The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

South Africa Kumbukumbu za nchi

Kiungo cha RSS kwa South Africa

2009-07-22

Afrika: Obama Atumia Nyenzo Mpya za Habari Kuzungumza na Waafrika

“Umeshawahi kutaka kumuuliza kijana wetu wa Nyangoma maswali yoyote? Kwa maneno mengine, je ungependa Rais wa Marekani, Barack Obama ajibu maswali yako?,” ndivyo inavyoanza makala kwenye blogu ya Hot Secrets inayohusu matumizi ya Obama ya zana mpya za habari ili kukutana na kuongea na Waafrika wa kawaida.

2009-07-19

Afrika Kusini: Kuvuvuzela au Kutovuvuzela?

Mjadala kuhusu kifaa maarufu kinachoitwa vuvuzela kinachopigwa na mashabiki wa mpira wa miguu Afrika Kusini umetawala katika blogu mbalimbali duniani tangu kuanza kwa Kombe la Mabara la mwaka huu nchini Afrika Kusini, lililohitimika wiki iliyopita. Waandishi wa habari, watazamaji wa televisheni, makocha na baadhi ya wachezaji wa kigeni walitoa wito wa kusitisha matumizi ya kifaa hiki katika Kombe la Dunia la 2010 nchini Afrika Kusini. Mabishano haya yana sauti kubwa kama chombo chenyewe.

2009-04-22

Afrika ya Kusini: ANC Yafanya Mjadala wa Uchaguzi Kwa Kutumia huduma ya Twita

Vyama vya siasa nchini Afrika ya kusini vimo katika hatua za mwisho za kampeni ya uchaguzi ujao. Chama tawala cha ANC (African National Congress) kilifanya mjadala kwa kutumia huduma ya twita.

2009-01-26

Blogu za Afrika Zapendekezwa Kupokea Tuzo ya Bloggies 2009

Blogu zilizopendekezwa kwa ajili ya Tuzo ya Tisa ya Zawadi za Weblog: Mapendekezo ya blogu katika mashindano ya Bloggies ya 2009 yalifunguliwa tarehe 1 Januari na kufungwa tarehe 19 Januari. Kwa mujibu wa waandalizi, mashindano hayo ya Bloggies ni mashindano ambayo yamedumu kwa muda mrefu zaidi mtandaoni, na mapendekezo pamoja na uchaguaji wa washindani katika fainali, ni juu ya msomaji wa blogu. Mshindi hupata senti 2,009 za Marekani! Je, ni mabloga gani wa Kiafrika waliopendekezwa kwa ajili ya kinyang'anyiro cha blogu bora zaidi?

2008-11-04

Afrika ya Kusini: Matumizi ya Simu za Viganjani Kupambana na UKIMWI

Afrika ya Kusini imegundua silaha mpya katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI - simu za viganjani. Kwenye mchakato mpya, jumbe za maandishi zitakuwa zikitumwa kila siku kuwahamasisha Wa-Afrika ya Kusini kwenda kupimwa na kutibiwa ugonjwa huo. Mradi huo, unaoitwa Mradi wa Masiluleke au Project M, ulitangazwa rasmi wiki iliyopita wakati wa kongamano ...

2008-10-26

Afrika ya Kusini: VVU na UKIMWI na mabadiliko ya sera

Mwishoni mwa mwezi Septemba, Barbara Hogan, aliteuliwa na Rais wa mpito Kgalema Motlanthe kuwa waziri mpya wa afya wa Afrika ya Kusini, akichukua nafasi ya mtangulizi wake mwenye utata mwingi, Manto Tshabalala-Msimang. Wanaharakati wa masuala ya UKIMWI na raia wengi wa Afrika ya Kusini wana matumaini makubwa kwamba hatua hii ...

2008-10-15

Macho ya Kimataifa kwenye Uchaguzi wa MarekaniVideo post

Kadiri uchaguzi wa Marekani unavyokaribia, ndivyo kadiri macho ya kimataifa yanavyozidi kuelekezwa katika sera za nje za taifa hilo na wagombea wake wakuu. Kazimiradi kama vile ile ya Collective Journalism inayofanywa na Current TV (Uandishi wa Habari wa Umma wa Current TV) na Global Voices' Voices Without Votes (Mradi wa Global Voices - Sauti Zisizo na Kura) zimechukua jukumu la kukusanya taarifa na kuzipa mtazamo wa kimataifa katika masuala ya ndani ya sehemu fulani tu ulimwenguni.

2008-10-01

Afrika Ya Kusini: Mjomba, Urais Uko Wapi?

Ulimwengu wa blogu nchini Afrika ya Kusini umelipuka kutokana habari za hivi karibuni kuhusu mawaziri 11 na manaibu 3 kujiuzulu wakiwemo mawaziri vinara, Trevor Manuel na Naibu Rais, Phumzile Mlambo-Ngcuka. Yafuatayo ni yale wanayosema mabloga …