Habari kuhusu Ghana kutoka Julai, 2009

Kameruni: Wanablogu Waijadili Hotuba ya Obama Ghana

  22 Julai 2009

Rais wa Marekani Barack Obama alitoa hotuba yake Ghana ambayo inaweza kuchukuliwa kuwa kama hotuba ya sera yake ya Afrika. Wakameruni wa nyumbani na wale wa ughaibuni wamekuwa wakijadili maneno yaliyotamkwa na Kiongozi wa Marekani mwenye asili ya Afrika kwa kupitia ulimwengu wa blogu.

Afrika: Obama Atumia Nyenzo Mpya za Habari Kuzungumza na Waafrika

  22 Julai 2009

“Umeshawahi kutaka kumuuliza kijana wetu wa Nyangoma maswali yoyote? Kwa maneno mengine, je ungependa Rais wa Marekani, Barack Obama ajibu maswali yako?,” ndivyo inavyoanza makala kwenye blogu ya Hot Secrets inayohusu matumizi ya Obama ya zana mpya za habari ili kukutana na kuongea na Waafrika wa kawaida.

Afrika: Wanablogu wamwombolezea Michael Jackson

  20 Julai 2009

Barani Afrika, wanablogu wanatoa heshima zao za mwisho kwa Michael Jackson baada ya kifo chake hivi karibuni kwa kutuma picha, video za muziki, mashairi pamoja na tafakari. “Pumzika Kwa Amani” anaandika Mwanablogu wa Kenya WildeYearnings. “Sasa unalo anga zima kucheza kwa madaha kwa staili ya kutembea mwezini…”