Kutokuwepo uwazi na weledi katika mchakato wa kumchagua mgombea, mbali na kufahamika nani hasa watachukua nafasi zinazogombewa kabla hata ya uchaguzi katika taasisi hiyo. Hizo zilikuwa baadhi ya sababu zilizotolewa na mwanaharakati wa haki za binadamu, Benilde Nhalivilo, wakati akijitoa rasmi kugombea nafasi kwenye Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Msumbiji[pt], chombo kinachohusika na kuandaa na kusimamia chaguzi nchini humo. Taarifa zaidi zinapatikana kwenye gazeti la A Verdade [pt].
Habari mpya Kuhusu Mozambique
10 Aprili 2013

Vyama vya Siasa Msumbiji na Matumizi ya Intaneti
(…) kuna nafasi ambayo mpaka sasa haijatumiwa ipasavyo na vyama vya siasa nchini Msumbiji, iwe ni kwa ajili ya kueneza propaganda za kisiasa au kufanya kampeni za uchaguzi: nalo ni mtandao wa intaneti.
Jukwaa la Msumbiji liitwalo Olho Cidadão (Jicho la Wananchi) lilizindua blogu mpya tarhe 2 Aprili, 2013, kwa uchambuzi wa uwepo wa vyama vya siasa mtandaoni [pt]. Msumbiji itafanya uchaguzi wa manispaa tarehe 20 Novemba mwaka huu.
29 Januari 2013

Msumbiji: Uhamasishaji wa Kiraia Kuwasaidia Waathirika wa Mafuriko
Baada ya mvua kubwa iliyosababisha mafuriko kusini mwa Msumbiji yaliyowaacha maelfu ya raia bila makazi na wengi kupoteza maisha, kikundi cha kiraia cha Msumbiji Makobo kimeanza kampeni ya mshikamano inayoitwa “S.O.S. Chókwè” kukusanya misaada ya hisani kwa ajili ya waathirika.
12 Julai 2012

Msumbiji: Je, Zana za Uandishi wa Kiraia Zimeua Blogu?
Katika mfululizo mfupi wa makala zake, Profesa Carlos Serra anabainisha baadhi ya sababu zinazoeleza kwa nini blogu za Msumbiji zinaendelea kupungua siku hadi siku. Msomaji mmoja anatoa maoni akidhani kwamba kublogu kunahitaji kazi kubwa katika kuhakikisha kuwa habari mpya zinaendelea kuwepo sambamba na kiwango cha habari hizo. Wakati Serra anasema kwamba zana za uandishi wa kiraia (kama vile twita na facebook) zinaweza kulaumiwa kusababisha hali hii, pamoja na faida za matumizi ya zana hizo.
2 Mei 2011
Msumbiji: Polisi Washambulia Waandamanaji
Siku ya tarehe 6 Aprili, maofisa wa tawi la Polisi wa jamhuri ya msumbiji (PRM) – Kikosi cha Askari Maalum wa Dharura (FIR) – walitumia nguvukusitisha maandamano ya wafanyakazi wa shirika binafsi la ulinzi Group Four Security (G4S). Kwenye Facebook, wanamtandao walionesha kuchukizwa kwao kutokana na vitendo hivyo vya kikatili na kuhoji wajibu wa polisi, sheria na haki za binadamu.
5 Septemba 2010
Msumbiji: Maputo katika Hali ya Tahadhari Kutokana na Machafuko
Jiji la Maputo lipo kwenye hali ya tahadhari wakati machafuko yakisambaa kutokana na kupanda kwa bei ya mkate, maji na umeme. Wakazi wanataarifu kuwepo kwa vurugu mitaani huku hali ikizidi kuwa mbaya.
24 Mei 2010
Msumbiji: Kasheshe la Misaada
Nchi wafadhili zilisitisha kwa muda msaada wa bajeti kwa serikali ya Msumbiji kutokana na hofu za rushwa, na kuwasha cheche za uchambuzi na mjadala kuhusu misaada, rushwa na utawala.
9 Januari 2010
Msumbiji: Kifo Cha Mradi Mkubwa wa Mazao Nishati
Mwishoni mwa mwezi Disemba, Baraza la Mawaziri la Msumbiji lilitoa tamko muhimu. Kibali cha kutumia Hekta 30,000 za ardhi kwa kampuni ya mazao nishati (biofuels) Procana, kimebatilishwa. Shauri la Mradi wa Procana, ulipo kwenye eneo kubwa linalopakana na Mbuga ya Taifa ya Limpopo ambayo imetanda mpaka nje mpaka wa nchi, lilikuwa na utata pamoja na mvutano mkubwa tangu (shauri hilo) lilipoanza mwanzoni mwa mwaka 2007.
30 Disemba 2009

Msumbiji: Je, ni Lugha Ngapi Zinazungumzwa Nchini?
Kuna lugha 20 zinazozungumzwa nchini Msumbiji, kwa mujibu wa tovuti ya serikali, zaidi ya lugha ya serikali ya Kireno. Carlos Serra [pt] anajiuliza kama kuna lugha nyingine zaidi, kwa mujibu wa wataalamu wa lugha mashuhuri:”Kuna mtu aliniambia kuwa zipo kati ya 20 na 26; mwingine akaniambia zipo 17 zilizoandikwa na nyingine bado hazijaweza kuandikwa”.
27 Julai 2009
Afrika: Ujio wa Mkonga wa Seacom Wazua Mjadala
Ujio wa mkonga unaopita chini ya bahari utakao ongeza uwezo na kupunguza gharama za intaneti barani Afrika umewasha majadiliano na mvuto katika ulimwengu wa blogu wa Afrika. Seacom, ambayo inaunganisha Afrika Kusini, Tanzania, Kenya, Uganda na Msumbiji na Ulaya pamoja na Asia, ilianza kutumika moja kwa moja Alhamisi, kwa kuziunganisha nchi za Afrika ya mashariki na Afrika ya kusini kwenye mtandao wa dunia wenye wigo mpana.




























Kiungo cha RSS kwa Mozambique 






mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...