MyWeku anatengeneza orodha ya Blogu 10 bora za Mapishiya ki- Afrika kwa mwaka 2013: “Inaonekana kuna blogu milioni moja zinazozungumzia mapishi, lakini ni chache sana zinazoonyesha vyakula vya Kiafrika. Pamoja na hayo imekuwa kazi ngumu kuchagua 10 kati ya nyingi nzuri kwa mwaka huu 2013.”
Habari mpya Kuhusu Cameroon
11 Februari 2013
11 Januari 2013

Mashoga Washambuliwa Kaskazini mwa Kameruni
Oscarine Mbozo’a anaripoti [fr] katika blogu ya L'Actu kuwa shoga mmoja akiwa ameambatana na mwenzi wake walizomewa karibu na soko mnamo tarehe 6, Januari 2013, mjini Maroua, Kaskazini mwa Kameruni:
Goche Lamine, mfanyabiashara wa madawa, alikamatwa na mwanafunzi wa shule ya sekondari aitwaye Sanda, mwenye umri wa miaka 17. Umati wa watu uliokuwepo sehemu hiyo baada ya kugutushwa na mtoto aliyekuwa akipiga kelele “samaroka! Samaroka (yaani mashoga katika lugha ya ki-Fulfulde), uliwakimbilia watu hao na kuanza kuwarushia mawe.
16 Septemba 2012

Global Voices Yashinda Tuzo Ya Highway Africa

Washindi: Dorothee Danedjo kutoka Kameruni akiwa na Ndesanjo Macha wa Global Voices. Picha ya Ettione Ferreira (imetumiwa kwa ruhusa)
Timu ya Global Voices inayoandika habari za Nchi za Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara imeshinda Tuzo ya Telekom Highway Africa katika kundi la “Blogu bora ya TEHAMA ya Kiafrika”. Mhariri wa Eneo hilo Ndesanjo Macha alikuwepo Afrika Kusini kuipokea tuzo hiyo (na kikombe cha ushindi!) tarehe 11 Sepetemba, 2012 kwa niaba ya timu nzima. Mwanablogu na mwandishi wa habari Dorothy Dandejo kutoka Kameruni alikuwa mshindani wa karibu aliyeibuka mshindi wa pili katika kundi hilo hilo.
8 Julai 2012
Cameroon: Ndoto za Umeme kwa Ajili ya Maendeleo ifikapo 2035
Cameroon inatarajiwa kufikia hadhi ya soko linalokua kwa kasi ifikapo mwaka 2035 kupitia "mafanikio makubwa" ya hatua kwa hatua katika maendeleo ya miundombinu ya usafiri na nishati. Hata hivyo kufikiwa kwa malengo hayo ndani ya muda uliopangwa hakuonekani kuwashawishi wachambuzi wengi wa masuala ya kisiasa, kwa sababu tu changamoto zilziopo ni nyingi.
4 Januari 2012
Suluhisho la Kiradikali la Umaskini Duniani: Ufunguzi wa Mipaka
Wataalamu kadhaa wanasema kuwa umaskini uliokithiri hauepukiki. Suluhisho la kiradikali zaidi la kupunguza umaskini kwa haraka duniani kwa wataalamu wengi wa uchumi ni kufungua mipaka kati ya nchi na kuruhusu wafanyakazi kuhamia sehemu ambazo nguvukazi inahitajika zaidi.
16 Julai 2010

Cameroon: Vyombo vya Habari Vyachochea Demokrasia
Célestin Lingo anaonyesha uhusiano kati ya vyombo vya habari na mchakato wa demokrasi nchini Cameroon.
13 Novemba 2009
Cameroon: Wezi “wakarimu” na Malipo kwa Kutumia Salio la Simu
Karibu wakazi milioni 20 wa Cameroon wanakabiliwa na kiwango kinachoongezeka cha unyang’anyi. Majambazi wameweza hata kuyavamia makao makuu ya taifa ya polisi na Wizara ya Mambo ya Nje katika mji mkuu wa Yaounde.
26 Oktoba 2009

Misri: Watawala Wa Kiimla na Wake Zao
Baada ya kuziangalia picha za mke wa Rais wa Cameroon, Mmisri Zeinobia anasema: “Sijui ni ni kiasi gani cha pesa alichotumia kwa ajili ya nywele zake na muonekano wake lakini ninafahamu kuwa watu wa Camerron wanazihitaji zaidi hizo pesa.”
22 Julai 2009
Kameruni: Wanablogu Waijadili Hotuba ya Obama Ghana
Rais wa Marekani Barack Obama alitoa hotuba yake Ghana ambayo inaweza kuchukuliwa kuwa kama hotuba ya sera yake ya Afrika. Wakameruni wa nyumbani na wale wa ughaibuni wamekuwa wakijadili maneno yaliyotamkwa na Kiongozi wa Marekani mwenye asili ya Afrika kwa kupitia ulimwengu wa blogu.
24 Machi 2009
Papa Nchini Kameruni (2): Wazee Wa Kanisa, Upotofu na Siasa
Ziara ya kiongozi wa Kanisa La Katoliki nchini Kameruni mwezi huu wa Machi 2009 imepelekea baadhi ya mabloga wa Kikameruni kuelekeza tochi zao kwenye matokeo ya kisiasa (kama yapo) yatakayotokana na ziara hiyo ya Papa nchini humo.




























Kiungo cha RSS kwa Cameroon 





mambo vipi wanablog muko powa wote.kama mumenisoma nijibuni.
Asante. Nimepita hapa natafuta japan na china wamemalizaje ugomvi wao kuhusu visiwa,pia chanzo cha ugomvi...