GlobalVoices katika

South Africa

Kumbukumbu za nchi · 19 jumbe


Habari mpya Kuhusu South Africa

11 Februari 2013

Blogu 10 Bora za Mapishi ya ki-Afrika

MyWeku anatengeneza orodha ya Blogu 10 bora za Mapishiya ki- Afrika kwa mwaka 2013: “Inaonekana kuna blogu milioni moja zinazozungumzia mapishi, lakini ni chache sana zinazoonyesha vyakula vya Kiafrika. Pamoja na hayo imekuwa kazi ngumu kuchagua 10 kati ya nyingi nzuri kwa mwaka huu 2013.”

16 Septemba 2012

Global Voices Yashinda Tuzo Ya Highway Africa

Highway Africa Award for Global Voices

Washindi: Dorothee Danedjo kutoka Kameruni akiwa na Ndesanjo Macha wa Global Voices. Picha ya Ettione Ferreira (imetumiwa kwa ruhusa)


Timu ya Global Voices inayoandika habari za Nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara imeshinda Tuzo ya Telekom Highway Africa katika kundi la “Blogu bora ya TEHAMA ya Kiafrika”. Mhariri wa Eneo hilo Ndesanjo Macha alikuwepo Afrika Kusini kuipokea tuzo hiyo (na kikombe cha ushindi!) tarehe 11 Sepetemba, 2012 kwa niaba ya timu nzima. Mwanablogu na mwandishi wa habari Dorothy Dandejo kutoka Kameruni alikuwa mshindani wa karibu aliyeibuka mshindi wa pili katika kundi hilo hilo.

8 Agosti 2010

Afrika Kusini: Wanablogu Wajadili Hukumu ya Mkuu wa Zamani wa Jeshi la Polisi

Soma makala hii.

Siku ya ijumaa tarehe 2 Julai 2010, aliyekuwa mkuu wa polisi na rais wa zamani wa Shirika la Kimataifa la Polisi (Interpol) Jack Selebi alihukumiwa kwa kosa la rushwa. Hukumu hiyo imezua mdahalo nchini na kadhalika imeacha maswali mengi yasiyo na majibu.

18 Julai 2010

Video jumbe
Afrika ya Kusini: Dakika 67 za Mabadikio – Siku ya Mandela

Soma makala hii.

Nelson Mandela alitumikia kifungo cha miaka 27 jela kule katika Kisiwa cha Robben, Afrika Kusini. Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kwamba Madiba (kama ambavyo wengi wanapenda kumwita huko Afrika ya Kusini) alitumia miaka 67 ya maisha yake katika kupiga vita ubaguzi wa rangi na umaskini. Jumapili hii Julai 18 2010, kutakuwa na maadhimisho ya miaka yake 92 - na pia Siku ya Mandela - siku ambayo watu duniani kote watajitolea dakika 67 ili kuifanya dunia iwe sehemu nzuri ya kuishi kwa wote.

12 Julai 2010

Afrika Kusini: Kandanda Ili Kupinga Ubaguzi

mahojiano mafupi ya video kuhusu mashindano yaliyoandaliwa na timu ya mpira wa miguu ya Refugee VI soccer ynakusudia kuelimisha umma juu ya suala la ubaguzi dhidi ya wageni nchini Afrika Kusini.

17 Machi 2010

Afrika Kusini: Ubaguzi wa Julius Malema

Wakati tabia za Rais Jacob Zuma zimekuwa zikizua mijadala mikali na yenye uhai katika ulimwengu wa blogu wa Afrika Kusini, hivi sasa ni mwanasiasa mwenye utata ambaye pia ni rais wa Umoja wa Vijana wa ANC, Julius malema ambaye anatengeneza vichwa vya habari. Hivi karibuni, aliwaongoza wanafunzi katika kuimba wimbo wa zamani wa kupinga ubaguzi wa rangi unaoitwa Ua Kaburu.

5 Disemba 2009

Video jumbe
Nyenzo ya Mtandaoni ya Kufuatilia Mabadiliko ya Tabianchi

Soma makala hii.

Kuelekea kwenye Mkutano wa Mabadiliko ya TabiaNchi utakaofanyika Copenhagen (COP15) mwezi Desemba 2009, zifuatazo ni baadhi ya nyenzo za mtandoni za kufuatilia mabadiliko ya Tabia Nchi.

23 Novemba 2009

Afrika Kusini: Kikaragosi Kiliochoathirika na VVU Kwenye Kipindi cha Sesame Chaelimisha Kuhusu Ukimwi

Soma makala hii.

Wakati kipindi cha watoto cha Mtaa wa Sesame (Sesame Street) kikisherehekea maadhimisho ya miaka 40 mwezi huu, kwa kizindua msimu wake mpya leo, kikaragosi kizuri kinachovutia cha Muppet katika toleo la Afrika Kusini kinaendelea kusaidia kupambana na kuelimisha kuhusu VVU/UKIMWI.

11 Novemba 2009

Afrika Kusini: Wimbo wa Taifa kwa Wanaoongea Kiingereza

Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya kutamka maneno yake na tatu ambao hatuongei lugha iliyo kwenye wimbo huo.

17 Oktoba 2009

Big Brother Africa msimu wa IV: Mageuzi yameanza

Big Brother Africa 4: Mapinduzi ni mfululizo wa nne wa vipindi vya kituo cha televisheni vinavyoonyesha maisha halisi vya Big Brother Africa, vilivyoanza Septemba 6, 2009. Kipindi hicho kimeshaanza kuzua mijadala na maoni kwenye mtandao wa intaneti kutoka kwa wanablogu na wasomaji wao.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha