<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; South Africa</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/sub-saharan-africa/south-africa/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 23 Nov 2009 10:38:13 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[Children]]></category>
		<category><![CDATA[Education]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[U.S.A.]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>
		<category><![CDATA[Youth]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=696</guid>
		<description><![CDATA[Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/11/south-africa-sesame-streets-hiv-positive-muppet-raises-awareness/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/11/Kami22.jpg" title="Kami" class="alignright" width="200" height="260" /><br />
Wakati kipindi cha watoto cha <a href="http://www.sesamestreet.org/home/">Mtaa wa Sesame</a> (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake  mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI. </p>
<p>Wakati kipindi cha Sesame Street kinatazamwa katika zaidi ya <a href="http://www.sesameworkshop.org/newsandevents/sesameupdates/sesame_40thbirthday">nchi 140</a>, kila toleo huzungumzia masuala yanayotokea kwenye jamii husika na kwa kumtumia vikaragosi tofauti. <a href="http://muppet.wikia.com/wiki/Kami">Kami</a> mwenye rangi ya Njano-dhahabu alionekana kwa mara ya kwanza kwenye kipindi mwenza cha Sisame Street cha Afrika Kusini kinachoitwa <a href="http://www.schooltv.co.za/TakHome.htm">Takalani Sesame</a>, mwaka 2002 kujibu matatizo ya nchi yanayohusiana na UKIMWI. Kama kikaragosi cha kwanza duniani chenye VVU, kinasaidia kuwaelimisha watoto kuhusu ugonjwa na kushughulikia masuala yanayohusiana na kuwa mwathirika wa UKIMWI. Jina la Kami <a href="http://www.sesameworkshop.org/aroundtheworld/southafrica">linatoka</a> kwenye neno la kiSetswana “Kamogelo”, lenye maana ya “kukubalika.” Sunshinestar110, anayeblogu kwenye <em>U dont Like My Opinion&#8230;That’s Fine!</em> <a href="http://thatsfine2009.blogspot.com/2009/11/happy-birthday-to-you.html">anazungumzia zaidi</a> kuhusu Kami:</p>
<blockquote><p>“Kami ni mwathirika wa VVU mwenye afya, yatima wa miaka mitano mwenye bashasha ambaye ana aibu kidogo lakini huchangamka akijongelewa kwa njia ya kirafiki, pia anajua mengi kuhusu Virusi vya UKIMWI, alimpoteza mama yake kwa ugonjwa huo. Kami alipozinduliwa, akiwa na nywele zake za kahawia na pia alivaa fulana, na kutembea kwenye mtaa wa Susame na kujiuliza huku akihofu kama wenyeji watataka kucheza nae. Hakuwa na haja ya kuogopa kwa sababu vikaragosi vingine vilimpokea kwa bashasha”</p></blockquote>
<p>Kami aliletwa kuwasaidia watoto wengi wa Afrika Kusini wanaotaabika na janga la VVU/UKIMWI. Inaaminika kuwa Afrika Kusini ina idadi kubwa zaidi ya watu walio na VVU duniani – inakadiriwa kuwa watu <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">milioni 5.7</a> Kwa makadirio, kati ya walioathirikia, 280,000 ni watoto wa umri wa miaka chini ya 14 na kuna yatima milioni 1.4 nchini kutokana na UKIMWI. Zaidi ya madhara ya kimwili ya kuwa na VVU, vilevile kuna unyanyapaa na miiko inayotokana na kuwa na ugonjwa, ambayo husababisha ugumu kwa watu kupata matibabu stahiki na msaada. Takalani Sesame, ambayo inajumuisha lugha zote rasmi 11 za Afrika Kusini, inajaribu kuwasaidia watoto kuyatazama masuala haya kwa ujasiri kupitia Kami.</p>
<p>Hata hivyo, kulikuwa na mkanganyiko wakati Kami alipoanza kuonyeshwa, hasa hasa nchini Marekani, ambapo wengi walikasirishwa na kuwa kipindi cha watoto kinanamchezesha mhusika mwenye VVU. <em>Haven on Earth</em> <a href="http://haven-on-earth.spaces.live.com/blog/cns!C13DE188EF218F14!382.entry?sa=500695506">anafafanua</a> mjadala huo:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ilitaarifiwa kuwa ujio wa Kami kwenye kipindi cha Sesame Street nchini Afrika Kusini ulikuwa unakaribishwa.(Nina wakati mgumu kukubaliana na ukweli huu kwa sababu kiwango kikubwa cha kukataa bado kipo), kulikuwa na mkanganyiko ulio wazi hapa Marekani. Ninakumbuka kusoma kuhusu suala hili (hii ni sababu ya mimi kufurahia kukutana na kipindi kikirushwa kutokea Afrika Kusini – nisingelifikiria kukitafuta). Iliondokea kuwa kundi la wabunge wa Congress wa chama cha Republican walituma barua kwa Rais wa Shirika la Utangazaji la Umma (PBS) linalorusha kipindi cha Sesame Street. Barua ilidai kwamba mipango ya kuleta mhusika kama huyo ambaye ni mwathirika wa UKIMWI nchini Marekani haikuwa sahihi, kwa kuzingatia umri wa watazamaji. Walipendekeza kwamba hatua hiyo ingeathiri ufadhili wa umma kwa Shirika hilo (PBS).”</p></blockquote>
<p>Kami hajawahi kuonekana kwenye kipindi cha Sesame Stree cha Marekani, ingawa amedhihirisha kuwa mhusika aliyefanikiwa sana kwenye kipindi cha Takalani Sesame na zaidi. Mwaka 2003, UNICEF <a href="http://www.unicef.org/media/media_16631.html">ilimteua</a> kuwa “Shujaa wa Watoto” duniani. Katika <a href="http://www.youtube.com/watch?v=9eXlNn-C8BY">video</a> hii, anaungana na Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton kutoa ujumbe kuhusu VVU/UKIMWI. Jamie, anayeblogu kwenye <em>No day but Today</em>&#8230;, <a href="http://phaino.blogspot.com/2006/12/world-according-to-sesame-street.html">anajadili</a> mafanikio mengine ya Kami:</p>
<blockquote><p> “Kwa sababu watoto wengi wa Afrika Kusini wanamfahamu mtu fulani mwenye UKIMWI, mhusika huyo amekuwa shujaa wa taifa, anayependwa na watu wa nchi hiyo. Kami ameonekana kwenye Umoja wa Mataifa na Benki ya Dunia na alihojiwa na Katie Couric. Ameteuliwa kuwa balozi wa UNICEF wa watoto na ameonekana kwenye vipande vya onyesho la Takalami pembeni mwa Desmond Tutu na Nelson Mandela.”</p></blockquote>
<p>Pamoja na mafanikio ya Kami, wanablogu wengine bado wanaamini kuwa si mhusika sahihi kwa toleo la Kimarekani la Sesame Street. Emily Meyer, anayeblogu kwa ajili ya darasa lake la heshima, <a href="http://hons101fall09eem.blogspot.com/2009/10/kami-hiv-muppet.html">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Ingawa ni muhimu kwa Wamerekani kufahamu kuhusu VVU/UKIMWI na hatari ya ugonjwa wenyewe, nadhani kuwafundisha watoto katika umri wa miaka miwili na mitatu ni kwenda mbali sana. Watoto wadogo kiasi hiki hawataweza kuelewa kuhusu VVU na hawataelewa madhara yake. Kama Kami alitakiwa aletwe Marekani kama njia kueneza elimu na kudhibiti UKIMWI, sidhani kama matokeo yaliyokusudiwa yangetokea&#8230;Watoto nchini Marekani hawalazimishwi kuhusika na masuala ya UKIMWI katika umri huo mdogo. Nadhani wakati sahihi kwa watoto nchini Marekani kujifunza kuhusu hatari ya virusi vya UKIMWI ni wanapokuwa wakubwa, kadri ya miaka kumi ama kumi na moja au wakati mwanafunzi anapoanza kujihusisha na vitendo vya mapenzi kimwili”</p></blockquote>
<p>Bado, wanablogu wengi, kama huyu hapa <a href="http://beckyluz.wordpress.com/2008/12/16/kami-the-hiv-positive-muppet/">anayeandika kwenye</a> <em>Muppets and History</em>, anamwona Kami kama mfano mwingine wa namna Sesame Street inavyosukuma mipaka. Wengine <a href="http://joburgjoblog.blogspot.com/2006/03/celebrating-aids-research.html">wanaonyesha upendo</a> wao kwa kikaragosi huyo na ujumbe anaowaletea watoto. Na wengine wanadhani anatakiwa atumike kwenye matoleo mengine ya Sesame Street. Katika blogu yake binafsi, Steisha Pintado <a href="http://steishapintado.wordpress.com/2008/12/18/final-grades-kami/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Anawaonyesha watoto kwamba ni sawa kumkumbatia mtu mwenye virusi vya UKIMWI, na anaeleza nini cha kufanya anapokuwa na kidonda kwenye kidole chake au kama umejikata mwenyewe. Anaifundisha hadhira ya watoto wadogo kuhusu kukabiliana na kuumwa na kupotelewa&#8230;.Ingawa ngono huwa haitajwi kamwe katika kuzungumzia hali ya Kami, watu wengine wamesema kuwa kuwepo kwa mhusika mwenye virusi vya UKIMWI lisingekuwa jambo sahihi kwa hadhira ya watazamaji wadogo. Mbunge mmoja hata alidai kuwa Warsha ya Sesame ingepoteza msaada wa kifedha kutoka serikalini kama ingerusha kipindi chenye mhusika huyo kwenye nchi yetu. Inashangaza kusikia maneno haya. Wazazi wanatumia muda mfupi (na unaopungua kila siku) na watoto wao, na wanaruhusu runinga kuwaelimisha zaidi na zaidi. Ni wazi wazazi wengi hawawafundishi watoto wao namna ya kuyakabili masuala nyeti  ya uelewa na kukubalika. Wazazi tayari wamewaruhusu Warsha ya Sesame kuingiza suala la kukubalika kwa wale wenye ulemavu na kuugua, na pia kwa wale wenye rangi na dini tofauti. Je, hii ina tofauti gani? </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-kikaragosi-kiliochoathirika-na-vvu-kwenye-kipindi-cha-sesame-chaelimisha-kuhusu-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika Kusini: Wimbo wa Taifa kwa Wanaoongea Kiingereza</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-wimbo-wa-taifa-kwa-wanaoongea-kiingereza/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-wimbo-wa-taifa-kwa-wanaoongea-kiingereza/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 11 Nov 2009 12:32:04 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[Language]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=626</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naNdesanjo Macha  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/10/south-africa-south-african-national-anthem-for-english-speakers/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://sarocks.co.za/2009/11/10/south-african-national-anthem-for-english-speakers/">Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza</a>: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya kutamka maneno yake na tatu ambao hatuongei lugha iliyo kwenye wimbo huo. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/afrika-kusini-wimbo-wa-taifa-kwa-wanaoongea-kiingereza/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Big Brother Africa msimu wa IV: Mageuzi yameanza</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/big-brother-africa-msimu-wa-iv-mageuzi-yameanza/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/big-brother-africa-msimu-wa-iv-mageuzi-yameanza/#comments</comments>
		<pubDate>Sat, 17 Oct 2009 06:30:15 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Entertainment]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=348</guid>
		<description><![CDATA[Big Brother Africa 4: Mapinduzi ni mfululizo wa nne wa vipindi vya kituo cha televisheni vinavyoonyesha maisha halisi vya Big Brother Africa, vilivyoanza Septemba 6, 2009. Kipindi hicho kimeshaanza kuzua mijadala na maoni kwenye mtandao wa intaneti kutoka kwa wanablogu na wasomaji wao. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/09/18/big-brother-africa-iv-the-revolution-is-on/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Big_Brother_Africa_4">Big Brother Africa 4: Mapinduzi</a> ni mfululizo wa nne wa vipindi vya kituo cha televisheni vinavyoonyesha maisha halisi vya Big Brother Africa, vilivyoanza Septemba 6, 2009. Mfululizo huu wa nne utakuwa hewani kwa siku 91 na mshindi atarudi nyumbani na kitita cha dola za kimarekani 200,000.</p>
<p>Kipindi hicho tayari kimezua mijadala mtandaoni kama ilivyokuwa kwa <a href="http://globalvoicesonline.org/2008/09/03/africa-here-comes-big-brother-africa-iii/">Big Brother III</a>. </p>
<p><a href="http://accraconsciousforever.blogspot.com/2009/09/big-brother-africa-iv-codename.html">Accra Conscious anatundika</a> taarifa za muhimu kuhusu kipindi hicho: </p>
<blockquote><p>Muda wa kulala hautakuwa ule ule tena kwa sababu washiriki wote 14 wanashindania kupata  usiku mtulivu wa kupanga namna ya kuzikamata Dola za Kimarekani 200,000 kama zawadi!<br />
Habari zaidi kuhusu BBA Mapinduzi.  </p>
<p>• Fedha za zawadi ya Big Brother Africa ya mwaka huu imezidishwa mara dufu –sasa itakuwa Dola za Kimarekani 200,000, bahati nasibu ya  ‘mshindi anachukua zote’. </p>
<p>• Msimu huu mpya una uwezo kama mara mbili zaidi wa uonekanaji na uwezo wa sauti kuliko ilivyokuwa msimu wa 1, 2 au wa 3: kutakuwa na kamera 40, ‘zinazoangalia kila kitu, na kufahamu yote’na vipaza sauti 100. </p>
<p>• Sheria za zamani za kuzuia njama kwenye jumba zimeondolewa na sasa washiriki watakuwa huru kuunda makundi, kujadili mikakati wazi wazi na kucheza mchezo kwa njia tofauti kabisa.</p>
<p>• Mwaka huu, watazamaji watatakiwa kuwapigia kura washiriki wanaowataka wabaki kwenye jumba badala ya kuwapigia kura wakaazi wanaotaka watoke. </p>
<p>• Mwaka huu kutakuwa na washiriki 14 watakaoishi kwenye jumba, ikilinganishwa na 12 wa misimu iliyopita, mwaka huu utajumuisha washiriki kutoka Msumbiji na Ethiopia. Nchi nyingine 12 ni: Angola, Botswana, Ghana, Kenya, Malawi, Namibia, Naijeria, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, Zambia na Zimbabwe. </p></blockquote>
<p>Rafiq anaandika kuhusu <a href="http://www.webaddict.co.za/2009/09/07/mxit-vote-big-brother-africa-4/">huduma ya bure ya SMS kwa jili ya kuwapigia kura washiriki</a>: </p>
<blockquote><p>Unapokuja wakati wa kupiga kura kwenye Big Brother Africa 4: The revolution kutuma SMS nyingi au kupiga kura kunaweza kuwa ghali sana. Kwa bahati kuna njia mbadala unazoweza kuwapiga kura kwa wakaazi wa jumba la Big Brother Africa kwa njia ya Mtandao na…*drum roll* MXit. </p>
<p>Hii ni njia ya haraka na rahisi kwa watumiaji milioni 14 wa huduma ya change MXit ili kuwapigia kura washiriki wawapendao wa BBA 4. Ninaona kuwa huu ni ushindi mkubwa kwa huduma ya MXit katika mchakato wao wa usiokoma wa kuwafikia watumiaji wengi zaidi barani kote Afrika. Nitaijaribu ili nipate kiasi fulani kabla na baada ya takwimu kutoka nchi zote 14 ambako washiriki wa BBA wanatoka na kuona kama idadi ya MXit kweli inaongezeka ndani ya sehemu hizo. </p></blockquote>
<p>David Ajao hafurahii <a href="http://www.davidajao.com/blog/2009/09/05/big-brother-africa-4-2009-the-revolution/#comment-46536">kushangiliwa kwa vitendo vya mahusiano ya kiholela-holela ya kimapenzi</a> kwenye kipindi hicho: </p>
<blockquote><p>Kusuasua au tahadhari yangu kuhusu Big Brother Africa siku zote imekuwa ni kule kushabikiwa kwa mahusiano holela ya kimapenzi. </p></blockquote>
<p>Noni anafikiri kuwa <a href="http://www.davidajao.com/blog/2009/09/05/big-brother-africa-4-2009-the-revolution/#comment-46658">toleo la mwaka huu la Big Brother linachefua</a>: </p>
<blockquote><p>BIG BROTHER INACHEFUA MWAKA HUU! WAVULANA WANA SURA MBAYA! KWA NINI BIG BROTHER MTUKATISHE TAMAA HIVI? HAKUNA HATA WAVULANA 2 AU 3 WENYE SURA NZURI KWENYE JUMBA LILE! NIMEKATISHWA TAMAA. </p></blockquote>
<p>Mika <a href="http://mikastefano.wordpress.com/2009/09/07/big-brother-africa-4/">anawachambua washiriki</a>:</p>
<blockquote><p>Jeremy kutoka Kenya anaonekana ni mzuri wa sura, na Itai wa Zimbabwe anaonekana kama ana maumbile makubwa…Siwezi kungeja saa ya kuoga. Hannington wa Uganda anaonekana kama malkia, anajielezea kwa maneno matano (sita) kama “Mimi ni mungu kati ya wanaume” …Ummm poa dada! Ninashangaa jamaa wangapi ni mashoga? Ni suala la kujificha ushoga…? Potelea mbali, Quinn, wa Afrika Kusini alikuwa katika nne bora katika kumtafuta Kijana Mweupe DJ wa YFM.</p></blockquote>
<p><a href="http://rafshizzle.blogspot.com/2009/09/big-brother-4-revolution-starts-with.html/">Na hivyo ndivyo anavyofanya Rafshizzle</a>, mwanablogu kutoka Uganda: </p>
<blockquote><p>Hannington Kuteesa Kavuma – ni mtoto wa Jaji Kavuma na Mbunge Ruth Kavuma. Ndio kwanza amerudi kutoka Malaysia alikokuwa akisoma kozi  ya Teknolojia ya Habari (IT). Huwezi kuamini tulikuwa na huyu jamaa pale kwenye Klabu ya Rugbi ya Kampala na alikuwa hatuambii kitu, naam, kila la heri kwake. Wakati huo huo, Mganda mwingine anaitwa Filbert Okure na bado tunakusanya habari zake kwa bakia hapa hapa. (Wanatuambia, Hannington atatolewa mbu). Haidhuru, Zimbabwe imemtuma Itai Makumbe –mwenye umri wa miaka 31 anayependa siasa. Na ulihisi sawa sawa, wanasiasa wengi wanachosha isipokuwa majamaa kama Ken Lukyamuzi, Rais Museveni na Idd Amin (Mungu Amweke Pema Peponi). Kenya nayo ina wawili Edward Muthusi (kwa jina lingine Teddy) na Jeremy Ndirangu. Naijeria imemtuma Kevin Chuwang – kijana asiye na kazi mwenye miaka 27. Kutoka Botswana: Kaone Ramontshonyana – Kwa kweli nimeshindwa kabisa kumwelewa huyu kijana. Ethiopia inayoingia kwa mara ya kwanza imewakilishwa na Yacob Yehdego –ameahidi kuwa mkweli, jambo ambalo karibu kila Muethiopia  hulisema. Jina lake la utani ni Yac. Tunahitaji kungoja…Mwenyeji Afrika Kusini ina Mzungu anayeitwa Quinn Silder –kwa umri wake wa miaka 21, huyu mcheshi mweupe anakuwa mshiriki mdogo zaidi kuliko wote jumbani; pia ni Dj na mtangazaji wa redio kwa hivyo lazima awe mjuzi wa namna ya kuwaburudisha watu. Nchi nyingine inayoshiriki kwa mara ya kwanza, Msumbiji imemtuma Leonel Estevda mwenye umri wa miaka 23.  </p></blockquote>
<p>Pen Powder <a href="http://penpowder.blogspot.com/2009/09/ghana-let-down-in-bba-4.html">anakosoa wazo la mwaka huu la Mapinduzi</a>: </p>
<blockquote><p>Nilikuwa naanza kufurahia mambo mapya kwenye Big Brother Africa Revolution lakini baada ya kushuhudia kuondolewa kwa Ras Wayo na kutotambulishwa mshiriki wa kike wa Ghana, Ninadhani dhana ya mageuzi haikufikiriwa kwa kina chake na pengine si jambo zuri. Mambo mengine yanayotokea hayana maana kabisa katika kina chake: kwa nini wawepo washiriki wengi zaidi kutoka nchi fulani zaidi ya nchi nyingine wakati kwa kweli dhana ya kuwa na kipindi cha bara zima ilikuwa ni kuzileta nchi mbalimbali pamoja. Baada ya kuingizwa washiriki 12 wa kike kwenye jumba jumapili, hivi sasa kuna Wanaijeria 4, Wakenya 2 na washiriki wawili wawili wa nchi nyingine wakati Ghana haina mwakilishi kipindi hiki. Hivi hii ni kwa ajili ya kuongeza mvuto kwa watazamaji?  Au baadhi ya nchi zinawakilishwa zaidi kwenye jumba hilo kwa sababu tu M-net/DStv inataka kuvuna faida zaidi kutoka kwenye nchi hizo? Jambo moja la kuchekesha ni kwamba Big Brother imeruhusu “njama za kura” msimu huu na inaonekana kuwa makundi yatatengenezwa kufuata utaifa.  Hili bila shaka litatengeneza  chuki miongoni mwa washiriki na bado eti M-net wakaja kwa ujasiri kusema kwamba wamebadili kanuni za kupiga kura mwaka huu ili eti watu wapige kura kumwokoa wampendae badala ya kupiga kura kumtoa wasiyemshabikia ili kusisitiza ‘uchanya’ badala ya ‘uhasi.’ Katika tangazo lisilotarajiwa, mwakilishi wa Ghana, Ras Wayo akawa mshiriki wa pili kuondolewa kutoka kwenye jumba la BBA wakati wa kipindi cha kwanza cha Kutolewa kwa mshiriki. Wayoe alipanda jukwaani huku washabiki wa jukwaani wakiliimba jina lake juu ya muziki wa miondoko ya Rege. Alimwambia IK, mwongoza kipindi, kwamba hakustaajabishwa kutoka jumbani na kwamba hafikiri kwamba mwenendo wake wa maisha ya Kirastafariani ilichangia kuwafanya watazamaji kutokumpigia kura. Naam, wa-Ghana hawajastaajabishwa pia kwa sababu lafudhi yake ya Kijamaika ya Patois ilikuwa ni jambo lilizongumzwa sana mara tu alipotambulishwa kwenye jumba hilo. Hivyo, kabla ya yote, ni kwa nini Ras Wayo alichaguliwa kuiwakilisha Ghana? M-net na watayarishaji wa kipindi walimchagua mtu ambaye kwa mtazamo wao angetoa thamani kubwa ya burudani kwa watazamaji kutoka kwenye nchi washiriki.</p></blockquote>
<p><a href="http://narcissusconceitus.blogspot.com/2009/09/big-brother-africa-4.html">Narcissus anauliza</a>, “hivi ni mimi tu au ni kila mtu anahisi Itai ni shoga?”: </p>
<blockquote><p>Hivi vijimambo vidogo vilistua rada zangu za kuwatambua mashoga kufikia upeo wake:  Moja ya vipindi anavyovipenda zaidi ni, subiri, America’s Next Top Model (Najua!.) Moja ya tabia zake mbaya ni pamoja na, kujitazama na kujichekelea mwenyewe kwenye kioo (haloo huku ni kujipa umuhimu kupita kiasi, aha). Mwisho, na kwa vyovyote si kwa umuhimu, akishinda mipesa hiyo, anapanga kuzitumia kugharamia safari za London, Paris, New York na Los Angeles, kweli? Wacha!<br />
Hizi mbili ndizo sababu pekee zinazonifanya ‘niweze’ kutazama kipindi hicho. Ninategemea jumba hilo limesheheni vipodozi na Geisha ambavyo “haviishi upesi”, kwa sababu itakuwa wiki ndefu kwa vijana, hebu nicheke mie. Kwa uwazi hata hivyo, Nilitegemea “mapinduzi” zaidi, na si kurejea dhana ambazo zimekwishatumika kule Uhispania katika toleo lao la Big Brother. </p></blockquote>
<p>Ms B anajichukulia yeye kuwa shabiki “’asiye na aibu wa kipindi hiki cha kuonyesha uhalisia” <a href="http://mycrimsonpages.blogspot.com/2009/09/big-brother-africa-4.html">Anazungumzia urembo wa washiriki wa kike</a>: </p>
<p>Mapodozi yalikuwa ya ajabu, hakuna mwanamke mweusi  duniani mwenye mashavu mekundu!!! Hakuna!! Ukitaka mtafute!!! Malkia ‘jike dume’ alikuwa na nyusi ndefu zinazoweza kumdaka nzi na Nonhle alikuwa na kucha zilizopakwa rangi ya njano ambayo haikuwa na cha kusaidia kwenye mavazi yake. Najua wanamitindo mara nyingine huwa hawaoanishi rangi ili kuzioanisha lakini ilionekana kama vile hakuwa na hakika avae vipi. Hatuwezi wote kuwa akina Rihanna sasa, sivyo? </p>
<blockquote><p>Nachukia wanawake wanapofanya hivyo! Hakuna kinachovutia (kwangu) mtu kuoneakana kama kituko. Kujiremba kunapaswa kuuzidisha zaidi urembo wako, na sio kuuficha. Rahisisheni kazi nyie wajinga!!! Na hawa wanawake wanawakilisha wanawake wengine wa Kiafrika wanapotoka, du masikini!!!</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/big-brother-africa-msimu-wa-iv-mageuzi-yameanza/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Ujio wa Mkonga wa Seacom Wazua Mjadala</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 27 Jul 2009 14:18:29 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Mozambique]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Tanzania]]></category>
		<category><![CDATA[Uganda]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=276</guid>
		<description><![CDATA[Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. Seacom, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, ilianza kutumika moja kwa moja Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana. ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rebekah-heacock/">Rebekah Heacock</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/24/africa-the-arrival-of-seacom-cable-sparks-debate/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. <a href="http://www.seacom.mu/index2.asp">Seacom</a>, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, <a href="http://www.guardian.co.uk/technology/2009/jul/23/east-africa-broadband-revolution">ilianza kutumika moja kwa moja</a> Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana.<br />
<div class="wp-caption aligncenter" style="width: 310px"><img alt="Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/07/picture-1-300x271.png" title="Seacom" width="300" height="271" /><p class="wp-caption-text">Seacom inaunganisha mwambao wa Afrika ya mashariki na Ulaya pamoja na Asia</p></div></p>
<p>Miji ya Johannesburg, Nairobi na Kampala <a href="http://www.google.com/hostednews/afp/article/ALeqM5iHrESmY6eTaALo3tbsjwGSPkPP1Q">iliunganishwa </a>Alhamisi, na Addis Ababa pamoja na Kigali inatarijia kufuata. Ujio wa mkonga huo ulipangwa kufikav mnamo mwanzoni mwa mwezi wa saba, lakini <a href="http://allafrica.com/stories/200906290065.html">mashumbulizi ya maharamia</a> nje kidogo ya pwani ya Somalia yalichelewesha utekelezaji.</p>
<p>Kiunganishi hiki cha chini ya bahari kinatarajiwa kupunguza gharama za upana wa masafa kwa asilimia 90 na kuongeza uwezo wa makongamano yanayotumia video, urushaji wa matangazo ya televisheni yenye picha za hali juu pamoja na huduma za intaneti zenye mwendo wa kasi kwenye mwambao wa Afrika ya mashariki.</p>
<p>“Mmmh… nasuburi kwa hamu kuanza upakuzi,” anaandika <a href="http://itblogkenya.blogspot.com/2009/07/seacom_22.html">IT blog Kenya</a>.</p>
<p>Huko Uganda, Josh kutoka blogu ya <a href="http://inanafricanminute.blogspot.com/2009/07/kung-fu-baby-and-seacom-cable-launch.html">In African Minute</a> ameshaanza kubaini tofauti:</p>
<blockquote><p>Mbinu inayojulikana ili kuangalia video za YouTube barani Afrika ni kwa kubonyeza alama ya kugandisha video wakati inapoanza, subiri kwa dakika 20 (au zaidi) mpaka hapo video itakapopakuliwa yote, halafu angalia. Leo nipo kwenye sherehe ya kuzindua SEACOM… kwenye kona ya chumba cha kongamano, Peter Mereton Meneja wa ununuzi wa SEACOM, alinipa ishara niionyeshe tarakilishi yenye ukurasa wa YouTube uliokuwa tayari. Tuliizindua <a href="http://www.youtube.com/watch?v=bxAirY-5QCQ">Kung Fu Baby</a> na kwa mara ya kwanza katika Afrika, niliona video ya YouTube ikipakuliwa yote na kuchezwa katika sekunde 6.</p></blockquote>
<p>Munashe wa <a href="http://www.techmasai.com/2009/07/24/seacom-the-under-sea-cable-has-arrived/">TechMasai</a> naye anafurahia:</p>
<blockquote><p>Mkonga wa chini ya bahari wa Seacom tuliouandika <a href="http://www.techmasai.com/2008/04/02/eassy-east-african-submarine-cable/">kitambo kidogo nyuma</a> umetimia na umeanza kufanya kazi leo. Ni mchakato wa kimapinduzi kutokana na ukweli kwamba nchi ambazo zitautumia hivi sasa, ambazo zinajumuisha kenye, Uganda, Msumbiji, Afrika Kusini na Uganda.</p>
<p>… Ni wakati mzuri kwa Afrika, Ninaweza kudhibitisha hilo kwa Kenya ambayo mpaka hivi sasa ilitegemea setilaiti kwa ajili ya mahitaji yake ya intaneti.</p></blockquote>
<p>Jeremy, mwanablogu wa Kinaijeria anayeandika katika <a href="http://naijablog.blogspot.com/2009/07/east-africa-goes-broadband.html">NaijaBlog</a>, analinganisha Seacom na mikongo mbalimbali ya Afrika magharibi. Afrika Magharibi bado ipo chini:</p>
<blockquote><p>Afrika ya Mashariki imekwenda na huduma ya masafa mapana ya intaneti… wakati Afrika ya Magharibi bado ipo kwenye sehemu ya kuanzia mbio (kwa kweli, bado ipo kwenye vyumba vya kubadilishia nguo ikijiuliza ni nini cha kuvaa) wakiwa na SAT3 isiyo na manufaa ambayo hukatika-katika, pamoja na Glo1 9je wakandarasi wa Alcatel wamekwama chini ya mabiwi ya mchanga?) na wakandarasi wengine wawili wapya, WACS na Main1 bado wakiwa mbali zaidi ya upeo (mwaka kesho kama tukiwa na bahati). Afrika ya mashariki imekumbatia huduma ya masafa mapana ya intaneti na kushika mbio wakati Afrika ya Magharibi  inasuasua na kukodoa macho.</p></blockquote>
<p>Twita nayo inanguruma na habari za Seacom. Baadhi ya watumniaji wana shauku, wakati wengine wana mashaka:</p>
<p>“Bado sijaweza kuamini kuwa unaweza kupakua mtandao wote wa Intaneti kupitia mkongo mmoja mdogo wa manjano <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a>&#8220;<br />
— <a href="http://twitter.com/ncallegari/statuses/2815733071">ncallegari</a></p>
<blockquote><p>“Seacom ilizinduliwa_kwa hakika_leo. Na tuangalie itachukua muda gani kwa mawakala wa intaneti kuongeza kasi na kupunguza gharama…”<br />
— <a href="http://twitter.com/dnyaga/status/2808617797">dnyaga</a></p>
<p>‘je ni mimi au ni huduma za intaneti katika Nairobi ambazo zimezorota leo tangu <a href="http://twitter.com/search?q=%23seacom">#seacom</a> ilipozinduliwa? Pengine uwezo wa mkubwa wa inteneti unaburudika na mandhari ya bahari kabla ya kutufikia”<br />
— <a href="http://twitter.com/mentalacrobatic/statuses/2804058608">mentalacrobatic</a>
</p></blockquote>
<p>Mengi ya mashaka juu ya Seacom yapo kwenye suala la bei: japokuwa baadhi ya wataalamu wa mambo wanadai kuwa gharama za upana wa masafa zitashuka kwa asilimia 90, wengine wanaamini kwamba makato ya gharama yanaweza yakawa madogo zaidi. <a href="http://www.kachwanya.com/?p=428">Kachwanya</a> anaandika:</p>
<blockquote><p>Katika dunia sawa gharama zinapaswa zishuke kwa zaidi ya asilimia 90, hivi sasa inawagharimu mawakala wa kutoa intaneti dola 6500  za Kimarekani (takriban Shilingi 487500 za Kenya) kwa kila kipimo cha Megabiti za upana wa masafa, lakini shika pumzi yako, usitarajie miujiza katika hili. Hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa UUnet Tom Omariba alidai kuwa mikonga itashusha gharama kwa asilimia 20-30.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu <a href="http://www.truekenyan.com/2009/07/23/oh-kenyans-we-have-been-duped-again/">TrueKenyan</a> guswa na suala la uwazi:</p>
<blockquote><p>
Seacom wamekataa katu kutuwekea wazi, sisi walaji wa intaneti, ni mawakala gani wa kusambaza intaneti walionunua upana wa masafa kutoka kwao. Hivyo bado tupo kizani na hatufahamu ni wapi tunapoweza kununua huduma ya intaneti yenye uhakika na kwa bei nafuu… kwa hiyo jambo pekee ninaloweza kufanya ni kuendelea na wakala wangu wa intaneti huku nikiitazama mashine wakati ikipakua kurasa kwa kasi inayoamua yenyewe huku nikiwaza kuwa siku moja ndoto yetu itatimia. </p></blockquote>
<p>Akitoa maoni katika blogu ya Mtanania <a href="http://issamichuzi.blogspot.com/2009/07/jk-azindua-kituo-cha-mkongo-wa-fibre.html">Issa Michuzi </a>[SW}, mdau pia anahofu juu ya gharama, japokuwa ana matumaini makubwa ya baadaye: </p>
<blockquote><p>Asanteni sana kwa huo mkonga. Sasa kutandaza fibre-optic cables kwenye miji mbalimbali tunaanza lini? Manake kuwa na inter-country connection wakati within the country hatuna connection nzuri bado gharama zitakuwa juu na kwa maoni yangu tutakuwa tuna-under utilise capacity ya hiyo under sea cable. For the moment, well done! For the future, we have to work had!</p></blockquote>
<p>Kwa <a href="http://jellyfishcoolman.wordpress.com/2009/07/24/seacom-goes-live/">Jellyfish</a>, ambaye anayatupilia mbali masuala ya gharama kwa kusema kuwa ongezeko la kasi la kiasi hicho na kiwango cha huduma mkwa kawaida huenda sambamba na ongezeko la bei, ujio wa Seacom ni jambo zuri:</p>
<blockquote><p>
Katika tukio lililoratibiwa na kutangzwa sana SEACOM iliwasha funguo ambayo mara moja ilieneza Terabiti za upana wa masafa katika kasi ya mwanga kupitia nyuzi za vioo zilizotengenezwa na kupigwa msasa katika kiwango cha hali juu. </p></blockquote>
<p>Na kwa mwanablogu wa Afrika Kusini <a href="http://twitter.com/akianastasiou/status/2797795511">Aki Anastasiou</a>, “Hii ni MB ndogo kwa talakilishi yangu ya mapajani, TB moja kubwa kwa Afrika.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-ujio-wa-mkonga-wa-seacom-wazua-mjadala/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika: Obama Atumia Nyenzo Mpya za Habari Kuzungumza na Waafrika</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-obama-atumia-nyenzo-mpya-za-habari-kuzungumza-na-waafrika/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-obama-atumia-nyenzo-mpya-za-habari-kuzungumza-na-waafrika/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 22 Jul 2009 13:06:14 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Ghana]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Kenya]]></category>
		<category><![CDATA[Nigeria]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Software & Tools]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=238</guid>
		<description><![CDATA[“Umeshawahi kutaka kumuuliza kijana wetu wa Nyangoma maswali yoyote? Kwa maneno mengine, je ungependa Rais wa Marekani, Barack Obama ajibu maswali yako?,” ndivyo inavyoanza makala kwenye blogu ya Hot Secrets inayohusu matumizi ya Obama ya zana mpya za habari ili kukutana na kuongea na Waafrika wa kawaida.  ]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/07/10/africa-obama-uses-new-media-to-talk-to-africans/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>“Umeshawahi kutaka kumuuliza kijana wetu wa Nyangoma maswali yoyote? Kwa maneno mengine, je ungependa Rais wa Marekani, Barack Obama ajibu maswali yako?,” <a href="http://hotsecretz.blogspot.com/2009/07/sms-son-of-kogelo-direct.html">ndivyo inavyoanza makala kwenye blogu ya Hot Secrets</a> inayohusu matumizi ya Obama ya zana mpya za habari ili kukutana na kuongea na Waafrika wa kawaida.  </p>
<p>Barack Obama anazuru <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Ghana">Ghana</a> tarehe 10 mpaka 11 Julai. Hii itakuwa ni ziara yake ya kwanza ya kihistoria kwenye nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara na atatumia nyenzo kama Twita, Facebook na Ujumbe mfupi wa Simu za kiganjani (SMS) kuzungumza moja kwa moja kwa moja na Waafrika. </p>
<p>Erik Hersman anayeblogu kwenye <a href="http://whiteafrican.com/">blogu ya White African</a>, <a href="http://whiteafrican.com/2009/07/02/obamas-new-media-strategies-for-ghana/">anajadili majukwaa-nyenzo ya habari</a> ambayo Obama anakusudia kuyatumia ili kuwafikia Waafrika zaidi ya wale wa Ghana. Erik alifanya kazi na ikulu ya Marekani katika kuandaa mikakati ya nyenzo mpya za habari kwa ajili ya Ghana na Afrika. Anaandika: </p>
<blockquote><p>Redio bado ni nia ya kwanza ya mawasiliano barani Afrika, na Ghana ina sekta ya redio iliyo hai na yenye kushirikisha jamii zilizo vitongojini na jamii ya kitaifa.<br />
Kama kila mmoja anavyojua, usambaaji wa simu za kiganjani umekua kwa kasi ya mlipuko barani Afrika, hii inamaanisha kwamba Ujumbe mfupi wa Simu (SMS) ni njia ya kidemokrasia ya kupata mrejesho kutoka kwa watu wa kila hali nchini. (jambo la kuchekesha ni kuwa huduma hii haipatikani kwa wakazi waaoishi Marekani – mengine juu ya suala hili yapo chini)<br />
Mwisho, hakuna mtandao wa kijamii ulioazaliwa nchini Ghana, na kama ilivyo kwa nchi nyingine kote Afrika, Facebook imeweza kusambaa kwa kiwango kizuri. Nchini Ghana, watumiaji ni zaidi 100,000, kwa hiyo inaleta maana sana kwa timu inayoshughulikia nyenzo za habari kuwafikia watu bila kuzisambaza nguvu zao kwenye huduma nyingi nyingine.  Kuwa na huduma ya Twita kama nyenzo ya akiba ni jambo linalotarajiwa, kwa sababu kutakuwa na matumizi huko vile vile.  </p></blockquote>
<p><a href="http://whiteafrican.com/2009/07/02/obamas-new-media-strategies-for-ghana/">Na anatundika </a>habari za kina kutoka Ikulu ya Marekani:</p>
<blockquote><p>SMS. Tunazindua jukwaa la SMS ili kuwaruhusu wananchi kutuma maswali, maoni na maneno ya ukaribisho (Kwa Kiingereza ama Kifaransa).  Kwa kutumia vifupisho vya tarakimu vya mahali husika kwa huduma ya  SMS nchini Ghana (1731) , Nigeria (32969) , Afrika Kusini (31958) na Kenya (5683), vile vile kutumia tarakimu ndefu kwa ajili ya wengine wote duniani *, Waafrika na raia ulimwenguni kote watahamasika kumwandikia Rais ujumbe mfupi wa maneno. Washiriki wa SMS wataweza pia kuomba kupatiwa dondoo za hotuba kwa Kiingereza na Kifaransa. Nambari zitakazotumika kwa ajili ya kuandikisha simu za mkononi kwa Afrika ni: 61418601934 na 45609910343.</p>
<p>Redio. Hotuba ya Rais itarushwa moja kwa moja kupitia vituo vya redio vya kitaifa na vile vya kanda wakati wa hotuba. Baada ya hotuba, jumbe zote zilizorekodiwa majibu ya Rais kwa jumbe zote fupi (SMS) zilizopokelewa zitapatikana katika vituo vya redio na wavuti. Rais anatarajia kujibu maswali anuai na maoni kwa mpangilio wa mada na eneo. Sauti zilizorekodiwa pia zitapatikana kwa ajili ya matumizi ya kila mtu atakayezihitaji kupitia wavuti ya Ikulu ya Marekani na teknolojia ya iTunes.<br />
Video. Hotuba itarushwa moja kwa moja kwenye www.whitehouse.gov/live. Alama-funguo za video hiyo inapatikana ili uweze kuitumia katika wavuti yoyote.<br />
Mazungumzo ya moja kwa moja kwenye mtandao. Tutawezesha gumzo la mtandaoni linalihusu hotuba kwenye Facebook (itakuwa hapa http://apps.facebook.com/whitehouselive). Ikulu ya Marekani itatengeneza “tukio” la Facebook kutokana na hotuba ambapo washiriki kutoka ulimwengu mzima wanaweza kujibishana. Anuani ya Twita ( #obamaghana) pia itatengenezwa na kutangazwa ili kuboresha maoni juu ya tukio hilo. </p></blockquote>
<p>Watumiaji wa mtandao wanaweza kutuma maswali yao kwenye <a href="http://allafrica.com/feedback/obama-ghana-2009.html">wavuti ya AllAfrica</a>: </p>
<blockquote><p>
Nafasi yako ya kumuuliza Rais Obama kuhusu Afrika:<br />
Unataka kumuuliza nini Rais Obama anapojiandaa kuitembelea Afrika ya Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa mara ya kwanza akiwa kiongozi wa Marekani –akitua Ghana tarehe 10-11 Julai? Andika swali lako hapa, na tutakusanya maombi yenu. Tafadhali, kama ungependa, usiasahau kutaja umri na kazi unayofanya.   </p></blockquote>
<p><a href="http://blog.foreignpolicy.com/posts/2009/07/07/africans_invited_to_text_obama_before_ghana_speech">Kwa mujibu wa Michael Wilkerson</a> anayeandika katika blogu ya Foreign Policy, matumizi ya Obama ya nyenzo mpya za mawasiliano kunaweza kuongeza umaarufu wake duniani:  </p>
<blockquote><p>Kama hapatakuwa na matatizo, udhihirishaji huu wa kupenda kupata mitazamo ya Waafrika huenda utapandisha umaarufu wa Obama duniani, ambao tayari ni kama mara mbili ya ule wa Marekani yenyewe. Katika soko la kitaalii la mjini Accra, fulana za Obama na michoro zinauzwa haraka kutoka kwenye safu na Waghana wanategema kupanda kwa biashara ya utalii baada ya ziara.</p></blockquote>
<p><a href="http://afrigator.com/link/url/?url=http%3A%2F%2Fghanapundit.blogspot.com%2F2009%2F07%2Fafrica-texts-obama-before-visit.html&#038;return_url=http%3A%2F%2Fafrigator.com%2Fhome&#038;blogid=13860&#038;postid=1189397">Mwanablogu Ghana Pundit anaripoti</a> kuwa maelfu ya jumbe za simu za viganjani yametumwa kwa Obama:</p>
<blockquote><p>Rais wa marekani amepokea maelfu ya jumbe za simu za viganjani zinazoihusu Afrika baada ya kuwataka watu kumtumia maswali kabla ya ziara yake nchini Ghana siku ya Ijumaa. </p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-obama-atumia-nyenzo-mpya-za-habari-kuzungumza-na-waafrika/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika Kusini: Kuvuvuzela au Kutovuvuzela?</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-kusini-kuvuvuzela-au-kutovuvuzela/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-kusini-kuvuvuzela-au-kutovuvuzela/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 19 Jul 2009 09:25:25 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Christian Bwaya</dc:creator>
				<category><![CDATA[Arts & Culture]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Humor]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sport]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=236</guid>
		<description><![CDATA[Mjadala kuhusu kifaa maarufu kinachoitwa vuvuzela kinachopigwa na mashabiki wa mpira wa miguu Afrika Kusini umetawala katika blogu mbalimbali duniani tangu kuanza kwa Kombe la Mabara la mwaka huu nchini Afrika Kusini, lililohitimika wiki iliyopita. Waandishi wa habari, watazamaji wa televisheni, makocha na baadhi ya wachezaji wa kigeni walitoa wito wa kusitisha matumizi ya kifaa hiki katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini. Mabishano haya yana sauti kubwa kama chombo chenyewe.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/bwaya/'>Christian Bwaya</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/06/30/south-africa-to-vuvuzela-or-not-to-vuvuzela/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Mjadala kuhusu kifaa maarufu kinachoitwa vuvuzela kinachopigwa na mashabiki wa mpira wa miguu Afrika Kusini umetawala katika blogu mbalimbali duniani tangu kuanza kwa Kombe la Mabara la mwaka huu nchini Afrika Kusini, lililohitimika wiki iliyopita. Waandishi wa habari, watazamaji wa televisheni, makocha na baadhi ya wachezaji wa kigeni walitoa wito wa kusitisha matumizi ya kifaa hiki katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini. Mabishano haya yana sauti kubwa kama chombo chenyewe. Kuna hata <a href="http://www.banvuvuzela.com/">kura ya mtandao ya kusitisha chombo hiki</a>. FIFA imeruhusu vuvuzela litumike wakati wa kombe la dunia mwaka 2010 ikitoa hoja kwamba hiyo ni sehemu ya utamaduni wa mpira wa Afrika Kusini. </p>
<p><a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Vuvuzela">Haya ni maelezo ya Wikipedia</a> kuhusu vuvuzela: </p>
<blockquote><p>
pembe ya kupuliza, yenye urefu wa kadiri ya mita moja , kwa kawaida hupulizwa na mashabiki katika mechi za mpira wa miguu huko Afrika Kusini. Asili ya jina hili ina utata. asili ya jina inaweza kuwa ni ya Kizulu yenye maana ya “kupiga kelele,” inayotokana na sauti  kupulizwa kwake ya “vuvu” , au kutokana na lugha ya mtaani inayohusiana na neno “kuoga”</p></blockquote>
<p>Mitazamo katika ulimwengu wa blogu imepishana sana. Wanablogu wengine wanakerwa na sauti inayotoka kwenye vuvuzela wakati wengine wanatoa wito wa watu kuwa na uvumilivu pamoja na uelewa wa mambo. Mwanablogu mmoja amefika mbali ha hata kudai kwamba kifaa hiki kinaeneza virusi vya UKIMWI!</p>
<p>Dave Taylor anaelezea vuvuzela kama <a href="http://www.southafricaproject.org/blog/2009/06/should-fifa-ban-the-vuvuzela-from-world-cup-2010/">“kifaa cha asili cha ghasia za mpira wa miguu”</a></p>
<p><a href="http://www.worldcupblog.org/world-football/death-to-the-vuvuzela.html">Kwa Chris wa blogu ya Kombe la Dunia</a>, vuvuzela ni “ile sauti kubwa ya jeshi la wadudu (<em>kama vile nzige</em>)”:</p>
<blockquote><p>Ile sauti kubwa kama ya kundi kubwa la nzige ambayo umekuwa ukiisikia katika kila mchezo Kombe la Mabara si, kwa hakika, mojawapo ya yale ‘mapigo’ yanayoelezwa katika biblia. Hiyo ndiyo inaitwa vuvuzela…</p></blockquote>
<p>Capitals Kremlin anaichukulia vuvuzela kama <a href="http://www.capitalskremlin.com/20090619102/2009-articles/june-2009/is-the-nhl-ready-for-the-vuvuzela.html">kipiga kelele kinachokera kuliko vyote</a>: </p>
<blockquote><p>Mabibi na Mabwana, Caps Kremlin anayofuraha kuwaletea: kipiga kelele kinachokera zaidi duniani, vuvuzela.</p></blockquote>
<p>Kuna <a href="http://afrigator.com/link/url/?url=http%3A%2F%2Fhealthblogs.24.com%2FViewComments.aspx%3Fblogid%3D04e33c05-58ce-4c36-89c5-978b35d54cf7%26mid%3Dfbb9aba7-4257-4a31-ac9b-ce9f91ede937&#038;return_url=http%3A%2F%2Fafrigator.com%2Fsearch">maelezo marefu ya vuvuzela</a> kutoka 24.com:</p>
<blockquote><p>…chukua mchezo kutoka Uingereza unaoitwa kandanda, chukua kamasi ya kinyago chenye macho yanayong&#39;ara na pua yenye unga ya mfanyabiashara wa kutangaza bidhaa, pamoja na wabia wa makampuni ya pombe ambao wanataka kuongeza hisa kwenye soko la biashara,  muongeze jamaa aitwaye Van Schalkwyk mwenye ile akili-ya-kuhepa uchanganye na kiwanda cha plastiki, unajua unapata nini? Vuvuzela. </p></blockquote>
<p>Pitch Invasion anaiita vuvuzela “<a href="http://pitchinvasion.net/blog/2009/06/21/satans-instrument-the-vuvuzela-and-noisemaking-in-world-football/">Chombo cha Shetani.</a>” </p>
<p>Karibu kwa  <a href="http://afrigator.com/link/url/?url=http%3A%2F%2Fhealthblogs.24.com%2FViewComments.aspx%3Fblogid%3D04e33c05-58ce-4c36-89c5-978b35d54cf7%26mid%3Dfbb9aba7-4257-4a31-ac9b-ce9f91ede937&#038;return_url=http%3A%2F%2Fafrigator.com%2Fsearch">plastic Africa</a>:</p>
<blockquote><p>halafu fuaatilia na mapigo makali ya taarifa rasmi za kutangaza habari juu ya jinsi pembe-ya-kudu ulivyokuwa ikitumika zama za kale kupiga mbiu za kuitawanakijiji mkutanoni, Vikundi vya wakristo vikidai kuwa hiyo ni sehemu ya ibada zao takatifu na tunaishia na mechi za soka ambazo zinaweza  kuangaliwa kwenye televisheni pale tu sauti ikiwa imeminywa. Na kama huipendi (<em>vuvuzela</em>), ni lazima uwe mbaguzi au mbaya zaidi kati ya wale jamaa ambao wakisikia neno “utamaduni” tayari huanza kuzifikia bunduki. </p>
<p>Karibia kwenye blogu ya Afrika plastiki. Na usikitikie fursa iliyopotea. </p></blockquote>
<p>Kutoka blogu ya Foreign Policy, “<a href="http://blog.foreignpolicy.com/posts/2009/06/19/the_world_cups_biggest_concern_is_a_trumpet">Jambo kubwa zaidi katika kombe la Dunia ni tarumbeta</a>,”</p>
<blockquote><p>Miaka mitano nyuma, wakati Afrika kusini iliposhinda haki ya kuandaa Kombe la Dunia la mwaka 2010, wengi walitaka zaidi kujua ikiwa nchi hiyo ilikuwa na miundo mbinu inayohitajika kuwa mwenyeji wa mashindano haya makubwa. Mwaka moja tu ukiwa umebakia, ingawa, waangalizi wengi wanakubaliana kwamba nchi imeshinda mtihani huo; badala yake, walalamikaji wakubwa wanatumia muda mwingi kulalamikia chombo kinachoitwa vuvuzela. </p></blockquote>
<p>ReasonCheck <a href="http://afrigator.com/link/url/?url=http%3A%2F%2Fwww.reasoncheck.com%2F2009%2F06%2F26%2Fthe-great-vuvuzela-war%2F&#038;return_url=http%3A%2F%2Fafrigator.com%2Fsearch">anawaza</a>, “…laiti haya mapagani zuzu yangejua furaha ya kutengeneza nota za muziki kwa kutumia mabomba haya ya jehanamu”:</p>
<blockquote><p>Kama ulifanikiwa kuipata mechi yoyote kupitia luninga, bila shaka ulisikia sauti mbaya, kama ya kundi la wadudu wanaoleta kero. Lakini pengine inabidi kuwa pale kuielewa kero hasa ya kelele ile mbaya. Nilimchukua mwanangu kwenda kwenye mchezo usiku wa siku chache zilizopita na tumekuwa tukitaabika na kuumwa kwa vichwa tangu wakati huo, na ninashitukashituka wakati nikilala. </p>
<p>Ndipo nikawaza kwamba ikiwa haya mapagani zuzu yangeonyeshwa furaha ya kutengeneza nota za muziki kwa kutumia mabomba haya ya plastiki basi pangeweza kutokea mabadiliko ya kifikra kati yao na wangejaribu kuanza kupiga muziki. </p></blockquote>
<p>Pitch Invasion anaangalia <a href="http://pitchinvasion.net/blog/2009/06/21/satans-instrument-the-vuvuzela-and-noisemaking-in-world-football/">historia ya upigaji kelele kwenye mpira wa miguu duniani</a> akianzia na kipiga kelele maarufu Uingereza, yale manyanga au machekeche ya mbao: </p>
<blockquote><p>Kipiga kelele maarufu cha kwanza mpirani – na kilichokuwa kinapiga kelele hata kuifanya vuvuzela kunyong&#39;onyea - kilikuwa ni lile chekeche la mbao huko Uingereza.<br />
Akiandika katika jarida la Guardian, Simon Burnton alitegemea kwamba “huenda Afrika Kusini ingejifunza kutoka kwenye yale manyanga ya mbao yaliyotumbuiza kandanda la Uingereza katika kipindi cha baada ya vita –na yaliyopoteza umaarufu wakati kila mmoja alivyogundua jinsi yanavyokera. natumaini kuwa siku hivi karibuni hatima mthili ya hiyo itayafikia haya mavuvuzela.”<br />
Hata hivyo, ni mageuzi ya kimsingi katika utamaduni mzima wa mashabiki na siyo utambuzi kwamba manyanga yale yalikuwa yanakera,ndiyo yaliyoyaondoa manyanga yale kwenye viambaza.&#8221;<br />
Ingawa ni chombo kilichojitokeza hivi karibuni tu katika mapambano ya kandanda, kuna baadhi ya watu wanaohusianisha asili yake na utamaduni wa Kiafrika. “Asili ya vuvuzela inasemekana kuwa ni pembe la mnyama kudu liitwalo ixilongo kwa kiXhosa, mhalamhala kwa kiTshivenda –linapulizwa ili kuwaita wanakijiji kwenye mikutano.<br />
Inaonekana vuvuzela lilianza kutumika mwaka 1992 katika mapambano ya mpira wa miguu huko Afrika Kusini, na wapenzi wa Timu ya AmaZulu. Mashabiki walitengeneza pembe kutokana na makopo yaliyotupwa, kwa furaha ya wengi na kero kwa wengine: Mwandishi wa Afrika Kusini Jon Qwelane aliandika mwaka 2007 kwamba “Siku hizi, kuna kifaa kilichotokea kuzimu, kinachoitwa vuvuzela, ambacho kimepelekea uamuzi wangu wa kuacha kuhudhuria mechi na badala yake kuzianngalia kwenye televisheni, huku sauti ikiwa imeminywa kabisa.”<br />
Katika miaka ya 2000, huku Afrika ya kusini ikiwa imewasilisha maombi ya kuandaa Kombe la Dunia, vuvuzela ilizalishwa kwa wingi kibiashara  kutokana na msaada uliotolewa na SAB Miller (Kiwanda cha kutengeneza Pombe Afrika Kusini) kwa kampuni ya Neil van Schalkwyk ya Masincedane Sport mwaka 2001, iliyoanza kuzalisha kwa wingi toleo nafuu la plastiki. </p></blockquote>
<p>SA Sucks anaipinga “historia” ya vuvuzela kama “<a href="http://www.zasucks.com/?p=3873">uongo wa kijinga unaosambazwa kupitia Wikipedia</a>”:</p>
<blockquote><p>
Kuna uongo wa ajabu unasambazwa kupitia Wikipedia (asante Karooboy kwa kuuonyesha) kwamba asili ya vuvuzela imetokana na “pembe ya Kudu” ambalo lilikuwa likipulizwa na weusi. Ilikuwa karibu nife kwa kucheka kutokana na hadithi hizi za kutunga, pengine ni jambo ambalo tungelitarajia - ukweli kuwa haya madudu maharibifu yaling&#39;oa (tarumbeta za honi) kutoka kwenye magari moshi wakati yakifanya uharibifu wao kwa pamoja ni wazi kuwa kisiasa hautaweza kumezwa kirahisi rahisi (au kukubalika). Chini kidogo katika makala hii kuna picha ya vuvuzela la manjano lenye umbo la pembe - niliipata picha hii kwenye mamia ya barua pepe zinazoingia kutoka kwa watu nisiowajua, zikiniomba eti nikiweke “oda” 10 000 ya majitu haya, yakiwa yamebandikwa nembo yangu ya kibiashara. Umbo la pembe yenyewe liko kiajabu lakini kama ile makala ya Wikipedia, ni dhahiri kuwa makampuni ya PR wanafanya kila linalowezekana kuzika historia ya kweli nyuma ya madude haya.  </p></blockquote>
<p>Kwa mujibu wa SA Sucks<a href="http://www.zasucks.com/?p=3873"> hakuna jambo lolote la dhati la Uafrika kwenye vuvuzela</a>: </p>
<blockquote><p>Moja ya mambo ninayopenda juu ya wanasiasa wanaoendesha himaya hii ni jinsi, kwa namna watakavyoamua, wanaweza kutunga historia wakati wowote.Vuvuzela ni mfano moja wapo.<br />
Wale wanaotetea vuvuzela wanasema kwamba vuvuzela ni sehemu ya utamaduni wa mpira wa miguu Afrika Kusini na kwamba kutokuliruhusu kuatakuwa ni uvunjaji wa haki. takataka. Yamekuwepo kwa miaka chini ya kumi. Ilikuwa mpaka mwanaharamu anayeitwa  “Neil van Schalkwyk, mmiliki mwenza  wa Masincedane Sport, inayozalisha mavuvuzela ya plastiki, aliposhinda Tuzo ya SAB KickSrart ya mwaka 2001, ambayo ni mradi wa kuwasaidia wajasiriamali kwa kutoa misaada na mwongozo katika kuanzisha biashara.” Ndipo vuvuzela lilipoanza <em>kujulikana</em>. </p></blockquote>
<p>Dave Taylor anadhani kuwa sauti ya vuvuzela <a href="http://www.southafricaproject.org/blog/2009/06/should-fifa-ban-the-vuvuzela-from-world-cup-2010/">inakera na kusumbua</a>: </p>
<blockquote><p>Mashabiki nusu-dazeni wakiwa na moja ya madude haya, au hata mashabiki wengi wanapoyapuliza kushangilia goli ama mchezo mzuri wa kulinda goli hilo ni jambo moja, lakini wale tulioangalia Kombe la Mabara la FIFA tumejifunza kuwa, namna ya ushangiliaji nchini Afrika Kusini inaonekana kuwa ni kuendeleza kelele hii moja kwa moja wakati wote wa pambano.<br />
Na hatuzungumzii watu ishirini ama thelathini kwenye uwanja, tunazungumzia mamia, kama sio maelfu ya wenyeji wanaoendeleza hii kelele inapasua masikio wakati wote wa mchezo. </p>
<p>Makelele haya ya moja kwa moja niliyaona kuwa yanakera na kusumbua, na yaliingilia kati uwezo wa kuwasikia watu wakishangilia  kabumbu safi ama kuzomea maamuzi mabaya ya refa. </p></blockquote>
<p><a href="http://languagelog.ldc.upenn.edu/nll/?p=1545">Language Log anasema kwamba</a> &#8220;thamani ya vuvuzela ni sawa na pointi 23 za mchezo wa bao la maandishi hata kabla ya kupewa faida - au pengine ni sawa na hivyo, kama lingeongezwa kwenye orodha rasmi ya maneno.&#8221;</p>
<p>Mark Gleeson wa blogu ya Reuters blog anafikiri kwamba <a href="http://blogs.reuters.com/africanews/2009/06/24/money-will-talk-louder-than-any-vuvuzela/">mwishowe pesa itazungumza zaidi ya vuvuzela lolote</a>. Anasema mabishano kuhusu vuvuzela yamegeuka “sawa tu na mgogoro wa ukoloni mambo-leo”: </p>
<blockquote><p>Kwa vyovyote mjadala kuhusu vuvuzela ingeanzisha kelele kubwa lakini kwa baadhi ya wachambuzi wa mambo wa Afrika Kusini mabishano hayo yamegeuka kuwa sawa na mgogoro wa ukoloni mambo-leo.<br />
Matarumbeta yenye kelele, yanayotawala viwanja vyote wakati wa Kombe la Mabara, yaliwasababishia watu wengi kufunga masikio yao.<br />
Malalamiko kutoka kwa watazamaji wa televisheni Ulaya nzima yamekuwa makali sana kiasi cha kumfanya mdudu huyu wa plastiki kuwa moja ya ajenda kuu katika mikutano ya waandishi wa habari na rais wa FIFA Sepp Blatter ambayo aliifanya wakati wa michuano huko Afrika Kusini. </p>
<p>Mwishoni mwa siku, ni fedha za televisheni ndizo zitakazoongea. Kama watangazaji wakubwa wa matangazo hayo wataihisi kero inayosababishwa na mavuvuzela kiasi cha kuwaondolea raha ya kutazama kwa watazamaji wao, FIFA italazimika kujirudi na kuyasitisha mavuvuzela kwenye viwanja vitakavyotumika kwenye mechi za Kombe la Dunia mwaka 2010. Uamuzi huo hautajali itikadi yoyote bali pesa.</p></blockquote>
<p>Bob wa blogu isiyo rasmi ya DC United <a href="http://dcunitedblog.blogspot.com/2009/06/ot-vuvuzela.html">hawaelewi wale wanaoichukia vuvuzela</a>:</p>
<blockquote><p>Binafsi siwaelewi wanaoichukia vuvuzela. Ninahisi watu wengine hawana uwezo wa kuchuja hizi kelele zinazotoka kwa wapiga kelele walio kwenye majukwaa ya uwanjani wakati wa mechi za  Kombe la Mabara. Yanaitwa mavuvuzela. Ninahitaji moja. </p>
<p>Kuanzia sekunde za mwanzo za pambano la kwanza kabisa la Kombe la Mabara ambalo nililiangalia mwaka huu, New Zealand dhidi ya Hispania, Nilifikiri, “ni kelele gani ile?” na haraka nikaichuja. Na kwa njia sawa na hiyo, wakati nilipoishi Rosslyn, chini ya njia za ndege zilizokuwa zikiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Taifa, kelele za ndege nilinibugushi kwa kiasi cha wiki tu. Baada ya hapo sikuzisikia tena.<br />
Yeyote ambaye amewahi kuhudhuria mechi anajua kwamba hilo huwa tukio la kujua mambo mengi tofauti. Kuna mchezo wenyewe, lakini kuna nyimbo, Mishumaa ya Kirumi, mabomu ya moshi, ngoma, honi. Enhhee, na hata mashabiki walevi vile vile. </p></blockquote>
<p>Baadhi ya wasomaji wake wanapinga. <a href="http://dcunitedblog.blogspot.com/2009/06/ot-vuvuzela.html#c8372890453722267066">Mmoja wao anachukia “dubwana lile”</a> kwa sababu linaharibu mandhari ya mchezo:</p>
<blockquote><p>Mimi ni mmoja wa wanaolichukia, siwezi kumuelewa yeyote ambaye anafurahia kuangalia soka kwenye televisheni ambaye anayapenda (mavuvuzela). Nayachukia madubwana haya. Lakini si kwa sababu yana kelele na yanakera. Ni mambo mengi – naam, watu wengi – wana kelele na wanaudhi, na hata (hasa) kwenye mapambano ya soka. Si kwa sababu wana kele na wanaudhi. Ni kwa sababu wanaharibu kabisa mandhari inayoendeana na pambano. Wanaiharibu.</p></blockquote>
<p>Msomaji mwingine anasema, “<a href="http://dcunitedblog.blogspot.com/2009/06/ot-vuvuzela.html#c3379660743659596991">huu ni wehu</a>”:</p>
<blockquote><p>*U*naweza kuwa na uwezo wa kuisukuma nyuma ya akili yako, lakini kwa wengi wetu, huu ni wehu. Sauti yake *si* ya “kimandhari”, *siyo* sehemu ndogo ya utazamaji, na haezi kukubalika.</p></blockquote>
<p>Setumo anaandika kuhusu <a href="http://www.sportsleader.co.za/setumostone/2009/06/22/on-the-vuvuzela-and-intolerance/">vuvuzela na kutokuvumiliana</a>: </p>
<blockquote><p>Kuweka kumbukumbu sawa, hatupulizi vuvuzela kwa sababu sisi ni Waafrika . Tunapuliza mavuvuzela kwa sababu tunapata mtawanyiko sawia wa homoni za adrenalini kutokana kelele zenye ubunifu zinazotoa. Vilevile, tunapata msisimuko wa adrenalini kwa sababu sisi ni binadamu. Siyo kwa sababu sisi ni Waafrika!<br />
Na kwa vile hivi sasa tumeachana na imani potofu zinazotokana na ubaguzi wa rangi, inaweza kuwa rahisi kuisafisha kelele hii. Hatimaye, tunaweza kukubaliana kwamba hili ni suala la kupenda, kutokupenda na kutokuvumiliana.</p></blockquote>
<p>Mmoja wa wasomaji wa Setumo anatoa hoja kwamba hili (vuvuzela) si jambo la Kiafrika: </p>
<blockquote><p>Kwa hiyo Vuvu ni jambo la Kiafrika?? Kushindwa kwa FIFA 2010 si jambo la Kiafrika…ni suala la kimataifa. Ukweli ni kwamba Afrika Kusini inaandaa tu mashindano haya, na inajitahidi sana kupata wageni wa kimataifa kuja Afrika Kusini mwaka ujao. Kwa hiyo, kuweni na uelewa mdogo kwamba wale wasio Waafrika wanaioona kelele ya vuvuzela kuwa inakera kupita kiasi. Sidhani kuwa nchi nyingi zisizo za Kiafrika zingependa kuwa na ‘Uafrika’ukizingatia mambo kama vurugu, mauaji &#038;  utawala mbaya uliopo katika bara hili taabani. </p></blockquote>
<p>Msomaji mwingine anaipenda sauti ya vuvuzela kiasi kwamba angeweza kununua sauti-mwito wa simu yake!:</p>
<blockquote><p>@mcOlly – Kama mwenyeji wa Texas, ningependa kununua sauti-mwito hiyo ya simu.<br />
Makelele haya dhidi ya vuvuzela ni ya kipuuzi. Kama haivutii kwenye televisheni, basi warusha matangazo washushe sauti za vipaza sauti vilivyoko uwanjani. Nimeijua vuvuzela kwa kuangalia Kombe la Mabara, na hiyo inanifanya nitamani kwenda kutazama Kombe la Dunia zaidi kuliko ilivyokuwa.</p></blockquote>
<p>Shine2010 anadhani mavuvuzela <a href="http://www.shine2010.co.za/goodnews.php?article_id=344">yataifundisha dunia heshima na uvumulivu</a>:</p>
<blockquote><p> …Labda kukutana na maelfu machache ya mavuvuzela yatailazimisha dunia, na soka, kutekeleza kwa hakika baadhi ya fikra za kimaadili –uvumilivu, heshima n.k –ambazo inazihubiri kila wakati. </p></blockquote>
<p>Robyn amekuwa <a href="http://inthefield.blogs.cnn.com/2009/06/29/how-i-became-a-football-trumpet-addict/">‘mlevi’ wa vuvuzela</a>:</p>
<blockquote><p>Kwa mara ya kwanza nilijaribu kulipuliza vuvuzela wiki mbili zilozopita, mwanzoni mwa Kombe la Mabara ambalo lilifanyika Afrika Kusini kabla ya Kombe la Dunia la mwaka ujao. Nilishindwa vibaya. Nilipuliza na kupuliza, hakuna kilichotokea,  vijisauti fulani vidogo tu vilivyotoka. Lakini kwenye mechi kati ya Brazili na Italia, Niliupata ujanja wa vuvuzela na nikaungana haraka na umati katika mlio wa nota moja. Baaaah! Baaaah! Baaaah!<br />
Ni sauti inayoudhi na kukera kiasi kwamba inabidi kutumia ule usemi “kama huwezi kuwashinda, ungana nao.” Kutokulipuliza vuvuzela katika mechi za za soka Afrika Kusini si tu kwamba inakufanya ujisikie kutengwa bali pia inakufanya uichukie kelele ambayo kila mmoja anaipiga. </p></blockquote>
<p>Mwanablogu I Luv SA anacho kipande cha ushauri kwa wale wanaoichukia vuvuzela, <a href="http://iluvsa.blogspot.com/2009/06/bye-bye-vuvuzela.html">“vumilieni”</a>:<br />
Mie, ninawaambia FIFA, mlinunua maneno matamu ya kuandaa mashindano nchini Afrika kusini, inawabidi mle chakula chote ambacho kinajumuisha kiungo kikuu, vuvuzela. Ni sawa na kuwaambia mashabiki wa uingereza kuizima kelele wanayoiita uimbaji. Vumilieni. </p>
<p> “Wakosoaji wanasema yana kelele sana. Sasa iweje,?” <a href="http://safootballfans.blogspot.com/2009/06/great-vuvuzela-debate-should-fifa-ban.html">anaandika Ash</a> kwenye blogu ya Wapenzi wa soka Afrika Kusini:</p>
<blockquote><p>Hilo ndilo lengo la mavuvuzela. Lipo pale ili kutengeneza mandhari yenye kelele. Hii ni Afrika na tunajulikana kwa kucheza na kuimba na kwa kawaida kwa kutengeneza mandhari nzuri katika mechi zetu za mpira wa miguu.<br />
Ni sehemu ya mazoea ya aina yake Afrika Kusini na nina hakika kama wageni wetu watahudhuria michezo hii na kushuhudia hali hii ya hewa (iliyojaa kelele ya mavuvuzela) basi watayapenda.</p>
<p>Kwangu, kuwaambia mashabiki wa nyumbani kuyaacha mavuvuzela yao nyumbani itakuwa kama kuwaomba wapenzi wa Liverpool kuacha kuimba “Katu Hutotembea Peke yako”, au kuwaambia mashabiki wa Brazili kuacha kusakata Samba kwenye mechi zao. </p></blockquote>
<p> “Nini kilichovikumba kucheza na kuimba na mavazi ya sare?.” <a href="http://safootballfans.blogspot.com/2009/06/great-vuvuzela-debate-should-fifa-ban.html?showComment=1245365041794#c644623439046368978">Msomaji mmoja anauliza</a> na kuongeza, “usiruhusu mchango wako kwa dunia uwe ni ule ambao unaudhi!”:</p>
<blockquote><p>Kama huo ndio utamaduni pekee ambao Afrika Kusini inao, basi hali n mbaya sana. Ni nini kilichovifika kucheza na kuimba na uvaaji wa sare? Mambo hayo yanafanya kazi vyema kwenye nchi nyingine Usiruhusu mchango wako kwa dunia uwe ni ule ambao unaudhi! Ni suala la ukarimu pia. Kutupigia kelele masikioni ni ushenzi. Mimi ninazima sauti. Namsikitikia yeyote anayekwenda Afrika Kusini kuangalia michezo. Hawatakuwa na chaguo lolote kuhusu suala hili.</p></blockquote>
<p>Msomaji mwingine analinganisha vuvuzela na <a href="http://safootballfans.blogspot.com/2009/06/great-vuvuzela-debate-should-fifa-ban.html?showComment=1245391850352#c61277141808386838">kelele inayoudhi ya jeshi la nyuki linalozinghuka juu ya kichwa chako…</a>”:</p>
<blockquote><p>Mtazamo anaotoa mwanablogu wa kufananisha nyimbo za Liverpool na mandhari ya samba huko Brazil uko karibu na utaahira. Bila ya shaka ningewataka mashabiki wa Liverpool waache ikiwa wangekuwa wanapiga kelele kwa nota moja tu ya YWNWA kwenye masikio yangu kwa muda wa saa moja na nusu. Kuna tofauti kubwa kati ya kelele inayoudhi ya nyuki wanaozunguka juu ya kichwa chako na ile ya dansi ya samba.</p></blockquote>
<p> “<a href="http://safootballfans.blogspot.com/2009/06/great-vuvuzela-debate-should-fifa-ban.html?showComment=1245395688925#c4991355901611150636">Hautakuwa unatazama timu za nyumbani au wachezaji,</a>” msomaji mwingine anajibu:</p>
<blockquote><p>
Ni kwa jinsi gani Afrika Kusini inaweza kuimbia dunia kuwa yupi ni  mgeni wa mpira wa miguu? Mgeni wa nchi, ndiyo. Mgeni wa mpira wa miguu? Usinifanye nicheke. Hautakuwa mpira wa Afrika kusini mwaka ujao. Utakuwa mpira wa miguu wa dunia nchini Afrika kusini. Hutakuwa unaangalia timu za nyumbani au wachezaji.</p></blockquote>
<p>Anders anatuambia kuwa <a href="http://www.runofplay.com/2009/06/17/notes-from-south-africa-the-forbidden-vuvuzela/">wanaochukia vuvuzela ni wale watu ambao wanaangalia michezo kwenye televisheni</a>:</p>
<blockquote><p>
Malalamiko juu ya vuvuzela yatoka kwa wale, kama huyu rafiki yangu, wanaoangalia mashindano kutokea ng’ambo. Kwenye viwanja, mashabiki wanayapenda. Ni moja ya yale mambo ambayo unayachukia mpaka pale utakapokuwa na uwezo wa kuyajaribu; fikiria tochi ya miale. Kwenye televisheni matarumbeta yanaingiliana na utangazaji, pamoja na mambo mengine, lakini uwanjani hali ya kelele ni sehemu ya mandhari. Bila ya shaka hayakwaruzi ukiwa nayo ana kwa ana kama vile ukiyasikia kwa kupitia setilaiti.</p></blockquote>
<p><a href="http://troyounce.blogspot.com/2009/06/vuvuzela-war-nosiest-worldcup-ever.html">Vita halisi ya vuvuzela</a>, tunaambiwa haiko kwenye Mtandao bali nchini Uholanzi:</p>
<blockquote><p>Kuna tishio la vita ya mavuvuzela huko Uholanzi. Kampuni ya SoccerID iliarifu siku ya Jumatatu kuwa itaingiza Ulaya mapembe haya yaliyosababishwa utata huko Afrika Kusini. Ndani ya  majuma matatu ama manne mavuvuzela ya awali yatauzwa Uswisi. Kampuni ya NoLimitation, inadai kuwa ina haki pekee ya kusambaza mavuvuzela hayo.  </p>
<p>Kampuni ya NoLimitation BV ilipata haki pekee ya mavuvuzela na ya kutumia jina hilo kupitia  kampuni ya Kijerumani ya Kehrberg GmbH, inayodai kuwa na haki katika nchi zote za Umoja wa Ulaya. Kwa mujibu wa NoLimitation, hii ina maana kwamba wao ndio kampuni pekee nchini Uholanzi yenye haki ya kuuza tarumbeta hizi zenye vijipembe vitatu kwa jina la vuvuzela. </p></blockquote>
<p>Chris wa blogu ya World Cup <a href="http://www.worldcupblog.org/world-football/death-to-the-vuvuzela.html">anaafiki kwamba vuvuzela “ina asili ya Afrika kusini”</a> bali…</p>
<blockquote><p>Tatizo ni kuwa, ina asili ya maudhi. Kama uliangalia japo sekunde 30 za Kombe la Mabara, uliweza kusikia ile kelele iwayo yote – na inawezekana kuwa matarumbeta yale yalikuwa ndiyo sababu iliyokufanya utazame kwa sekunde 30 tu.<br />
Ni kelele moja endelevu kwa dakika 90. mpaka inafikia unaanza kujiuliza ni muda gani ambapo filamu hii ya kutisha ya dalaja la B itakapovunjika mbele ya macho yako. Binafsi nimeanza kuangalia mapambano hayo huku nimezima sauti –mchanganyiko wa timu ya utangazaji wa ESPN na vuvuzela vina uwezo wa kutumika kama sindano m’badala ya sumu au kitu kama hicho.</p></blockquote>
<p>Phobian anashauri kwamba <a href="http://phobian.blat.co.za/2009/06/21/the-vuvuzela-debate/">mavuvuzela yaruhusiwe tu Afrika Kusini inapocheza</a>:</p>
<blockquote><p>Kombe la Dunia ni la kila mmoja, si  kwa wapuliza mavuvuzela peke yao. Labda yaruhusiwe tu pale Afrika Kusini inapocheza. Timu nyingine zinapocheza ziwe na sauti ya kuamua ikiwa wako tayari mavuvuzela yatumiwe ama yasitumiwe kwenye mechi zao.</p></blockquote>
<p>SA Sucks anayapeleka mbali zaidi mabishano ya vuvuzela kwenye uwanja mwingine kabisa akitoa hoja kwamba mbali na uwezekano wa kuharibu masikio ya mtu, c<a href="http://www.zasucks.com/?p=3873">hombo hiki kinaweza kusambaza VVU/UKIMWI! </a></p>
<p>SA Sucks anaandika, “Ni wazi, Sipho hulisafisha vuvuzela kwa kulipekecha kila upande, huku akisambaza mate yenye virusi vya UKIMWI/TB (&#038; na Mungu anajua ni magonjwa gani mengine) kwa watu wengine walio nyuma, mbele na pembeni yake.”: </p>
<blockquote><p>
Madaktari wataalamu wanaonya kwamba kelele za vuvuzela zinaweza kuharibu kabisa uwezo wa mtu kusikia, lakini hiyo haijazingatia hatari ya kuambukiza UKIMWI ya hili dude.<br />
Tangu mechi za Kombe la Mabara, watazamaji walilipuliwa kutokea pande zote za uwanja na kelele zenye-kutikisa dunia za vuvuzela.Zaidi ya madhara ya kiafya ya masikio na maumivu ya kichwa, bidhaa nyingine itokanayo na upulizaji wa kifaa hiki ni mkusanyiko mkubwa wa mate. Ni wazi, Sipho hulisafisha vuvuzela kwa kulipekecha kila upande, huku akisambaza mate yenye virusi vya UKIMWI/TB (&#038; na Mungu anajua ni magonjwa gani mengine) kwa watu wengine walio nyuma, mbele na pembeni yake. </p></blockquote>
<p>Vuvuzela ni alama ya kila jambo lililoharibika katika “<a href="http://www.zasucks.com/?p=3873">Afrika chini ya jangwa la Sahara the “Sahara Sub Saharan Africoon</a>”:</p>
<blockquote><p>
Binafsi, ninalipenda (vuvuzela)! Kama kuna chochote kinaweza kuliangusha Kombe la Dunia la 2010, na kuwa ushahidi wa kila kisichofaa katika Afrika Nyeusi (Kusini mwa Jangwa la Sahara), yatakuwa haya mavuvuzela. Hebu fikiri namna uchafu unaokinaisha, ufukara uliokithiri, tabia za fujo za kinyani nyani na kele zilizokithiri zinazoletwa na hili dude; yote yatasafirishwa mpaka kwenye nyumba milioni 500 za Wazungu wa magharibi, huku dunia nzima ikishuhudia. </p></blockquote>
<p>SA Sucks anawaonya wahudhuriaji wa Kombe la Dunia kujiandaa kwa “ubatizo wa moto” wa historia ya mwanadamu.” <a href="http://www.zasucks.com/?p=3873">Mwanablogu huyu alishuhudia mwenyewe</a> “masaa matatu ya kuzimu hapa hapa duniani”: </p>
<blockquote><p>Jumapili nilijikuta kwenye masaa matatu ya kuzimu hapa hapa duniani. Nikaapa, pale pale, baada ya jioni ile ya kwanza (na ya pekee) ya kujionea mwenyewe soka la Afrika Kusini linavyokuwa kwamba, sitajiruhusu kujikuta mahala pale tena. Yapo mengi yaliyonikwaza na kuniudhi jioni ile, lakini hakuna kililonikera kama Vuvuzela. </p></blockquote>
<p> “Kama FIFA wangeyapiga marufuku mavuvuzela basi na waifute sera ya mzunguko wa Kombe la Dunia kuyaandaa mshindano hayo Ulaya kila mwaka katika muda ambao unawafaa watu wa Ulaya na hali ya hewa ya Kiulaya katika viwanja,” <a href="http://visualguidanceltd.blogspot.com/2009/06/vuvuzela-horn-of-africa-which-almost.html">anaandika Visual Guidance</a>: </p>
<blockquote><p>Ni lazima kiwepo kitu cha kulalamikia. Hakuna malalamiko kutoka kwa watu waliopo kwenye viwanja. Wanaipenda vuvuzela. Tatizo ni wazembe wanaoketi kwenye sofa maelfu ya maili mbali na viwanja, wanaojilaza kivivu vivu mbele ya televisheni zao na kulalamika kuwa kelele (za mavuvuzela) zinawapa maumivu ya kichwa. Boo hoo. Nijibuni –hivi matarumbeta yanakera zaidi ya Wana-Ultra na vipaza-sauti vyao katika viwanja vyao vya nyumbani kwenye ghuba yote Ultra au bendi ya Uingereza ikipiga wimbo wa ‘Great Escape’ pale Wembley?<br />
Mashindano haya yanafanyikia Afrika. Hivi ndivyo wanavyofanya kwenye mechi za mpira nchini kwao, ndio utamaduni wao wa mpira.<br />
Kama FIFA watayapiga marufuku mavuvuzela basi na waifute sera ya mzunguko wa Kombe la Dunia kuyaandaa mshindano hayo Ulaya kila mwaka katika muda ambao unawafaa watu wa Ulaya na hali ya hewa ya Kiulaya katika viwanja.</p></blockquote>
<p>Garreth anaziona kelele za vuvuzela zinakera na mbaya lakini anafikiri kwamba <a href="http://www.worldcupbuzz.com/buzzing-about-vuvuzelas/">jamii ya mpira duniani inahitaji kufahamu tamaduni mpya za mpira</a>:  </p>
<blockquote><p>Hata kama sauti ni mbaya napelekea kukubaliana na SAFA (Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika Kusini) katika hili. Pamoja na kwamba Kombe la Dunia linahusu mpira, vile vile kombe hilo linahusu jamii ya mpira wa dunia na kuzijua tamaduni mpya za mpira. Kama ninaanza kuonekana kama mtu wa siasa-za-ruksa, samahani sana, lakini hivyo ndivyo ninavyooona.</p></blockquote>
<p>Sauti ya vuvuzela <a href="http://southernafrica.wordpress.com/2009/06/19/vuvuzela-trumpets/">inaudhi na ndiyo maana kuta za Yeriko zilianguka!</a>:</p>
<p>Sauti hii inaudhi! Ndio maana kuta za Yericho zilianguka! Watu wa Yeriko walijiangushia kuta wenyewe ili kuzikimbia zile kelele! Kifo kikawa chaguo lao sawia. Sasa, vivyo hivyo kwa mashabiki wa Afrika Kusini, WOTE NI MAPAFU! Je. hawajagundua kelele wanazosababisha? Hakuna atakayenunua tiketi ili eti jamaa ampigie kelele za vuvuzela mechi nzima!  </p>
<p>Mwanablogu wa Cape Town Daily Photo <a href="http://www.capetowndailyphoto.com/blog/2009/06/football-world-cup-logistics-organisation-and-the-vuvuzela/">hafikiri kama sauti hiyo ilikuwa ni mbaya kiasi hicho</a>: </p>
<blockquote><p>Sijawahi kuwa shabiki wa mavuvuzela (Tarumbeta la plastiki ambalo mashabiki wa Afrika Kusini hupuliza wakati wa mechi za mpira wa miguu) , lakini nikiwa mkweli, haikuwa mbaya sana. Haikuwa na sauti kubwa sana na ni lazima niseme mavuvuzela yaliongeza utamu wa mechi kwa kiasi kikubwa. Ni sehemu ya utamaduni wa soka la Afrika Kusini na haitakuwa kawaida yasipokuwepo.</p></blockquote>
<p><a href="http://www.capetowndailyphoto.com/blog/2009/06/football-world-cup-logistics-organisation-and-the-vuvuzela/"><br />
Unajiandaa kwa Kombe la Dunia 2010?</a>:</p>
<blockquote><p>Nunua viziba masikio kutoka kwenye duka la muziki –utaweza kufurahia mandhari, hata kama patakuwa na vuvuzela linalopigwa pembeni ya sikio lako. </p></blockquote>
<p>Kama wewe ni shabiki wa mavuvuzela, unaweza kutembelea <a href="http://www.blowme.co.za/">tovuti ya Blow Me</a> na uipulize vuvuzela.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/07/afrika-kusini-kuvuvuzela-au-kutovuvuzela/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika ya Kusini: ANC Yafanya Mjadala wa Uchaguzi Kwa Kutumia huduma ya Twita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/afrika-ya-kusini-anc-yafanya-mjadala-wa-uchaguzi-kwa-kutumia-huduma-ya-twita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/afrika-ya-kusini-anc-yafanya-mjadala-wa-uchaguzi-kwa-kutumia-huduma-ya-twita/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 22 Apr 2009 15:06:34 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=134</guid>
		<description><![CDATA[Vyama vya siasa nchini Afrika ya kusini vimo katika hatua za mwisho za kampeni ya uchaguzi ujao. Chama tawala cha ANC (African National Congress) kilifanya mjadala kwa kutumia huduma ya twita.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ismail-dhorat/">Ismail Dhorat</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/04/17/south-africa-anc-hosts-debate-on-twitter-for-upcoming-elections/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Vyama vya siasa nchini Afrika ya kusini vimo katika hatua za mwisho za kampeni ya uchaguzi ujao. Chama tawala cha <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/African_National_Congress">ANC</a> (African National Congress) kilifanya mjadala kwa kutumia huduma ya <a href="http://www.twitter.com/">twita</a>.</p>
<p>Vyama vya siasa vimeanza kutumia mitandao ya kijamii kwenye intaneti ili kufikisha ujumbe. Chama kikubwa ambacho kimekuwa kikitumia huduma hizo ni chama cha <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Democratic_Alliance_(South_Africa)">DA</a> (Democtratic Alliance) ambacho kampeni yake imetiwa moyo na kampeni ya mwaka jana ya Obama.</p>
<p>Chama cha DA kinaendesha kampeni ya kujitangaza kwenye mitandao ya kijamii pamoja na akaunti kadhaa za twita kama ile ya meya wa mji wa Cape Town na mkuu wa chama cha DA, <a href="http://twitter.com/helenzille">Helen Zille</a>.</p>
<p>Tarehe 17-04-2009 chama cha ANC kilitangaza akaunti yake mpya ya twita &#8220;<a href="http://twitter.com/anc_debate">ANC_DEBATE </a>&#8221; ambayo itakuwa ikiendesha mijadala ya moja kwa moja huku <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Jessie_Duarte">Jessie Duarte</a>, mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi na msemaji wa sasa wa chama cha ANC akijibu maswali.</p>
<p>Baada ya kutangazwa kulizuka majadiliano kuhusu umuhimu (wa akaunti hiyo). Mtumiaji wa huduma ya twita wa Kiafrika ya Kusini <a href="http://twitter.com/woganmay">@ woganmay</a> alitengeneza <a href="http://twittersa.com/anc_debate">kurasa maalum </a>kwenye tovuti ya twittersa ili kukusanya maoni. Maoni kadhaa katika mjadala huo yalikuwa hasi na chama cha ANC kililaumiwa.</p>
<p>Kwa mfano, Jason <a href="http://twitter.com/jasonzoopy/status/1540793789">alihisi</a> kuwa jitihada hizi zimechelewa na muda umekwisha.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/04/picture-72.png" title="picture-72.png" class="aligncenter" width="500" height="73" /></p>
<p>Wakati <a href="http://twitter.com/naeem_coza/status/1540731542">Naeem</a> alihisi kwamba idadi ya Waafrika kusini wanaotumia huduma ya twita ni ndogo sana.</p>
<p><img alt="" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/04/picture-41.png" title="picture-41.png" class="alignnone" width="484" height="72" /></p>
<p>Tovuti ya ANC_Debate ilifikiwa na mafuriko ya maswali na ufuatao ni muhtasari wa baadhi ya majibu.</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/saulkza">@Saulkza</a>: tuongelee uchumi: Mtafanya nini kuzuia kudhoofika kwa uchumi? Vipi kuhusu ukosefu wa ajira?</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1540982756">@ANC_debate:</a> Uwekezaji kabambe kwenye miundombinu utachangamsha shughuli za kiuchumi, huduma za jamii ni uti wa mgongo wa sekta muhimu.</p>
<p><a href="http://twitter.com/nikzaz">@nikzaz:</a> mtafanya nini kuhusu uhalifu nchini Afrika ya Kusini?</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541003840">@ANC_debate:</a> tutakarabati mfumo wa sheria za uhalifu - uratibu bora, tutatengeneza miundo ya kisasa na tutaongeza rasilimali. Tutaiandaa jamii na kukabili vyanzo (vya uhalifu).</p>
<p><a href="http://twitter.com/shaynekrige">@shaynekrige:</a>Kwa maoni yako ni kosa gani kubwa ambalo ANC imelifanya katika miaka 15 iliyopita?</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541119792">@ANC_debate:</a> Siyo kosa kubwa, bali kutotilia mkazo iapasavyo kwenye kushirikisha wananchi serikalini na katika maamuzi yanayowahusu.</p></blockquote>
<p>Oni hili, linazua swali: Je tutauona ukarabati katika ANC ya leo, njia mpya za kuushirikisha umma kwenye maamuzi ya serikali? Labda serikali ya kidijitali 2.0?</p>
<p>Pia walijibu maswali yanayohusu hofu za uchujwaji wa habari </p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/jasdonwar">@jasdonwar:</a> je unalo lolote la kusema dhidi ya madai kwamba vyombo vya habari vya Afrika ya Kusini vitapunguzwa baada ya uchaguzi?</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541151039">@ANC_debate:</a> hiyo ni mbinu ya kujazana hofu. Chama cha ANC kilipigania uhuru wa vyombo vya habari na hakuna lolote linaloashiria kuwa tutapuuza (msimamo huo)</p></blockquote>
<p>Kuhusu swala la kuchuja michoro ya kuchekesha (vikatuni) vyenye mandhari ya kebehi</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/JeremyTNell">@JeremyTNel:</a> Je unaamini kuwa michoro ya kuchekesha ina utovu wa heshima? Je chama cha ANC kingependa kudhibiti michoro hiyo?</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541132368">@ANC_debate:</a> Wachoraji wa vikatuni wanapaswa kuwa si waoga. Sanaa ya michoro ya kuchekesha (vikatuni) yenye mandhari ya kusanifu ni sanaa muhimu. Lakini wanapaswa kufuata maadili kama wana habari wengine.</p></blockquote>
<p>Kuhusu masuala ya (nishati) endelevu</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/flintza">@flintza:</a> Je mnakidhi vipi mahitaji ya nishati ya Afrika ya kusini huku mkiwa mnadhibiti nyayo za gesi ya ukaa. Inavyoonekana mnamakinikia makaa ya mawe (hamna uwezo wa kuona mbali)</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541104324">@ANC_debate:</a> Afrika ya kusini inapaswa kusogea mbali na nishati ya makaa ya mawe lakini bado ni moja ya vyanzo vikuu vya nishati katika upeo ulipo mbele yetu. Nishati hiyo inaongeza uwezo wa kuwekeza kwenye nishati nyuklia, jua na upepo.</p></blockquote>
<p>Kuhusu suala la mgombea kiti cha urais Jacob Zuma kuwa kizimbani kwa tuhuma za rushwa</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541125094">@ANC_debate:</a> kila mtu ana haki sawa mbele ya sheria na ana haki ya kudhaniwa kuwa hajakosa. Chama cha ANC kinasema sheria lazima ichukue mkondo wake &#038; mkondo huo ni kwa ajili ya Zuma na mtu mwingine yeyote.</p></blockquote>
<p>Kuhusu mikakati ya kuzuia UKIMWI</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541157270">@ANC_Debate:</a> Tunatilia maanani kuzuia maambukizi, kuhamasisha matumizi ya kondomu na tabia njema. Usambazaji wa dawa za ART ili ziwafikie wote wanaozihitaji. Tutaimarisha ushirikiano na jamii yote</p>
<p><a href="http://twitter.com/irenebarnard">@irenebarnard:</a> je ni kwa jinsi gani mtawapasha habari wananchi kuhusu maendeleo  ya &#8220;kampeni yenu ngangari ya kuzuia Virusi Vya Ukimwi&#8221;</p>
<p><a href="http://twitter.com/ANC_Debate/status/1541183801">@ANC_debate:</a> Watu wanatakiwa kushirikishwa katika utekelezaji kwa kupitia zahanati, mashirika yasiyo ya kiserikali, taarifa za serikali na vyombo vya habari.</p></blockquote>
<p>Ili kusoma zaidi juu ya mjadala huu, tembelea tovuti ya <a href="http://www.capetownalive.co.za/blogs/2922-anc-debates-on-twitter-and-answers-to-the-public-jesse-duarte-on-elections-2009.html">Capetownalive</a> ambayo ina muhtasari wa baadhi ya maswali.</p>
<p>Baadhi ya watumiaji wameripoti kuwa walizuiwa kushiriki au pengine walidharauliwa na Jessie aliwajibu kuwa hakuna mtumiaji ambaye alizuiwa, hata hivyo walikiri kuwa si maswali yote ambayo yalijibiwa. Kuna mipango ya kufanya wasaa huu wa maswali na majibu kuwa wa mara kwa mara kwa sababu imetangazwa kwamba ijumaa ijayo patakuwa na wasaa mwingine.</p>
<p>Niliandika <a href="http://ismaild.com/anc-hosts-election-debate-twitter/">katika blogu yangu </a>kuwa japokuwa mjadala huu umekuja katika ngwe za mwisho na unashirikisha watumiaji wa huduma ya twita pekee, hii ni hatua kubwa yenye mwelekeo mzuri kwa chama cha ANC kwani kinawapa wananchi fursa ya kujadiliana nao moja kwa moja. Kama mpango huu utasambazwa nchini kote na kuruhusu watu wenye simu za mkononi kutuma maswali yao na kupokea majibu kutoka kwa wagombea, hatua hiyo itakuwa yenye manufaa sana katika kuwashirikisha Waafrika ya Kusini wote.   </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/04/afrika-ya-kusini-anc-yafanya-mjadala-wa-uchaguzi-kwa-kutumia-huduma-ya-twita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Blogu za Afrika Zapendekezwa Kupokea Tuzo ya Bloggies 2009</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/blogu-za-afrika-zapendekezwa-kupokea-tuzo-ya-bloggies-2009/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/blogu-za-afrika-zapendekezwa-kupokea-tuzo-ya-bloggies-2009/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 26 Jan 2009 11:57:01 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Blogger News]]></category>
		<category><![CDATA[Cote d'Ivoire]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[Liberia]]></category>
		<category><![CDATA[Media]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Uganda]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=50</guid>
		<description><![CDATA[Blogu zilizopendekezwa kwa ajili ya Tuzo ya Tisa ya Zawadi za Weblog: Mapendekezo ya blogu katika mashindano ya Bloggies ya 2009 yalifunguliwa tarehe 1 Januari na kufungwa tarehe 19 Januari. Kwa mujibu  wa waandalizi, mashindano hayo ya Bloggies ni mashindano ambayo yamedumu kwa muda mrefu zaidi mtandaoni, na mapendekezo pamoja na uchaguaji wa washindani katika fainali, ni juu ya msomaji wa blogu. Mshindi hupata senti 2,009 za Marekani! Je, ni mabloga gani wa Kiafrika waliopendekezwa kwa ajili ya kinyang'anyiro cha blogu bora zaidi?]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/ndesanjo-macha/">Ndesanjo Macha</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/01/23/african-blogs-nominated-for-the-2009-bloggies/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Blogu zilizopendekezwa kwa ajili ya Mashindano ya Tisa ya Zawadi za Weblog: <a href="http://2009.bloggies.com/">Mapendekezo ya blogu katika mashindano ya Bloggies ya 2009</a> yalifunguliwa tarehe 1 Januari na kufungwa tarehe 19 Januari. Kwa mujibu wa <a href="http://2009.bloggies.com/">tovuti ya waandalizi</a>, mashindano hayo ya Bloggies ni mashindano ambayo yamedumu kwa muda mrefu zaidi mtandaoni, na mapendekezo, pamoja na uchaguaji wa washindani katika fainali, ni juu ya msomaji wa blogu. Mshindi hupata senti 2,009 za Marekani!</p>
<p>Blogu tano zimependekezwa katika kinyang&#39;anyiro cha blogu Bora Zaidi:<br />
Blogu ya <a href="http://beingbrazen.blogspot.com/"><strong>Being Brazen</strong></a>: Hii ni blogu iliyoko Afrika ya Kusini. Wasifu wa mwanablogu huyo <a href="http://www.blogger.com/profile/05238202392512794465">unaelezwa</a>:</p>
<blockquote><p>Sitabiriki, huota ndoto za mchana, umri wangu ni katika miaka ya 20, ninaamini katika mapenzi, Mungu na nguvu ya maneno, nina mawazo huru na pengine kucheka ndio dawa bora kuliko zote. Sipendi kuruka angani [kupanda ndege], sehemu zenye watu wengi, kupanga foleni, kadhalika sipendi wadudu. Hujikwaa nikavaa viatu virefu. Ninaandika ili kuepuka wehu.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <a href="http://appfrica.net/blog/"><strong>AppAfrica</strong></a>: Hii ni tovuti ya habari mpya mpya zinazohusu ubunifu wa Kiafrika, elimu na ujasiriamali kwenye teknolojia:</p>
<p>Blogu ya <a href="http://www.gladtobeagirl.co.za/"><strong>Glad To Be A Girl</strong></a>: Ni mwanablogu wa Kiafrika ya Kusini anayekaa mjini Johannesburg.  </p>
<p><a href="http://www.blogger.com/profile/16618315315456011985">Wasifu wake</a>:</p>
<blockquote><p>Huchambua wehu wangu na hujisifu kwa akili zangu! Unyonge [kutopenda makuu] unanichirizika ndoo kwa ndoo :) kejeli ndiyo silaha yangu ninayoipenda. Wakristu, Waislamu &#038; Wayahudi wanaamini katika Mungu mmoja zaidi ya yule ninayemuamini.</p></blockquote>
<p>Blogu ya <a href="http://nofoodforlazyman.blogspot.com/"><strong>West Africa Wins Always</strong></a>: <a href="http://www.blogger.com/profile/07378753725707688050">Hii ni blogu ya mwanablogu Pauline</a>, mwanahabari ambaye amekuwa akiishi nchini Ivory Coast tangu mwaka 2003. </p>
<p>Na blogu ya mwisho ni ile ya <a href="http://ugandascarlettlion.blogspot.com/"><strong>Scarlett Lion</strong>: Yeye ni mwanahabari aliyeko nchini Liberia. </p>
<p><a href="http://www.blogger.com/profile/02190972002862387574">Kwa mujibu wa maneno yake mwenyewe</a>:</p>
<blockquote><p>Mpiga picha, mwandishi, ripota. Napita maishani nikiwa na jicho linalolenga kutengeneza historia na kuiorodhesha. Awali katika nchi ya Uganda na sasa katika Liberia. Blogu hii inakuletea udadisi na maoni. Pamoja na picha.</p></blockquote>
<p>Upigaji kura utafungwa tarehe 2 Februari na washindi watatangazwa mwezi Machi mjini Austin, Texas, huko Marekani katika Tamasha la South by South West Interactive.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/01/blogu-za-afrika-zapendekezwa-kupokea-tuzo-ya-bloggies-2009/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika ya Kusini: Matumizi ya Simu za Viganjani Kupambana na UKIMWI</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/afrika-ya-kusini-matumizi-ya-simu-za-viganjani-kupambana-na-ukimwi/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/afrika-ya-kusini-matumizi-ya-simu-za-viganjani-kupambana-na-ukimwi/#comments</comments>
		<pubDate>Tue, 04 Nov 2008 13:38:33 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Internet & Telecoms]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Technology]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=36</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naJuhie Bhatia  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Afrika ya Kusini imegundua silaha mpya katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI - simu za viganjani. Kwenye mchakato mpya, jumbe za maandishi zitakuwa zikitumwa kila siku kuwahamasisha Wa-Afrika ya Kusini kwenda kupimwa na kutibiwa ugonjwa huo.
Mradi huo, unaoitwa Mradi wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/">Juhie Bhatia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/11/02/south-africa-using-cell-phones-to-combat-aids/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/11/340305918_6413d10fcc_m.jpg' alt='' class='alignright' />Afrika ya Kusini imegundua silaha mpya katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI - simu za viganjani. Kwenye mchakato mpya, jumbe za maandishi zitakuwa zikitumwa kila siku kuwahamasisha Wa-Afrika ya Kusini kwenda kupimwa na kutibiwa ugonjwa huo.</p>
<p>Mradi huo, unaoitwa Mradi wa Masiluleke au Project M, <a href="http://www.poptech.org/blog/index.php/2008/10/24/project-masiluleke-tackling-hiv-with-technology/">ulitangazwa rasmi</a> wiki iliyopita wakati wa kongamano la <a href="http://www.poptech.org/conferences/">Pop!Tech 2008 </a>huko Maine, Marekani. Mradi huo umerahisishwa na mteremko unaotokana na umaarufu wa simu za viganjani nchini Afrika ya Kusini, na unatumia simu hizo za viganjani kupambana na idadi kubwa ya VVU na kifua kikuu (TB). Sehemu ya kwanza ya mradi huo itatuma takriban jumbe za bure zipatazo milioni moja kwa umma wa kawaida kila siku kwa mwaka mmoja, wakiuasa umma kwenda kwenye vituo vya VVU na kifua kikuu. Jumbe hizo zitatumwa kama sehemu ya jumbe zinazoitwa &#8220;Tafadhali Nipigie Simu&#8221;, ambayo ni aina ya ujumbe unaotumiwa sana katika Afrika.</p>
<p><em>White African </em><a href="http://whiteafrican.com/2008/10/24/frontlinesms-clay-shirky-and-project-masiluleke/">anafafanua</a> mradi huo pamoja na teknolojia yake:</p>
<blockquote><p>&#8220;Gustav Praekelt - mmoja wa wataalamu wa simu za viganjani wenye ufahamu mkubwa - anasaidia kuendesha programu hiyo. Mradi huo unafanywa kwa kutumia nafasi ya bure ya herufi au alama 120 katika mfumo wa jumbe za &#8220;Tafadhali Nipigie Simu&#8221; unaotumika huko Afrika ya Kusini, wanaweka jumbe zitakazowafanya watu waende kutibiwa VVU kwa faragha, hivyo kutohofu doa au aibu inayoambatana na matibabu hayo.  </p></blockquote>
<p>Doa au aibu, pamoja na taarifa potofu, <a href="http://www.poptech.org/project_m_the_challenge/">vinaaminika</a> kuwa ndiyo sababu kuu zinazosababisha Wa-Afrika ya Kusini wachache mno kujitokeza kutibiwa VVU. Japokuwa <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">takriban watu wapatao milioni 5.7</a> nchini Afrika ya Kusini wanaishi na VVU, kwa mujibu wa waandalizi wa mradi huo ni <a href="http://www.poptech.org/blog/index.php/2008/10/24/project-masiluleke-tackling-hiv-with-technology/">asilimia 5 tu </a>ya watu wamepimwa virusi hivyo. Afrika ya Kusini pia ina <a href="http://www.who.int/tb/publications/global_report/2008/key_points/en/index.html">idadi kubwa ya kesi za Kifua Kikuu</a>, ugonjwa ambao unaua wengi wenye VVU.</p>
<p>Mradi M umeundwa ili kusaidia kupambana na magonjwa hayo mawili. Ulichipuka kutoka kwenye programu ya <a href="http://www.poptech.org/accelerator/">Pop!Tech Accelerator </a>na umewakusanya pamoja <a href="http://www.poptech.org/project_m_partners/">wadau wa kimataifa</a>, wakiwemo iTech, the Praekelt Foundation, frog design, Nokia Siemens Networks na the National Geographic Society. <em>3 Sheep </em><a href="http://www.3sheep.co.uk/2008/10/25/south-africa-texting-health-care/">anaeleza</a> kwamba utumiaji wa simu za viganjani unaofanywa na mradi huu unaonyesha ni jinsi gani simu hizo zimejikita katika utamaduni wa Afrika ya Kusini, na anaongeza:</p>
<blockquote><p>&#8220;Nchi nyingi hazina miundombinu inayotumia mtandao wa waya na zinaangalia mitandao ya simu za viganjani kama njia ya mawasiliano… huko nyuma njia nyingine za mawasiliano kama vile redio, zingetumika kufanya kazi kama hii lakini mradi huu wa Afrika ya Kusini unaonyesha umuhimu wa kuziangalia njia zote ili kuufikia umma.&#8221;</p></blockquote>
<p>Japo huu <a href="http://mobileactive.org/cell-life-update-using-mobiles-fight-hiv-aids">sio mradi wa kwanza wa aina hii </a>huko Afrika ya Kusini, waandaaji <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/technology/7688268.stm">wanasema</a> haya ni matumizi makubwa zaidi ya simu za viganjani yaliyowahi kujaribiwa ili kutuma taarifa za afya. Na mpaka sasa mradi huo una matumaini makubwa. Majaribio ya kwanza ya kampeni hii inayotumia ujumbe wa simu za viganjani ulisaidia kuongeza wastani <a href="http://www.poptech.org/project_m_the_solution/">mara tatu zaidi </a>ya watu wanaopiga simu kwenye huduma ya simu ya UKIMWI mjini Johannersburg. Kama mradi utafaulu baada ya kuzinduliwa, kunamatumaini kwamba mradi huu utaweza kusambazwa sehemu nyingine Afrika.</p>
<p>Akitoa maoni katika ujumbe uliotumwa kwenye <em>African Globalization</em>, ahellgeth, <a href="http://africanglobalization.blogspot.com/2008/10/texts-tackle-hiv-in-south-africa.html">anaamini</a> kwamba mradi huu una matumaini makubwa.</p>
<blockquote><p>&#8220;Utumiaji wa teknolojia ni njia nzuri ya kufikisha ujumbe wenye nguvu kwa umma. Utrumiaji wa ujumbe wa simu za viganjani unatoa fursa kwa watu kuusoma ujumbe mara kwa mara, ikilinganishwa kuangalia ujumbe kwenye matangazo ya biashara au mara moja tu kwenye vipeperushi. Ujumbe kwenye simu za viganjani hukaa kwenye simu kwa siku kadhaa, hii inamruhusu mtumiaji kurejea na kuangalia ujumbe huo. Nadhani ujumbe utawafikia watu na kunasa na utawahamasisha kuchukua hatua… jumbe hizi ni sawa na matangazo kwa ya wazi kwa umma kwa kutumia simu za viganjani.&#8221;</p></blockquote>
<p>Akiblogu katika <em>Design in Africa</em>, Dave <a href="http://designinafrica.posterous.com/project-masiluleke">anaafiki</a> kwamba mradi huu una uwezekano wa kufanikiwa:</p>
<blockquote><p>Ni suala muhimu linalotatuliwa, ufumbuzi rahisi na unaoeleweka umebuniwa kwa kujumuisha hazina au nguvu za wadau, na kuna manufaa yanayopimika kwa watu na jamii na gharama za kupokea ujumbe bure. Safi sana! </p></blockquote>
<p>Akiblogu katika <em>Wise Advice</em>, lablady, anaona ni jambo linalosumbua kidogo kwamba teknolojia imwekwa kwenye ulingo mkuu katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI. <a href="http://wiseadvice.wordpress.com/2008/10/27/puzzling-aids-news-item/">Anasema</a>: </p>
<blockquote><p>&#8220;Katika nukta au wakati gani ambapo jamii imefanya chaguo hili kuwa rahisi, na lenye uwazi na mvuto kwa watu masikini waliobanwa na janga la VVU, kwenda kununua simu za viganjani badala ya kondomu? Naliona hili ni jambo lililo kinyume, kwamba teknolojia sasa imekuwa ni chombo kinachoanzisha kampeni ambayo katika wakati mwingine, ingekuwa ni kampeni ya umma kwenye ngazi za chini kwenda kupima damu na kuelimishwa zaidi. Je dharau kwa upande wangu kuhoji kwa nini umma mzima umiliki simu za mkononi kabla ya kunufaika na mkakati wa kinga ya afya kupingana na ugonjwa unaoweza kuzuilika?&#8221; </p></blockquote>
<p>Naye Catherine Forsythe, akiblogu kwenye <em>DogReader</em>, <a href="http://www.lockergnome.com/forsythe/2008/10/24/health-text-messages/">anaongeza</a> kwamba jumbe hizi hatimaye zitaweza kuchukuliwa kama &#8220;jumbe za kero&#8221; za afya.</p>
<blockquote><p>&#8220;Swali linaweza kuwa &#8216;ni kwa muda gani mbinu hii inaeweza kufanya kazi?&#39; Baada ya kusoma kwa mara ya kwanza, jumbe hizi za afya kwa umma zinaweza kufutwa mara moja kama vile zinavyofutwa jumbe nyingine za kero.&#8221;</p></blockquote>
<p>Ni matumaini ya Project M kwamba haitakuwa hivyo. <a href="http://www.poptech.org/project_m_the_solution/">Awamu zijazo </a>za mradi huu zitajumuisha usambazwaji wa vifaa vya kupimia VVU majumbani, pia uendelezwaji wa &#8220;huduma za vituo vya simu mtandaoni,&#8221; na utumiaji wa ujumbe wa maandishi wa simu za mkononi ili kutoa huduma binafsi za taarifa za afya kwa wale wanaotibiwa UKIMWI.</p>
<p><em><a href="http://flickr.com/photos/jonjon_2k8/340305918/">Picha ya Simu ya Kiganjani</a> na <a href="http://flickr.com/photos/jonjon_2k8/">JonJon2k8</a> kwenye Flickr.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/11/afrika-ya-kusini-matumizi-ya-simu-za-viganjani-kupambana-na-ukimwi/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/#comments</comments>
		<pubDate>Sun, 26 Oct 2008 08:21:20 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Health]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[Science]]></category>
		<category><![CDATA[South Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Sub-Saharan Africa]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=33</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza nahttp://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 

Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="Juhie Bhatia">http://globalvoicesonline.org/author/juhie-bhatia/</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/10/19/south-africa-a-new-era-in-the-fight-against-hivaids/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><img src='http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2008/10/166594216_8891fa8210_m1.jpg' alt='' class='alignright' /><br />
Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, <a href="http://www.mediaclubsouthafrica.com/index.php?option=com_content&#038;view=article&#038;id=746:cabinet260908&#038;catid=44:developmentnews&#038;Itemid=111">aliteuliwa</a> na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii huenda ikaashiria mabadiliko ya sera za serikali kuhusu suala la VVU na UKIMWI.</p>
<p>Hogan, mwanamama mwanaharakati mkongwe dhidi ya ubaguzi wa rangi na mwanachama wa muda mrefu wa ANC, yaani African National Congress, hapo awali alikuwa mwenyekiti wa kamati ya kusimamia masuala ya fedha. Tangu kuteuliwa kwake kuwa waziri wa afya, amebadili mwelekeo wa serikali iliyopita kuhusu VVU na UKIMWI na <a href="http://www.plusnews.org/Report.aspx?ReportId=80715">kuapa</a><br />
kutoa kipaumbele kwa masuala ya UKIMWI. Jambo hili limezua mshawasha miongoni mwa raia wa Afrika ya Kusini, ambapo wengi wao wanaamini kwamba Hogan anaweza kuimarisha vita vya nchi dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kufuata sera yenye kuzingatia mtizamo wa kisayansi zaidi. Katika picha hii ya <a href="http://www.beatit.co.za/flash/popup.php?videourl=http://www.youtube.com/v/Ml0baEkwhyA">video</a>, wanaharakati wa masuala ya UKIMWI wanashangilia uteuzi wa Hogan katika nafasi yake hiyo mpya.</p>
<p>Siku za nyuma Hogan alipata <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2414">kumkosoa waziwazi </a>Rais wa zamani Thabo Mbeki na msimamo wake juu ya sera ya VVU na UKIMWI. Wastani wa watu milioni 5.7 nchini Afrika ya Kusini wanasemekana <a href="http://www.unaids.org/en/CountryResponses/Countries/south_africa.asp">kuishi na VVU</a> na kiasi cha watu 350,000 walifariki kutokana na UKIMWI mwaka jana nchini humo (wastani wa watu 1,000 kila siku). Kwa upande mwingine Tshabalala-Msimang amelaumiwa vikali kwa kutofanya juhudi za kutosha kukabili tatizo la VVU na UKIMWI nchini humo. Waziri huyo wa zamani wa afya alihamasisha matumizi ya vyakula kama vile beetroot, vitunguu saumu na vinginevyo kama tiba ya VVU na UKIMWI, jambo lililosababisha watu kumbatiza jina la &#8220;Dkt Beetroot&#8221;, na zaidi <a href="http://bunpai.com/2008/10/07/new-era/">ameshutumiwa</a> kwa kusababisha mkanganyo kuhusu matumizi ya dawa za kurefusha maisha (ARV). </p>
<p>Stephen, akiandika kwenye tovuti ya <em>irreverence</em>, <a href="http://www.irreverence.co.za/2008/09/three-cheers-for-barbara-hogan/">alimuita</a> Tshabalala-Msimang kama aibu ya taifa na papo hapo akimwita Hogan kama tumaini lililorejea. Ciaran Parker, akitumia blogu yake ya <em>Ciaran’s Peculier [sic] Blog</em>, <a href="http://ciaranparker.com/2008/09/26/bye-bye-dr-beetroot/">anafafanua</a> kuhusu msimamo wa Tshabalala-Msimang usiokubaliwa na wengi:</p>
<blockquote><p>“Ingawa Kgalema Motlanthe ameahidi kutoleta mabadiliko makubwa, bado ameatosa baadhi wa mawaziri wenye utata mkubwa waliokuwa kwenye serikali ya Mbeki. Mmoja wao akiwa ni Waziri wa Afya, Dkt Manto<br />
Tshabalala-Msimang, aliyekuwa mwananadharia mkubwa katika hoja ya Mbeki ya sera za kukana uwepo wa UKIMWI. Serikali ya Mbeki ilikataa katakata kuona uhusiano uliopo kati ya VVU na UKIMWI, na waziri wake wa afya alijenga hoja kwamba hata dawa za kurefusha maisha, ambazo kwa kweli zimeonyesha kusaidia katika juhudi za kukabili gonjwa hili, zilikuwa ghali mno &#8230; Wataalamu wa afya wanaofanya kazi nchini Afrika ya Kusini na ambao walipingana waziwazi na nadharia za kushangaza za waziri huyu walijikuta wakifanywa kuwa wahanga.&#8221; </p></blockquote>
<p>Mapema juma lililopita, wakati wa  uzinduzi wa <a href="http://www.hivvaccineenterprise.org/conference/2008/">mkutano juu ya Chanjo ya UKIMWI ya Kimataifa ya 2008 </a> (International AIDS Vaccine 2008) huko Cape Town, Hogan, <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2421">alitangaza hadharani </a>kwamba VVU husababisha UKIMWI na kwamba ni lazima kukabiliana nao kwa kutumia dawa za hospitalini. Pia alieleza kwamba serikali ilikuwa na nia ya dhati<br />
kuongeza nguvu katika programu za kuzuia uambukizaji wa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, dawa zinazozuia akina mama wajawazito wenye VVU kuwapatia watoto wao ambao hawajazaliwa maambukizo na kueleza kwamba chango madhubuti ya VVU ilikuwa ikihitajika mno.</p>
<p>Wanasayansi, wanaharakati na wanablogu wengi wameeleza furaha yao kufuatia hotuba iliyotolewa na Hogan. Haley, akiblogu katika tovuti inayoitwa <em>ujasura kama mwanafunzi balozi</em>, ana hili la <a href="http://whereishaley.blogspot.com/2008/10/hallelujah-south-african-health.html">kusema</a>:</p>
<blockquote><p>“Kusema kweli, watu wengi ninaozungumza nao wanashangazwa na jambo hili - kwamba maafisa wa serikali waliochaguliwa kwa njia za kidemokrasi wanakana fikra &#8230; kwamba &#8230; VVU husababisha UKIMWI. Hata hivyo, kwa bahati mbaya, hapa Afrika ya Kusini hivyo ndivyo hali ilivyokuwa &#8230; lakini sasa mambo yamebadilika, msimamo si huo tena.”</p></blockquote>
<p>Ray Hartley, anayeandika katika <em>The Times, Afrika ya Kusini</em>, anablogu <a href="http://blogs.thetimes.co.za/hartley/2008/10/14/hogans-simple-bold-statement-ends-era-of-aids-denialism/">akiongeza</a>: </p>
<blockquote><p>“‘Tunajua kwamba VVU husababisha UKIMWI.&#39;</p>
<p>Kwa kauli hii, Waziri wa Afya, Barbara Hogan, amehitimisha muongo mzima wa aibu ya kukana uwepo wa UKIMWI jambo ambalo limeigharimu Afrika ya Kusini idadi isiyohesabika ya maisha ya binadamu, wakati huohuo wale waliokuwa wakiishi na VVU wakiishia kuishi kana kwamba kwenye kivuli chao wenyewe.”</p></blockquote>
<p>Ni vigumu kueleza idadi kamili ya watu walioathiriwa na sera zilizopita juu ya VVU na UKIMWI, lakini Shirika la Treatment Action Campaign (TAC) (Kampeni ya Kutetea Tiba) <a href="http://www.tac.org.za/community/node/2414">linakadiria</a> kwamba kiasi cha raia milioni mbili wa Afrika ya Kusini walikufa kutokana na kuugua UKIMWI katika kipindi ambapo Mbeki alikuwa madarakani, na kwamba walau jumla ya vifo 300,000 vingeweza kuepukwa endapo tu angetimiza baadhi ya mambo ya msingi ya kikatiba. Baadhi ya wanablogu wanasema kwamba wote wawili, Mbeki na Tshabalala-Msimang wametapakaa damu mikononi mwao. Soneka Kamuhuza, anayeandika kupitia blogu ya <em>Things That Make You Go Mmmh!</em> <a href="http://thingsthatmakeyougommmh.blogspot.com/2008/10/mbeki-war-criminal.html">anamshutumu</a> vikali Mbeki.</p>
<blockquote><p>“Umawazo mgando wao [Mbeki na Tshabalala-Msimang], umbumbumbu wa kukusudia na kujitia kwao kuwa wanyofu kulichochea tu uendelevu wa janga hili. Kutumia njia ya kutazama tatizo zima kwa upana badala ya chanzo chake, pasipo kuingiza na njia nyingine, hakuwezi kuwa njia madhubuti ya kutibu VVU, waliingiza nchi katika wakati mgumu kwa kutumia umbumbumbu wao ambao waliulinda kwa njia zote. Hivi sasa inakadiriwa kwamba Afrika ya Kusini inaongoza duniani kwa kuwa na idadi kubwa ya watu wanaoishi na VVU. Kwa namna fulani, naona ushawishi wa Mbeki katika jambo hili &#8230; Katika nchi ambayo ina utajiri mkubwa wa maliasili, amehadaa rasilimali watu iliyo muhimu sana, kwa kuwanyima fursa ya watu kuamua na kuanza kupambana na tatizo hili la UKIMWI kikamilifu.”</p></blockquote>
<p>Wengi wanaamini kwamba Hogan atarekebisha mambo yaliyoharibika kwa sehemu fulani. Makala katika <em>Peripheries</em> <a href="http://www.peripheries.org/2008/09/26/south-africa-appoints-new-health-minister/">inaonyesha kwamba </a>watu wanatarajia kwamba wakati wa kuwa na ukanaji wa UKIMWI huku ukipewa nguvu na msukumo wa kisiasa nchini Afrika ya Kusini tayari umefikia kikomo. Hata hivyo, wapo ambao hawako kupaparikia mambo haraka hivyo. BillyC, akitoa maoni yake juu ya makala iliyoandikwa katika <em>The Times, la Afrika ya Kusini </em><a href="http://blogs.thetimes.co.za/hartley/2008/10/14/hogans-simple-bold-statement-ends-era-of-aids-denialism/">anasema</a>:</p>
<blockquote><p>“Barbara Hogan ana kazi kubwa mbele yake ili kurekebisha mambo ambayo kwa kiasi fulani tayari amekwishasababisha madhara kwa mfumo wa afya katika uangalizi wa Manto. Uwezo wa wafanyakazi, ari ya kazi, na viwango vya utendaji ukiachia mbali sera za afya na sheria, yote ni mambo ambayo hayana budi kushughulikiwa. Zaidi ya hilo, kuna uhamasishaji wa matumizi ya dawa na upungaji pepo wa kivuduu, vilevile uhusianishaji wa kishetani na sayansi ya magharibi vyote vikiwa vimejikita sawasawa katika mfumo wa kufikiri wa taifa. Itachukua miaka mingi ya kazi ngumu, yenye kujaa ujasiri na unyoofu ili kuturejesha katika mfumo wa afya ulio wa heshima na wenye ufanisi. Tumwombee Barbara Hogan apate kasi. Kusema kweli anaihitaji.”</p></blockquote>
<p><em>Picha ya <a href="http://flickr.com/photos/mvcorks/166594216/">Utepe wa Ukimwi wa Afrika ya Kusini </a>imetoka kwa <a href="http://flickr.com/photos/mvcorks/">mvcorks</a> katika mtandao wa picha wa Flickr.</em></p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/10/afrika-ya-kusini-vvu-na-ukimwi-na-mabadiliko-ya-sera/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
