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Announcements]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger News]]></category>
		<category><![CDATA[Blogger Profiles]]></category>
		<category><![CDATA[Cyber-Activism]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Projects]]></category>
		<category><![CDATA[Software & Tools]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=554</guid>
		<description><![CDATA[Leo, kitengo cha utetezi cha Global Voices, kinazindua tovuti mpya inayoitwa Threatened Voices, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/sami-ben-gharbia/">Sami Ben Gharbia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/introducing-threatened-voices/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/threatened-logo-1.gif" title="threatened-logo" class="aligncenter" width="352" height="77" /><br />
Haijawahi kutokea hapo kabla kwamba watu wengi kiasi hicho wametishwa au kutupwa gerezani kwa sababu ya maneno wanayoandika kwenye mtandao.</p>
<p>Kwa kuwa wanaharakati wengi na raia wa kawaida wameongeza sana utumiaji wa Intaneti ili kutoa maoni yao na kuwasiliana na wengine, serikali nyingi pia zimeongeza ufuatiliaji wa kichunguzi, kujipenyeza, uchukuaji wa hatua za kisheria na unyanyasaji. Matokeo mabaya zaidi ya vitendo hivyo yanapata hasa msukumo wa kisiasa na hivyo kusababisha ukamataji wa wanablogu na waandishi wengine wa mtandaoni kutokana na shughuli zao za mtandaoni na nje ya mtandao, katika baadhi ya matukio ya kusikitisha hata vifo vimetokea. Waandishi wa habari wa mtandaoni na wanablogu wanawakilisha <a href="http://cpj.org/imprisoned/cpjs-2008-census-online-journalists-now-jailed-mor.php">asilimia 45 ya wanahabari </a>walio magerezani duniani kote.</p>
<p>Leo, <a href="http://advocacy.globalvoicesonline.org/">kitengo cha utetezi cha Global Voices</a>, kinazindua tovuti mpya inayoitwa <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Threatened Voices</a>, yaani, Sauti Zinazotishwa ili kusaidia kufuatilia unyamazishaji wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni. Inaonyesha ramani ya dunia na mwingiliano wa saa unaosaidia kuonyesha taarifa za vitisho na ukamataji unaofanywa dhidi ya wanablogu duniani kote, na ni mhimili mkuu wa kukusanyia taarifa kutoka katika asasi na wanaharakati walioamua kujitoa muhanga kwelikweli, zikiwemo <a href="http://www.committeetoprotectbloggers.org/">Committee to Protect Bloggers</a> (Kamati ya Kuwalinda Wanablogu), <a href="http://www.anhri.net/en/">The Arabic Network for Human Rights Information</a> (Mtandao wa Kiarabu wa Haki za Binadamu kwa Taarifa), <a href="http://rsf.org/">Wanahabari Wasio na Mipaka</a>, <a href="http://hrw.org/">Shrika la Kuchunguza Haki za Binadamu</a>, B<a href="http://cyberlaw.org.uk/">logu ya Sherika za Mitandao</a>, <a href="http://www.amnesty.org/">Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.cpj.org/">Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari</a>, <a href="http://advocacy.globalvoicesonline.org/">Kitengo cha Utetezi cha Global Voices</a>.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/threatened_voices1.jpg" title="threatened_voices" class="aligncenter" width="450" height="352" /></p>
<p><strong>Mwanablogu yupi, wapi?</strong></p>
<p>Kupata taarifa sahihi kuhusu wanablogu na waandishi wa mitandaoni waliokamatwa ni jambo gumu kwa sababu mbalimbali.</p>
<p>Kwanza, usiri unaotawala udhibiti wa mtandaoni na ukandamizaji unafanya taarifa sahihi liwe jambo gumu sana. Hakuna wiki inayopita bila kuwepo habari za kukamwatwa kwa mwandishi au mwanaharakati mwingine wa mtandaoni katika nchi kama vile Misri au Irani, lakini undani na sababu mara nyingi hugubikwa na utata usioelezeka.</p>
<p>Pili, bado kuna mkanganyiko kuhusu ufafanuzi wa &#8220;Mwanablogu&#8221; ni nani. Wanahabari mahiri wanazidi kuhamia katika matumizi ya vyombo vya habari vya mtandaoni na blogu ili kutafuta uhuru zaidi, hivyo kufanya ufafanuzi uliokuwepo hapo kabla kuingia ukungu. Na wengi kati ya wale wanaoitwa watukutu wa mitandaoni huko Uchina, Tunisia, Vietinamu, au Irani, hawana blogu zao binafsi. Katika nyakati nyingine, wanablogu hukamatwa kwa sababu ya shughuli zao zilizo nje ya mtandao, kuliko yale waliyoyachapishwa kwenye mtandao.</p>
<p>Mkanganyiko huu mara nyingine umefanya iwe vigumu kwa watetezi wa uhuru wa kujieleza wa mtandaoni kuja na mkakati na ushirikiano wa kuwatetea wanablogu na wanaharakati wa mtandaoni, lakini haikutokea kuwa ni muhimu zaidi kujaribu.</p>
<p><strong>Tushirikiane</strong></p>
<p>Katika <a href="http://globalvoicesonline.org/">Global Voices</a> tunawashirikisha waandishi, wahariri, na watafsiri, ambao hutufahamisha kuhusu ukiukwaji wa uhuru wa kujieleza na haki za binadamu.  Kwa kuanzisha <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Threatened Voices</a> tunakusudia <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/submit">kufungua mchakato wa kutolea taarifa</a> hata kwa mtu mwingine zaidi aliye na taarifa fulani.</p>
<p>Tunatoa wito kwa wale wote ambao rafiki, ndugu, wenzao, au wapiganaji wenzao wametishwa kwa namna moja au nyingine ili kusaidia <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/submit">kutengeneza</a> na kutoa taarifa mpya kuhusu wale waliopotea au waliokamatwa, ili kwamba tutafute vyanzo zaidi ili kuthibitisha na kuunganisha na kampeni za mtandaoni zinazolenga kuhakikisha wanaachiwa huru.</p>
<p>Katika mchakato, tunataraji kujifunza zaidi kuhusu ni lini, wapi na kwa kiasi gani wanablogu wanatendewa vibaya katika nchi mbalimbali, ili tuweze kuwashirikisha taarifa hizi waandishi wa habari, watafiti, na wanaharakati, na kujaribu kupigania uwepo wa Intaneti ambamo kila mmoja anaweza kutumia uhuru wake wa kujieleza, na mahali ambapo wanablogu walio magerezani hawasahauliwi.</p>
<p><strong>Saidia kueneza neno. Twiti, blogu na toa taarifa mpya kwenye facebook kuhusu <a href="http://threatened.globalvoicesonline.org/">Sauti Zinazotishwa</a>! </strong></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kutambulisha-sauti-zinazotishwa/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Tamasha la Blogu Indonesia</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 10:39:42 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Indonesia]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Photos]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=547</guid>
		<description><![CDATA[Tulitembelea tamasha la blogu la Indonesia au PestaBlogger 2009. Hii nim ara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika. Tukio hili lilishuhudia wanablogu kutoka kila sehemu ya Kisiwa hiki ambacho pia ni Taifa wakimiminika mjini Jakarta ili kusherehekea, kujadili na kujumuika.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/preetam/">Preetam Rai</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/27/at-the-indonesian-blogger-festival/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Indonesia ina uwanja wa blogu uliosisimka na wenye msisitizo mkubwa kwa jamii. Tamasha la mwaka la wanablogu (Pestablogger) la Indonesia liliwavutia wanablogu na wapenzi wa teknolojia kutoka sehemu zote za taifa.  </p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger011.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /></p>
<p>Ukumbi uliojaa wa tamasha la blogu la Indonesia</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/cZwFCS2aO4U&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/cZwFCS2aO4U&#038;rel=0&#038;color1=0xb1b1b1&#038;color2=0xcfcfcf&#038;hl=en&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
Taswira kutoka kwenye tamasha la blogu.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger02.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Hii ilikuwa ni mara ya tatu kwa tukio hili la mwaka kufanyika na ni vizuri kuona idadi ya washiriki inaongezeka kila mwaka.<br />
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 490px"><img alt="pestablogger09" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger03.jpg" width="480" height="271" /><p class="wp-caption-text">pestablogger09</p></div><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya maadili ya kublogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger06.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya uanahabari wa kiraia<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger07.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Mwanahabari wa kiraia akielezea uzoefu wake kwa wanablogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger08.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="360" /><br />
Kipindi cha majadiliano juu ya kuunganisha kwenye utengano ndani ya Indonesia kwa kutumia blogu. Washiriki pia walijadili njia ambazo Indonesia inaweza kutumia kuiunganisha na dunia ya nje.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger101.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Tristam (aliyewakilisha shirika la wadhamini), Chip, (mkereketwa wa teknolojia kutoka Vietnam) na Retty (Mwanablogu wa Indonesia) wakiwa katika majadiliano. Tukio hili la Indonesia halikushuhudia viwango vya ushiriki kutoka nje ambavyo Kampuchea au Thailand huvishuhudia. Hata hivyo, watu waliojaa udadisi wanatiririka na tunatumaini kupata watu zaidi kutoka maeneo ya Kusini Mashariki ya Asia wakati ujao.<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger12.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="270" /><br />
Msanii wa Batik akitengeneza shati la tamasha la blogu<br />
<img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/pbblogger11.jpg" title="pestablogger09" class="aligncenter" width="480" height="271" /><br />
Wanablogu wanachukua mapumziko kutoka kwenye majadiliano na kuburudika na muziki.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/tamasha-la-blogu-indonesia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Misri: Mwanablogu wa Kiume Aagizia Bikra ya Bandia</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 10:13:43 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[China]]></category>
		<category><![CDATA[Egypt]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Entertainment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Gender]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Ideas]]></category>
		<category><![CDATA[Middle East & North Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=543</guid>
		<description><![CDATA[Mengi yalisemwa na kuandikwa juu ya zana ya kutengeneza bikra ya bandia - mpaka mwanablogu Mmisri wa kiume Mohamed Al Rahhal akanunua moja. Marwa Rakha anatuletea habari hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/marwa-rakha/">Marwa Rakha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/29/egypt-egyptian-male-blogger-orders-artificial-hymen/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Wakati <a href="http://www.rnw.nl/english">Redio ya Uholanzi</a> ilporusha hewani tafsiri ya Kiarabu kuhusu <em>Zana ya Kutengeneza Bikira ya Bandia</em>, pale <a href="http://www.youm7.com/News.asp?NewsID=136364">gazeti la Youm7</a> lilipotangaza kuwa bidhaa hiyo itaanza kupatikana kwenye soko la Misri, wabunge wahafidhina huko Misri walitaka <a href="http://www.huffingtonpost.com/2009/10/05/egypt-fake-hymen-kit-may-_n_309737.html">bidhaa hiyo izuiwe na muagizaji yeyote afukuzwe nchini au akatwe kichwa</a>, na habari hiyo <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/10/08/will-egypt-import-chinese-hymens/">ilipozua kelele kwenye ulimwengu wa blogu wa Misri</a>, <a href="http://www.guardian.co.uk/commentisfree/2009/oct/28/artificial-hymen">Mohamed Al Rahhal</a> alinunua zana hiyo maalum ya kutengeneza bikira ya bandia.</p>
<p>Wakati alipokwenda kuchukua kifurushi chake ofisi ya posta:</p>
<blockquote><p>
Nilikuta kimeshafunguliwa na maafisa mbalimbali wa forodha na posta ambao, baada ya kukosa majibu, waliandika utambulisho wa bidhaa hiyo kama “yenye majimaji mekundu yasiyofahamika” – na walisubiri maelezo yangu.</p></blockquote>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/fakehymen.jpg" title="fakehymen" class="aligncenter" width="460" height="276" /></p>
<p>Aliwaeleza kuwa ni “vipodozi vya wacheza sinema” na kuichukua bidhaa ile nyumbani:</p>
<blockquote><p>Hiyo ndiyo “bikira”: kipande kilichokunjwa cha plastiki cha sentimeta 5&#215;7 – cha ute wa protini unaoitwa albumin, maelezo yalinisahihisha kwa haraka – kilichopakwa wino mwekundu kwenye upande mmoja. Kikiwekwa ukeni kabla ya kujamiiana, plastiki hiyo huganda kidogo, na hupasuka wakati wa tendo. Matone machache ya “damu” huchafua shuka, na kutunza “heshima” ya mwanamke, familia yake au jamii yake.</p>
<p>Kama fanya kazi au la siwezi kujibu. Kutokuwepo kabisa kwa maelezo ya kitaalamu kwenye bidhaa hiyo, pamoja na shutuma mtandaoni kuwa bidhaa hii inaweza kusababisha magonjwa, vilinifanya nisite kumpoatia mtu atakayejitolea kufanya jaribio.</p></blockquote>
<p><em>Mona El Tahawy</em> hakupendezwea na jinsi Wamisri <a href="http://www.monaeltahawy.com/blog/?p=188">walivyopamba moto na kuguswa</a> juu ya bikira bandia pamoja na matatizo yote Wamisri wanayoyakabili siku hizi – gharama za maisha zinazopanda, rais aliye madarakani kwa miaka 28 ambaye mwanawe anaelekea kumrithi, nk. – kelele zote za nini juu ya bikira, iwe ya kweli au ya bandia? </p>
<p>Karibuni kwenye unafiki na kujidanganya ambavyo kwa pamoja vinadunda katikati ya roho mitazamo ya kihafidhina ya kidini juu ya wanawake na uadilifu katika kufanya mapenzi. Na katika shauri la Misri, uhafidhina huo upokatika mizani sawa kote, kwa Waislamu na Wakristu.</p>
<p>Kama Muislamu, ninajua kuwa Qur’an inahubiri uadilifu katika kufanya mapenzi kwa wanaume na wanawake, lakini kushupaliwa huku kwa wanawake na wahafidhina kunamaanisha kuwa ni wanawake tu ambao wanatarajiwa kuzingatia makatazo juu ngono nje ya ndoa. Huku kushupaliwa kwa bikira kumekosa kina zaidi ya yote na kuna hali ya umauti zaidi.</p>
<p><em>Mohamed El Rahhal</em> anashutumu vikali:</p>
<blockquote><p>Unafiki ambao unaturuhusu kubagua dhidi ya asilimia 50 ya jamii wakati tunatoa kibali cha bure kwa nusu nyingine. Ninapinga kuwalazimisha wanawake kwenda umbali huo, mara nyingine kuhatarisha afya zao, ili kuruhusu kucheleweshwa kwa sheria ya kitaifa juu ya mahusiano ya kijinsia. </p>
<p>Uadilifu unatafsiriwa vibaya zaidi na maumbile. Na kama tunasubiri kipande kidogo cha plastiki kifafanue uadilifu, basi tumeshashindwa – na ni budi tutafute ufafanuzi mzuri zaidi.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/misri-mwanablogu-wa-kiume-aagizia-bikra-ya-bandia/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Vietnam: Matangazo Mengi Katika Uwanja wa Ndege</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/vietnam-matangazo-mengi-katika-uwanja-wa-ndege/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/vietnam-matangazo-mengi-katika-uwanja-wa-ndege/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 06 Nov 2009 09:57:37 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Business]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Economics]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Travel]]></category>
		<category><![CDATA[Vietnam]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=540</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naMong Palatino  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Charvey amebaini matangazo mengi kuliko kawaida katika uwanja wa ndege wa Vietnam.
]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/mong/">Mong Palatino</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/06/vietnam-too-many-ads-in-an-airport/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Charvey amebaini <a href="http://chrisfharvey.typepad.com/charvey_in_vietnam/2009/10/i-snapped-this-pic-last-week-at-tan-son-nhat-airport-on-the-way-to-hanoi-every-seat-back-was-covered-with-an-ad-more-eviden.html">matangazo</a> mengi kuliko kawaida katika uwanja wa ndege wa Vietnam.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/vietnam-matangazo-mengi-katika-uwanja-wa-ndege/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Chungu cha Kuiyeyusha Afrika</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:36:02 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=536</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/05/africa-africas-melting-pot/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://marvintumbo.wordpress.com/2009/11/04/africa%E2%80%99s-melting-pot/">Marvin anaandika kuhusu Afripot</a>, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la kutosha na kulazimisha mabadiliko tuayoyahitaji sana.” </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-chungu-cha-kuiyeyusha-afrika/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Ujauzito na Magereza: Afya na Haki za Wanawake Magerezani</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/#comments</comments>
		<pubDate>Thu, 05 Nov 2009 13:24:11 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Americas]]></category>
		<category><![CDATA[Argentina]]></category>
		<category><![CDATA[Brazil]]></category>
		<category><![CDATA[Conversations for a Better World]]></category>
		<category><![CDATA[East Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Eastern & Central Europe]]></category>
		<category><![CDATA[Ecuador]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Laos]]></category>
		<category><![CDATA[Peru]]></category>
		<category><![CDATA[Photography]]></category>
		<category><![CDATA[Russia]]></category>
		<category><![CDATA[Spain]]></category>
		<category><![CDATA[Spanish]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Video]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Western Europe]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=493</guid>
		<description><![CDATA[Mapambano bado yanaendelea kuhakikisha haki za binadamu kwa wanawake wajawazito duniani pote, ni inaelekea kwamba katika mchakato huo, wanawake waliopo magerezani wanasahauliwa. Je ni hatua zipi zilizochukuliwa kuhakikisha kuwa nao wanaangaliwa kwa utu, kwa kuzingatia uhai wanaoubeba.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juliana-rincon-parra/">Juliana Rincón Parra</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/24/pregnancy-and-prisons-womens-health-and-rights-behind-bars/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/2044749780_4ade9e2e3f-300x225.jpg" title="2044749780_4ade9e2e3f" class="aligncenter" width="300" height="225" /></p>
<p><strong>Je, wanawake wote wajawazito wanastahili haki sawa za binadamu, au wanawake wajawazito walio jela huziacha haki hizo? </strong></p>
<p>Kuna maswali machache yanayokuja akilini kuhusu haki ya mwanamke mjamzito kuishi na kumlea mwanae anapokuwa kapatikana na hatia kwa kosa la jinai la namna fulani:<br />
•	Inakuwaje kwao wanapokuwa wajawazito na kupata mtoto wakiwa gerezani?<br />
•	Je, wanapaswa kuwa kipaumbele wakati kuna wanawake wengine nje ya vyuo vya mafunzo bila msaada wa kitabibu?<br />
•	Je, ujauzito unapaswa kuwa juu ya hali nyinginezo za kisheria kumhakikishia mwanamke mjamzito haki zake za kibinadamu? </p>
<p><strong>Marekani: wanawake walio kwenye uchungu wa kuzaa hawatafungwa tena minyororo.  </strong></p>
<p>Je unaweza kufikira mwanamke akijifungua huku mikono yake ikiwa kwenye pingu na miguu yake ikiwa imefungwa na minyororo kwenye kitanda? <a href="http://www.rhrealitycheck.org/user/malika-sadaa-saar">Malika Saada Saar</a>, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa <a href="http://www.rebeccaproject.org/">Mradi wa Rabecca kwa Haki za Binadamu</a>, <a href="http://www.rhrealitycheck.org/blog/2009/10/06/in-labor-and-in-chains">anatuelezea</a> kuhusu kitendo hiki ambacho bado kinatokea nchini Marekani, ambapo wanawake wajazito wanaotumikia kifungo wamekuwa wakifungwa minyororo wakati wa uchungu na kujifungua na kuwa hiki ni kitendo kilichozoeleka katika baadhi ya magereza (ya kurekebishia tabia), ingawa ni hatari kwa afya ya mama na mtoto. Ifuatayo ni video ya mahojiano yaliyoambatanishwa kwenye makala iliyoandikwa kwa ajili ya mradi wa <em>RH Reality Check</em>, jamii ya mtandaoni kuhusu afya na haki ya uzazi na jinsia inatupa taarifa na uchambuzi kwa afya ya uzazi:</p>
<p><object width="425" height="344"><param name="movie" value="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1"></param><param name="allowFullScreen" value="true"></param><param name="allowScriptAccess" value="always"></param><embed src="http://www.youtube.com/v/CWj1uHdxnt8&#038;color1=0x234900&#038;color2=0x4e9e00&#038;hl=es&#038;feature=player_embedded&#038;fs=1" type="application/x-shockwave-flash" allowfullscreen="true" allowScriptAccess="always" width="425" height="344"></embed></object><br />
<strong><br />
Kitu gani hutokea kwa mtoto mchanga wa wa mfungwa baada ya kuzaliwa?</strong></p>
<p>Nchi mbalimbali zina kanuni tofauti kuhusiana na watoto magerezani. Kwa mfano, nchini Argentina, kwa mujibu wa <em>Ajintem</em>, chombo cha mawasiliano cha taarifa za uhamamiaji,  <a href="http://portal.ajintem.com/archivo/80-argentina-prision-domiciliaria-para-embarazadas-y-madres.html">sheria ilipitishwa</a> mwaka uliopita ikifafanua kwamba wanawake wajawazito, wanawake wenye watoto wadogo chini ya miaka mitano na wale wenye watoto walemavu wangenufaika na mpango wa kutumikia kifungo chao makwao chini ya ulinzi wa nyumbani. Sheria hii ingewanufaisha si tu akina mama, ambao kwa kuwa gerezani wasingepata huduma za afya wakati wa ujauzito, lakini pia (ingemnufaisha) mtoto, ambaye angelelewa ama katika mazingira yasiyo salama yanayokosa uhuru na upungufu wa udhibiti wa afya na chakula, au wangelelewa mbali na mama, na hivyo kusababisha mlolongo wa matatizo mengine. Hata hivyo, ujumbe ni kwa ajili ya mahakimu kufuatilia kiini cha sheria na kutoa ruhusa hii kwa wanawake wale ambao hawahusishwi na mashitaka ya jinai ya matumizi ya nguvu, kuhakikisha kwamba idadi kubwa ya raia iliyobaki haiuchukulii ujauzito kama kadi ya kumtoa mtu jela bure.</p>
<p>Katika visiwa vya Canary, kwa mujibu wa blogu ya <em>Prisiones y penas</em>, ambayo huandika kuhusu habari zinazohusu jela na magereza, wanawake wanaruhusiwa <a href="http://prisionesypenas.blogspot.com/2009/09/detenidas-con-hijos-en-carceles.html">kuishi na watoto wao hadi umri wa miaka mitatu</a> ndani ya selo zao, lakini wakiwa pamoja na wafungwa wenzao, kitu ambacho sio mazingira mazuri sana kwako. Kwa hiyo, wanawake wajawazito au wanawake wenye watoto wenye umri wa chini ya miaka 3 huambiwa kuhusiana na kuingia kwenye magereza kuwa si vizuri kwa mtoto kukualia gerezani, na hupewa uchaguzi wa kumpeleka mtoto kwa wanafamilia wengine. Hali ni hii hii huko <a href="http://www.reuters.com/article/worldNews/idUSTRE5085ZV20090109">Peru</a> na <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">Urusi</a>. Nchini Marekani, kuna magereza mawili tu yenye kuruhusu jambo hili, huko New York na Nebraska, <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/e_moms.html">kama ilivyoonyeshwa na mpiga picha maarufu Jane Evelyn Atwood</a> kwenye insha ya picha zake tatu kwa ajili ya <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/"><em>Shirika la kimataifa la Amnesty International</em>, inayoitwa <em>Too Much Time</em></a>, ambapo alitembelea dazani nyingi za magereza kote duniani kurekodi na kuweka kumbukumbu za maisha ya wafungwa.</p>
<p>Kwa nini mfumo wa magereza nchini Marekani hauruhusu, kwa ujumla, wanawake wenye watoto kubaki nao? Atwood anaeleza kwamba kwa sababu ya mazingira ufungwa, hairuhusiwi. Kwenye <a href="http://prisonphotography.wordpress.com/2009/10/07/women-behind-bars-jane-evelyn-atwoods-too-much-time/"><em>blogu ya Prison Photography</em> wanaelezea madai haya</a>: </p>
<blockquote><p>Watoto hawahusishwi kwenye magereza yote isipokuwa mawili tu nchini Marekani. Tishio la usalama linatajwa kama sababu: mtoto ndani ya gereza ni dhaifu na atakuwa shabaha ya malengo maovu siku zote. Madai yanaonekana kuwa hayana maana kwa kiasi fulani kwa unapofananisha na mifumo ya adhabu kwa nchi nyinginezo.</p></blockquote>
<p>Insha ya Atwood kwenye wavuti ya <em>Amnesty International</em> inaonyesha mambo mawili, sehemu inayohusu taratibu za kujifungua huku umefungwa minyororo kama yalivyoelezwa kwenye <a href="http://www.amnestyusa.org/women/custody/toomuchtime/pt_02/f_vanbab.html">Mtoto wa Vanessa</a> na pia inaonyesha jambo jingine kuhusu mfumo wa magereza na umama, kwa kutumia picha za wanawake wakati mpigapicha akisoma insha kuhusu uzoefu wake wa kutembelea magereza huku akipiga picha. </p>
<p><strong>Ujauzito kama zana ya mapatano? </strong></p>
<p>Kwa nini haki za wanawake wajawazito gerezani zinatatanisha? Katika  <em>Russia Today</em>, idhaa ya matangazo ya Kirusi, <a href="http://russiatoday.com/Top_News/2009-07-27/russia-s-prison-born-children-marked-for-life.html">mada hii inatajwa</a> panapojadiliwa suala la watoto kuzaliwa na kulelewa katika mfumo wa magereza wa Kirusi:</p>
<blockquote><p>Wenye kutilia mashaka (suala hili) wanadhani akina mama wengine hupata ujauzito kwa makusudi ili tu kurahisisha maisha huko gerezani. Ruhusa ya kwenda hospitali, halafu kuwa na ratiba iliyojaa muda mwingi na mwanao –ni afadhali kuliko kukaa kwenye seli ya magereza, wanadai. </p></blockquote>
<p>Na kuna wanawake ambao wanaona kwamba kuwa na mimba ni njia pekee ya kukwepa hukumu, kama ilivyotokea mwezi Juni, pale mwanamama wa Kiingereza aliwekwa ndani na kuhukumiwa kifo huko Laos kwa sababu ya kusafirisha madawa ya kulevya akapata ujauzito gerezani na akanusurika kunyongwa, kwa sababu serikali ya Laos isingemnyonga mwanamama mjamzito. <a href="http://www.dailyexpress.co.uk/posts/view/105278/No-firing-squad-for-girl-who-fell-pregnant-in-jail">Madai yaliyotolewa </a>kwa mujibu wa jarida la Kiingereza la <em>Daily Express</em>, ni kwamba alipata ujauzito kwa kupandikiziwa mbegu za kiume ‘ili kupata hukumu nyepesi zaidi” </p>
<p><strong>Kwa maneno yao: Wanawake wanaeleza kuhusu watoto wao na maisha ya gerezani</strong></p>
<p>Geraldin Rodríguez, Mwajentina aliye kwenye jela za Ecuador kwa sababu ya biashara ya madawa ya kulevya anamueleza <a href="http://marcosbrugiati.blogspot.com/2009/07/carcel-de-mujeres.html">Marcos Brugiati</a>, mwandishi mshiriki katika chapisho la mtandaoni linalohusiana na masuala ya sanaa liitwalo <em><a href="http://www.indexarte.com.ar/noticias/562/las-rejas-de-la-carcel-el-arte-de-la-espera.htm">Plastica-Argentina</a></em>, masimulizi kuhusu kuigiza na kufanya maonyesho ndani ya jela, kupata ujauzito gerezani na kumpata mwanae. Aliruhusiwa kuwa na mwanae, lakini akaamua kwamba mwanae anahitaji kukua akiwa mtu huru:</p>
<blockquote><p> “Decidí que salga para vivir, tenía miedo que sufra de grande los traumas que hoy tengo. Se lo llevó al año mi hermano quien se hice cargo con su esposa”.</p></blockquote>
<div class="translation">Niliamua aondoke ili aishi, nilikuwa na wasiwasi angeteswa na msongo wa mawazo nilionao leo. Baada ya mwaka kaka yangu alimchukua na anamtunza kwa kushirikiana wa mke wake. </div>
<p>Juvinete yuko kwenye <a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">gereza la Kihispania</a>, na alikuwa mjamzito wakati alipofungwa kwa kusafirisha madawa ya kulevya. Anasimulia habari zake kwenye gazeti la kanda huko Uhispania linaloitwa <em><a href="http://www.nortecastilla.es/20080908/vida/quedarse-embarazada-prision-irresponsable-20080908.html">NorteCastilla</a></em>. Miaka mitatu baada ya kujifungua mwanae akiwa gerezani, mwanae ilibidi aondoke, na alipelekwa kwa familia ya kufikia. Juvinete humuona mwanae huyo wa kike kila baada ya siku 15 na kila miezi miwili hupata ruhusa ya wiki mbili kukaa na mwanae. Hata hivyo, mambo hayaonekani kuwa mazuri sana: kuna uwezekano kwamba Juvinete atapelekwa Brazil alikozaliwa, na anahofia matokeo ya mabadiliko haya kwa mwanae. Anao ushauri kwa mwanamke yeyote anayeamua kupata ujauzito akiwa jela:</p>
<blockquote><p>-Intento convencerlas para que no se queden en estado dentro porque ver a un niño privado de libertad es muy duro, es irresponsable. Ellos no tienen que pagar nuestros errores.</p></blockquote>
<div class="translation">
Ninajaribu kuwashawishi wasipate ujauzito wakiwa bado ndani kwa sababu kumuona mtoto akikosa uhuru wake ni vigumu sana, ni kutokuwajibika. (Watoto wanaozaliwa jela) wasilipie gharama ya makosa yetu</div>
<p>.  </p>
<p>Kwenye wavuti ya <em><a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">Woman and Prison</a></em>, iliyojikita katika kuyatazama maisha ya wanawake wakiwa kwenye mifumo ya magereza , <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/kebby-warner.html">mfungwa Kebby Warner anaongelea ujauzito wake</a> mwenyewe alipokuwa akitumikia kifungo kwenye gereza la Kimarekani, na jinsi alivyotendewa wakati wa ujauzito wake, utungu na baadae, wakati alipokuja kunyang’anywa mwanae. Hapa ni muhtasari anapoandika kuhusu hatua za kujifungua: </p>
<blockquote><p>Wakati wa utungu, hakuna mtu anaruhusiwa kuwa kwenye chumba cha kujifungulia. Familia yangu wala haikujua kwamba nilikuwa ninajifungua au nimempata (mwanagu) mpaka nilipokuwa nimetoka hospitali. Wakati huo wa siku tatu baadhi ya walinzi walikuwa ndani ya chumba, lakini muda mwingi, wakati wauguzi walipowaomba kukaa nje ya mlango, walitii. Nimesikia simulizi za kutisha za wanawake wakifungwa kwa mnyororo kwenye kitanda cha uzazi. Ninashukuru kwa kutokukumbana na hali hiyo. Wauguzi wengi walinitendea kama binadamu badala ya mfungwa.</p></blockquote>
<p>Unaweza kusoma shuhuda zaidi kuhusu kukua na mzazi gerezani na madhara mbalimbali ambayo kufunga wanawake kunaweza kuyawasababisha kwa watoto wao <a href="http://www.womenandprison.org/motherhood/index.html">kwenye Wanawake na Magereza</a>.</p>
<p>Kwa hiyo unafikiriaje? Kwa wanawake wajawazito duniani kote kutokupata huduma za afya za namna yoyote, je jitihada zaidi zinahitajika kuwanufaisha wanawake walio gerezani? Je, kuna tofauti kati ya wanawake wanaotumikia kifungo kwenye magereza (ya mafunzo) na wale wanaoishi nje? Je, ni lazima kuwatendea tofauti?<br />
<em><br />
Picha iliyotumika kwenye makala hii ni “17 de noviembre” ya <a href="http://www.flickr.com/photos/daquellamanera/2044749780/">daquella manera</a>.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/ujauzito-na-magereza-afya-na-haki-za-wanawake-magerezani/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Georgia: Aibu Katika Kanisa la Orthodox</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/georgia-aibu-katika-kanisa-la-orthodox/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/georgia-aibu-katika-kanisa-la-orthodox/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 04 Nov 2009 10:58:04 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Central Asia & Caucasus]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Freedom of Speech]]></category>
		<category><![CDATA[Georgia]]></category>
		<category><![CDATA[Religion]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=528</guid>
		<description><![CDATA[Katika nchi inayofuata dini zaidi kwenye maeneo ya kusini mwa Caucasus ambako mkuu wa Kanisa la Orthodox (madhehebu ya Kanisa la zamani au kihafidhina) anaweza kuhamasisha ongezeko la watoto, kukosoa watumishi wa kanisa bado ni mwiko. Kuwatania, hata hivyo, ni jambo baya zaidi na lililojaa hatari.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/onnik-krikorian/">Onnik Krikorian</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/georgia-orthodox-scandal/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Katika nchi inayofuata dini zaidi kwenye maeneo ya kusini mwa Caucasus ambako mkuu wa Kanisa la Orthodox (madhehebu ya Kanisa la zamani au kihafidhina) <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/03/30/georgia-holy-baby-boom/">anaweza hata kuhamasisha ongezeko la watoto</a>, kukosoa watumishi wa kanisa bado ni mwiko. Kuwatania, hata hivyo, ni jambo baya zaidi na lililojaa hatari, kama blogu hii ya <em>This is Tbilisi Calling</em> <a href="http://caucasusreports.blogspot.com/2009/11/heretics-nabbed-for-indecent-video.html">inavyoripoti</a>.  </p>
<blockquote><p>Askari polisi wa Georgia wanaripotiwa kuwa wameweza kuwafuatilia na kuwapata waharibifu wa fikra waliohusika katika utengenezaji wa video za masihara ‘chafu na zinazotusi’ ambazo zilimlenga mkuu wa Kanisa la Orthodox na kusababisha aibu katika taifa zima kwenye nchi hii yenye kufuata dini kwa bidii. Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani iliwatambua wakosefu hao kuwa ni mwanafunzi wa shule ya msingi na mwanafunzi mwingine mkubwa. [&#8230;]</p></blockquote>
<p><em><br />
Evolutsia</em>, anaangalia suala kubwa zaidi linalohusiana na nguvu za Kanisa pamoja na uhuru wa maoni. Katika makala ya maoni kwenye blogu mpya ya habari kwa lugha ya Kiingereza iliyozinduliwa, Inge Snip <a href="http://networkedblogs.com/p16567796">anapiga kengele za tahadhari</a>.  </p>
<blockquote><p>Moja ya uhuru wa msingi, ninaamini, ni uhuru wa maoni. Uhuru wa maoni unawezesha nchi kumuonyesha kila mwananchi wake kuwa maoni yao yanaruhusiwa kusikilizwa, bila kujali yaliyomo. Na kwa kuongeza, demokrasia ya kweli inaruhusu kutaniwa kwa watu muhimu kwenye jamii, na kwa kufanya hivyo, inaonyesha kukomaa kwake.</p>
<p>[…]</p>
<p>Na kwa kumalizia, hakuna sababu ya kuchunguza suala hili, na wala haipaswi kuwepo; hata hivyo, vyombo vya kutunza sheria vilifanya kinyume, kwa sababu kuna namna fulani ya matakwa ya wengi. Kama mwanafunzi wa sheria, kwa urahisi, hii ni moja ya sababu za kijinga katika uchunguzi wowote wa kisheria ambao nimewahi kuusikia.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/georgia-aibu-katika-kanisa-la-orthodox/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Kenya: Ramani Mpya Ya Wazi ya Kitongoji Cha Kibera Kwenye Blogu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kenya-ramani-mpya-ya-wazi-ya-kitongoji-cha-kibera-kwenye-blogu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kenya-ramani-mpya-ya-wazi-ya-kitongoji-cha-kibera-kwenye-blogu/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 04 Nov 2009 10:50:12 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Development]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=525</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Mradi wenye lengo la kutengeneza ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi, Kenya:  “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/kenya-blogging-the-first-open-map-of-kibera/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mradi wenye lengo la kutengeneza <a href="http://www.mapkibera.org/blog/?p=21">ramani mpya ya wazi ya kitongoji cha Kibera mjini Nairobi</a>, Kenya:  “Na jana tulimaliza siku nzima pale MS Action Aid kenya, ambako wanafunzi wa ki-Denmark pamoja na wengine waliotokea kwenye mashirika mbalimbali kama vile Ushahidi, UNICEF, Umande Trust na World Bike, walipoonyeshwa mbinu za kutengeneza ramani.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/kenya-ramani-mpya-ya-wazi-ya-kitongoji-cha-kibera-kwenye-blogu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
