GlobalVoices katika

Tanzania

Kumbukumbu za nchi · 11 jumbe


Habari mpya Kuhusu Tanzania

7 Mei 2013

Mfululizo wa Tamthilia ya Runinga ya Nchini Tanzania

The Team Tanzania (Timu Tanzania) ni mfululizo wa Tamthilia ya Runinga yenye kuzungumzia:

[...] Bi. Wito, mwalimu mahiri wa somo la uraia, anaigeuza kabisa mitazamo ya vijana makinda watatu anapowauliza maswali mazito mfano “Wewe ni nani”? vijana wale wenye umri wa miaka 16, waliofahamiana vyema tangu wakikua. Katika kuingia katika umri wa utu uzima, vijana hao wanatafuta kujitambua huku wakikabiliwa na misongo mingi ya kifamilia na kiutamaduni.

Michoro ya Dar: Sanaa kwa Maendeleo Endelevu

Dar Sketches (Michoro ya Dar) ni sehemu ya mradi unaoanzia ngazi ya Mtaa jijini Dar Es Salaam, Tanzania ulioanzishwa na msanii na mchoraji Sarah Markes:

Ni katika kuenzi urithi wa kitamaduni na wa sanaa ya ubunifu wa majengo kwa jiji la Dar Es Salaam sambamba na juhudi za kukuza uelewa kwa wananchi juu ua tishio la urithi huu linalotokana na kasi kubwa ya kupanuka holela kwa jiji hilo.

2 Aprili 2013

Tanzania: Ghorofa Laporomoka jijini Dar Es Salaam

Pernille anaweka picha mtandaoni zinazoonyesha ghorofa lililoporomoka jijini Dar Es Salaam, Tanzania siku ya Ijumaa, 29 Machi 20013: “Karibu kabisa na jengo hilo kuna uwanja wa kandanda unaotumiwa na watoto. Zaidi ya watu 60, pamoja na watoto, wanaripotiwa kupotea kwa mujibu wa kituo cha televisheni cha ITV. Hakuna kauli rasmi iliyotolewa mpaka sasa.”

19 Septemba 2012

Je, Sifa ya ‘Kisiwa cha Amani’ Tanzania Imeanza Kutoweka?

Soma makala hii.

Tanzania imeshuhudia matukio kadhaa mabaya tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa 2010. Tukio la hivi karibuni ni kifo cha kikatili cha mwandishi wa habari wa Tanzania Daudi Mwangosi, aliyeuawa kwa bomu la machozi huko Iringa, Kusini mwa Tanzania, wakati polisi walipojaribu kukitawanya kikundi cha wafuasi wa chama cha upinzani.

30 Agosti 2012

Tanzania/Malawi: Utafutaji Mafuta kwenye Ziwa Nyasa WachocheaMgogoro wa Umiliki

Soma makala hii.

Taarifa kwamba Malawi inatafiti mafuta katika Ziwa Nyasa (linalojulilkana pia kama Ziwa Malawi) zimeibua mjadala motomoto. Wakati ambapo serikali ya Malawi inadai umiliki kamili wa ziwa hilo, Tanzania inataka mpaka utambuliwe kuwa katikati ya ziwa.

31 Julai 2012

Afrika: Usanii wa Kisasa wa ki-Afrika Mtandaoni

Usanii Afrika blogu inayoonyesha usanii wa kisasa wa ki-Afrika: Usanii Afrika ni blogu iliyozaliwa kutokana na upenzi. Akiwa amezaliwa na kipaji cha ubunifu yeye mwenyewe, mwanablogu, Kirsty Macdonald amekuwa na mahusiano ya karibu na masuala ya sanaa na kujieleza”

13 Aprili 2012

Photos jumbe Video jumbe
Tanzania: Mwigizaji Nyota wa Filamu, Steven Kanumba, Afariki Dunia

Soma makala hii.

Tanzania ilimuaga mmoja wa wasanii wake maarufu na nyota wa tasnia ya filamu, Steven Kanumba, kwa maziko yaliyogubikwa na majonzi mazito mnamo tarehe 11 Aprili 2012. Alifariki alfajiri ya Jumamosi, akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kile kilichodaiwa kuwa ugomvi wa kimapenzi na rafiki yake wa kike aitwaye Elizabeth Michael kwa jina maarufu “Lulu”.

30 Oktoba 2010

Tanzania: Majumuisho ya Habari za Uchaguzi Mkuu wa 2010

Mnamo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania watashiriki katika uchaguzi wa Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar pamoja na Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Huu ni mjumuisho wa yale yaliyojiri katika blogu mbalimbali kuhusiana na uchaguzi huo.

27 Oktoba 2010

Tanzania: Ulimwengu wa Blogu Wachambua Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2010

Ifikapo tarehe 31 Oktoba 2010, Watanzania zaidi ya milioni 19.6 watafanya uamuzi muhimu kuhusu hatma ya nchi yao. Watafanya hivyo kupitia uchaguzi mkuu wa nne chini ya mfumo wa vyama vingi. Wakati zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi huo, ulimwengu wa blogu wa Tanzania nao unafuatilia kwa karibu yale yanayotokea katika kampeni za vyama mbalimbali.

9 Oktoba 2010

Video jumbe
Tanzania: Matumizi ya Vyombo vya Habari vya Kijamii kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2010 Nchini Tanzania

Soma makala hii.

Tanzania inaelekea katika uchaguzi wake mkuu mnamo Oktoba 31 mwaka huu na hivi sasa kampeni za uchaguzi zinaelekea kileleni. Wakati kampeni zikipamba moto, wagombea wa nafasi ya urais, ubunge na udiwani wameanza kutumia zana mpya za mawasiliano ya jamii ili kuwasiliana na wapiga kura. Sanjari na mikutano ya kampeni, ambayo hulenga watu wengi zaidi, idadi ndogo ya wanasiasa wameanza kutumia zana za mawasiliano ya kijamii kama vile blogu, picha za video za mtandaoni, Facebook na Twitter ili kukuza mawasiliano na wapiga kura.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha