GlobalVoices katika

Cote d'Ivoire

Kumbukumbu za nchi · 5 jumbe


Habari mpya Kuhusu Cote d'Ivoire

2 Januari 2013

Watu 60 Wauawa kwa Msongamano nchini Abidjan

Magogo ya miti yaliyokuwa yameanguka barabarani yanaonekana kusababisha msongamano mkubwa na ulioua watu 60 na kujeruhi wengine 49 wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya mjini Abidjan, Côte d'Ivoire. Kutokana na ukweli kuwa eneo hilo halikuwa na mwanga wa kutosha inawezekana ndio sababu iliyochangia tukio hilo la msongamano ulisababisha mkanyagano wa watu.

Israel Yoroba jijini Abidjan anaripoti kuhusu msongamano huo wa kutisha [fr] wakati watu wengi wakiwa wamekusanyika kusubiri kushuhudia milipuko ya fataki kuashirika mwaka mpya katika wilaya ya Plateau. Alama habari #drameplateau ilianzishwa kutoa nafasi ya kupatikana kwa habari za wakati huo huo kuhusu tukio hilo la kusikitisha na namna ya kuwasaidia waathirika. Hili nijanga la tatu la namna hii tangu mwaka 2009 [fr] nchini Côte d'Ivoire.

10 Oktoba 2012

Côte d'Ivoire: Wafanyakazi wa Afya Wagoma baada Miezi Minne Bila Mshahara

S.B anatoa maoni juu ya kuanza kwa mgomo usio na ukomo unaoratibiwa na wafanyakazi wa taasisi za afya mjini Abidjan. Katika mtandao wa Connection Ivorienne, anabainisha [fr] kwamba:

Kufuatia mabadiliko ya utolewaji wa huduma za afya ambazo zilitolewa bure kabisa baada tu ya kumalizika kwa mgogoro wa baada ya uchaguzi, sera iliyoanzishwa na serikali ya Côte d'Ivoire, ambayo sasa imeelekeza baadhi ya huduma tu ndizo zitakuwa bure, wafanyakazi wa taasisi kadhaa za afya hawajapata mishahara yao kwa wakati. Kibaya zaidi ni kwamba wakubwa wao hawakupata fungu lolote kwa ajili hiyo kwa zaidi ya miezi kumi na sita.

25 Januari 2012

Ivory Coast: Mjadala Mkali dhidi ya Chombo cha Habari kilichotumia Picha za Mwanablogu Bila Ruhusa

Soma makala hii.

For the blogger and professional photographer Audrey Carlalie, the Christmas 2011 holidays were marked by the fact that her photos of a celebratory firework display were used by certain Ivorian newspapers without her authorization. Kanigui reports.For the blogger and professional photographer Audrey Carlalie, the Christmas 2011 holidays were marked by the fact that her photos of a celebratory firework display were used by certain Ivorian newspapers without her authorization. Kanigui reports.

4 Aprili 2011

Côte d'Ivoire: Televisheni ya Taifa RTI Inawezekana kuwa Inatangaza Kutokea Kwenye Gari la Matangazo

Kama vile alivyoelezea Julie Owono , ni vigumu kupembua mapambano ya kudhibiti vyombo vya habari vya Pwani ya Pembe (Cote d'Ivoire). Taarifa kutoka Waandishi Wasio na Mipaka inaashiria kuwa RTI inaweza ikawa inatangaza kutokea kwenye gari lililoegeshwa kwenye nyumba ya mtu binafsi (fr).

14 Novemba 2010

Ivory Coast: Wimbo Mpya Kwa Ajili Ya Uchaguzi wa Rais

Museke imeweka video ya wimbo mpya “Mpiga Kura” ulioandikwa maalum kwa ajili ya uchaguzi wa rais nchini Ivory coast. Wimbo huo unachezwa na Le Griot-Guére, Jackivoire, Soro Solo, na gitaa la kuongoza linapigwa na mpiga gitaa gwiji kutoka Kongo, Huit-kilos.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha