Habari kuhusu Ghana kutoka Februari, 2010

Ghana: Mkuu wa Mkoa, Kofi Opoku-Manu, Anapoteza Umaarufu?

  27 Februari 2010

Mkuu wa Mkoa wa Ashanti, Kofi Opoku-Manu, hivi karibuni alionja joto ya jiwe kutokana na matamshi aliyoyatoa kwenye hotuba yake kwa mashabiki wa chama tawala, Nationa Democratic Congress (NDC) tarehe 6 Januari. Kwa mujibu wa Ato-Kwemena Dadzie, Opoku-Manu “aliwasihi mashabiki wa chama kutumia ghasia kusuluhisha tofauti zao.”

Je, Ghana Ipo Tayari kwa Upigaji Kura wa Kwenye Mtandao?

  22 Februari 2010

Tukio la siku mbili lililoanza jana; linaratibiwa na Danquah Instite (DI), kituo cha kutafakari sera, utafiti na uchambuzi, kutengeneza jukwaa la kitaifa kwa washikadau kuongoza majadiliano kuhusu uwezekano wa uanzishwaji wa kuandikisha wapiga kura kwa njia za vipimo vya kibaiolojia na hatimaye mfumo wa upigaji kura kwa njia ya mtandao nchini Ghana.

Ghana: Mapendekezo ya Kuvutia Kwenye Mapitio ya Katiba

  17 Februari 2010

Mwaka 2008, wakati wa Uchaguzi wa rais, wagombea waliwaahidi Waghana kuwa wangeitazama tena katiba ya nchi hiyo. Jambo lililoifanya ahadi hii kuonekana kama ni ya kweli lilikuwa ni nia ya wagombea – pamoja na Rais John Atta Mills – ya kuwashirikisha Waghana katika mchakato huo wa kuitathmini katiba. Inaonekana kuwa rais ametimiza ahadi hiyo, na sasa mapendekezo mapya yanachochea mijadala ya kuvutia.

Misri: Sisi Ni Washindi

Timu ya kandanda ya Misri iliifunga Ghana katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika, na ikapata ushindi wake kwa mara ya tatu mfululizo. Huu pia ni ushindi wa saba tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo kwenye miaka ya hamsini. Wanablogu wanaungana na wananchi wa nchi hiyo kusherehekea mafanikio hayo.