mahojiano mafupi ya video kuhusu mashindano yaliyoandaliwa na timu ya mpira wa miguu ya Refugee VI soccer ynakusudia kuelimisha umma juu ya suala la ubaguzi dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini.
Habari Maalum Kuhusu Uganda
Habari za Upotoshaji Kuhusu Afrika Katika Vyombo vya Habari vya Kimataifa

Kampeni ya kumkamata #Kony2012 ilibeba mambo yaliyorahisishwa mno kuhusu Afrika. Vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe, hata hivyo, kwa sasa havina kinga dhidi ya ukosoaji wa aina hii. Hapa ni muhtasari wa watu maarufu, makosa na kutokuwepo umakini katika habari zinazopewa nafasi katika vyombo vya habari vya dunia kuhusu Afrika na katika vyombo vya habari vya Afrika vyenyewe
Kitabu-pepe Kipya cha GV: Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko

"Sauti ya Kiafrika ya Matumaini na Mabadiliko", kinakupa mtazamano wa kipekee kuhusu watu na habari za eneo la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia posti zetu zilizo bora zilizoandikwa kwa lugha ya Kiingereza kwa mwaka 2012. Hii ni zawadi sahihi kabisa ya kuukaribisha mwaka mpya.
Uganda: Binti awa Mbunge wa Kwanza Mdogo Kuliko wote Afrika

Afrika inachipuka na wanawake wa ki-Afrika wanachipuka nayo. Hivi sasa, Malawi na Liberia zinaongozwa na maraisi wanawake. Sasa nchini Uganda mbunge kinda kabisa kuliko wote barani Afrika amechaguliwa - naye ni Proscovia Alengot Oromait umri wa miaka 19 .
-
Uganda: Aina Mpya ya Kifafa Yatishia Maisha ya Watoto.
14 Julai 2012
-
Uganda: Kuvunja Utamaduni wa Ukimya Kuhusu Haki za Afya.
11 Julai 2012
-
Uganda: Ndiyo Tunampinga Kony! 30 Aprili 2012
-
Dondoo za Video: Utetezi wa haki za binadamu
25 Machi 2012
-
Baada ya Kony 2012, “What I Love About Africa” Yanyakua Mazungumzo
16 Machi 2012
Habari mpya Kuhusu Uganda
28 Aprili 2013
Uganda: Kukumbuka milipuko ya mabomu ya 2010
Wananchi wa Uganda wameutumia mtandao wa Twita na Facebook kuwakumbuka wahanga 2010 wa milipuko yha mabomu iliyotokea kwenye klabu ya Rugby huko Kyaddondo na katika baa ya Kijiji cha Kiethiopia jijini Kampala Uganda.Mashambulizi hayo yalitokea wakati ambao wapenzi wa kandanda walikuwa wakitazama mpambano wa fainali kati ya Uhispania na Uholanzi uliofanyika nchini Afrika Kusini.
10 Oktoba 2012
Uganda Yaadhimisha Miaka 50 ya Uhuru
Terehe 9 Oktoba, 1962, Uganda ilijipatia uhuru wake kutoka kwa Mwingereza. Wakati nchi hiyo iliposherehekea Kumbukumbu yake ya Dhahabu hivi karibuni, wa-Ganda wanaotumia mtandao wamekuwa wakitumia zana za kijamii kama Twita na Facebook kusema maoni yao kuhusu sherehe hizo za kutimiza miaka 50!
15 Julai 2012
Afrika: Ujuzi wa Matumizi ya Zana za Habari za Kijamii kwa Vijana Wanaoishi na Ulemavu.
Warsha ya vijana walemavu kutoka kote barani Afrika lafanyika Dakar, Senegali. Warsha hii ilipangwa na DRI na YI. Imeandikiwa na Haute Haiku.
3 Juni 2012
Uganda: Je, Uganda inageuka kuwa dola ya kifalme?
Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni amekuwa madarakani tangu mwaka 1986. Majuma machache yaliyopita, wananchi walianza kudodosa habari za nani hasa atamrithi kama ataamua kutokugombea kwa awamu ya nne mwaka 2016. Tetesi zinadai kwamba rais anamwunga mkono mkewe, Waziri wa mambo ya Karamoja kurithi kiti cha rais.
11 Januari 2012
Afrika: TEKNOHAMA Kwa Ajili ya Wakimbizi na Watu Wasio na Makazi
Barani Afrika na kwingineko TEKNOHAMA imeondokea kuwa nyenzo muhimu wakati wa matatizo wakati teknolojia kama vile Ujumbe mfupi wa Simu za Mkononi, VOIP, na Simu za mkononi zinapozidi kuwa na manufaa kwa wakimbizi na kwa watu waliokosa makazi.
18 Mei 2011
Uganda: Polisi Wawanyunyizia Waandamanaji Rangi ya Waridi
Polisi wa Uganda wameikabili kampeni inayoendelea kwa mwezi mmoja sasa ya Kutembea Kwenda Kazini kwa kuwanyunyuzia waandamanaji moshi wa machozi na risasi sa moto. Wakati wa maandamano siku ya Jumanne, walitumia mbinu mpya, ya kuwashambula waandamanaji waliokuwa wakijaribu kuandamana kuelekea viwanja vya katiba katikati ya jiji la Kampala kwa maji yaliyochanganywa na uji wa rangi ya waridi.
2 Mei 2011
Uganda: Wananchi Wakasirishwa na Kukamatwa Kikatili kwa Kiongozi wa Upinzani
Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Dk.Kiiza Besigye alikamatwa tena katika mji mkuu wa Kampala kutokana na kushiriki kwake katika Kampeni ya Kutembea Kwenda Kazini usiku mmoja baada ya kuachiwa huru kwa dhamana. Besigye alipewa dhamana kwa sharti kuwa asijihusishe na kampeni ambayo imeuweka utawala wa Uganda kwenye vichwa vya habari kwa majuma matatu sasa.
9 Septemba 2010
Africa: Waafrika Wasimulia Kumbukumbu Zao za Utotoni
That African Girl ni blogu yenye mfululizo wa makala zilizoandikwa na Waafrika kutoka dunia nzima kuhusu maisha ya utotoni. Ni blogu inayoelezea kuhusu makuzi katika familia za Kiafrika na uzoefu wa kuishi katika tamaduni mbili.
15 Julai 2010
Uganda: Wanablogu Washtushwa na Milipuko ya Mabomu
Mashabiki wa soka kote ulimwenguni walikusanyika kwenye kumbi za baa na migahawa ili kushuhudia mechi ya fainali za Kombe la Dunia usiku wa Jumapili iliyopita. Nchini uganda usherehekeaji huu ulikatishwa pale milipuko ya mabomu iliposambaratisha maeneo mawili maarufu kwa sherehe za mpaka majogoo jijini Kampala, mji mkuu wa nchi hiyo.




























Kiungo cha RSS kwa Uganda 












mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...