GlobalVoices katika

Western Europe

Kumbukumbu za sehemu · 26 jumbe


Habari mpya Kuhusu Western Europe

22 Januari 2013

“Wanasemaje Bamako?” Mazungumzo na Awa anayeishi Mali

Mazungumzo ya kila siku kwa njia ya skype(kwa Kifaransa)  kati ya Awa Traoré aliyeko Bamako na Anne Morin akiwa Ufaransa (kupitia anuani ya @annagueye)

Anne Morin na Awa Traoré wanabadilishana mawazo kuhusiana na maisha ya kila siku mjini Bamako, ujira usiokidhi mahitaji, gharama za maisha na hali ya kisiasa isiyotabirika wakati huu ambapo vita vinanukia nchini humo.

15 Oktoba 2012

DRC Kongo: Misuguano Kati ya Kinshasa na Paris Mkutano Unapoanza

Le Potentiel anaandika kwamba [fr] tathmini ya Uvunjaji wa Haki za Binadamu nchini DRC Kongo iliyofanywa na Rais wa Ufaransa Hollande haikuchukuliwa kijuu juu na serikali ya Kongo wakati ambapo Mkutano wa nchi zizungumzazo Kifaransa ndio kwanza umeanza mjini Kinshasa, DRC. SErikali hizi mbili zinaonekana kutofautiana sana kuhusu mambo kama kifo cha mtetezi wa Haki za Binadamu Ndg Chebeya, tume ya taifa ya uchaguzi na uhitaji wa kamati itakayosimamia masuala ya haki za binadamu.

5 Disemba 2010

Urusi: Habari ya Putin-Berlusconi Kwenye WikiLeaks

Kwenye The Daily Beast, Julia Ioffe anatoa maoni juu ya masuala yaliyowekwa wazi katika Wikileaks kuhusu uhusiano kati ya Waziri Mkuu wa Urusi na mwenzake wa Italia Silvio Berlusconi.

23 Agosti 2010

Cape Verde: Midahalo Kuhusu Vijana na Siasa Inayoendelea Huko Ureno

Kuna kundi la raia wa Cape Verde ambalo huandaa mikutano mjini Lisbon ili kujadili uhusiano kati ya vijana na siasa, kama anavyoeleza Suzano Costa katika video [pt] kama ilivyowekwa tena na Amilcar Tavares. Katika blogu yao – Tertúlia Crioula [pt] - unaweza kusoma maelezo yaliyochukuliwa kutoka “Cape Verde katika Mdahalo” kadhalika unaweza kusoma majadiliano mengine kuhusu masuala muhimu.

3 Julai 2010

Ghana: Tangazo la Kibaguzi la Kombe la Dunia

Sokari anaandika kuhusu tangazo la biashara la Kombe la Dunia la kibaguzi lililotengenezwa na wakodishaji wa magari wa Kijerumani SIXT: “Tangazo hilo hapo juu lilitumwa kwangu na rafiki kutoka Ujerumani ambaye alifafanua hivi: Linacheza kauli mbiu kadhaa zenye mtazamo wa kiUlaya, mtazamo unaodharau Uafrika kuhusiana na mchezo wa mpira unaokuja kati ya Ghana/Ujerumani.”

14 Aprili 2010

Piga kura kuchagua “Blogu Bora Zaidi”

Soma makala hii.

Upigaji kura mtandaoni umeanza kwa ajili ya Tuzo ya Blogu Bora Zaidi inayotolewa na Deutsche Welle (Shirika la Habari la Ujerumani), moja kati ya mashindano ya blogu yenye hadhi kubwa kimataifa na blogu zilizotajwa kushiriki ni za lugha kumi na moja tofauti. Unaweza kuipigia kura blogu uipendayo hadi April 14, 2010.

28 Machi 2010

Siku ya Ada Lovelace: Kuwapongeza Wanawake Wanajishughulisha Kupigania Teknolojia na Uwazi Ulimwenguni

Soma makala hii. Technology for Transparency Network

Katika kusherehekea Siku ya Ada Lovelace tunawaletea makala fupifupi kuhusu wanawake kadhaa walio sehemu mbalimbali duniani ambao hutumia teknolojia ili kuzifanya serikali ziwe wazi na zinazowajibika zaidi.

27 Februari 2010

Kadri Liberia inavyotulia, vijana waanza kuzungumzia ngono

Conversations for a Better World

Kadri Liberia inavyoendelea kutoka kwenye vita ya kutisha ya wenyewe kwa wenyewe, wengi wanahofu mchanganyiko wa umaskini uliokithiri na maamuzi yenye hatari ya ngono vitaongeza kiwango cha VVU/UKIMWI na idadi ya mimba zisizotarajiwa.

20 Disemba 2009

Canada Imesema Nini? Upotoshaji wa Habari Kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya Tabianchi

Soma makala hii.

Serikali ya Canada inasemekana imetoa tamko la jazba leo, ikikanusha upotoshaji wa habari zinazodaiwa kufanywa nayo kwa mujibu wa Jarida la Wall Street likidai kwamba Canada imebadili sera yake na itakuwa ikikubaliana na malengo ya kupunguza hewa ya ukaa.

13 Disemba 2009

Austria: Jinsi Nyenzo Za Habari Za Kijamii “Zinavyoviwashia Moto Vyuo Vikuu”

Soma makala hii.

Je, ulijua kwamba katika wakati huu vyuo vikuu vingi kote Ulaya vinakaliwa na wanafunzi? Vuguvugu hili lote limeratibiwa kwa kutumia nyenzo za uanahabari wa kijamii katika mtandao.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha