Habari maalum kuhusu Madagascar
Madagaska: Zaidi ya 25 Wauwawa Katika Maandamano Kuelekea Ikulu
Watu wapatao 25 walipigwa risasi na kuuwawa leo katika mji mkuu wa Madagaska, Antananarivo, wakati wa maandamano ya kuelekea ikulu ya nchi hiyo yaliyoitishwa na meya wa jiji Andry Rajoelina baada ya kujitangaza kama kiongozi wa serikali mpya ya mpito katika mkutano wa hadhara wa kisiasa. Katika majuma yaliyopita, ugombeaji wa nguvu za kisiasa kati ya Meya na Rais Marc Ravolamanana kumesababisha ghasia na uporaji.
Madagaska: Kimbunga Chasababisha Kimbunga Cha Kisiasa
Baada ya siku chache kupita nchini Madagaska, idadi rasmi ya madhara yaliyosababishwa na kimbunga kilichopewa jina la Fanele zimewasilishwa. Rais Ravalomanana alikwenda kwenye moja ya maeneo yaliathirika na kimbunga ili kutathmini madhara yaliyotokea.
Uandishi wa kiraia wakati wa kimbunga
Wakati idara inayoangalia athari na majanga, BGNRC bado haina tovuti, taarifa zinahusu ...
2008-10-21
Madagascar: Kuishi ughaibuni hubadili uhusiano
Katika makala iliyochapishwa mwezi Machi, wachumi William Easterly na Yaw Nyarko wanaeleza kwamba katika nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara, kiasi cha fedha kinachotumwa na wahamiaji wanaotoka bara hilo ni wastani wa asilimia 81 ya misaada ya fedha kutoka nchi za kigeni kwa kila nchi.
Dhima ya waMadagascar walio nchi ...
2008-09-06
Nia ya Mwanablogu Mmoja Kumsaidia Mtoto Kamba huko Madagaska
Ikiwa unataka kwenda sambamba na habari mpya mpya kutoka Madagaska, inawezekana kabisa ukawa ni msomaji wa Madagascar Tribune. Na kama wewe ni mdau wa gazeti hilo, hivi karibuni yawezekana ulishakutana na habari iliyoandikwa na mwandishi wa habari Herimanda R kuhusu upasuaji wa maradhi ya nadra na mafanikio yake ambao ulifanyika ...



