GlobalVoices katika

Sub-Saharan Africa

Kumbukumbu za sehemu · 284 jumbe


Habari mpya Kuhusu Sub-Saharan Africa

12 Juni 2013

Simu za Bure Kwa Wakulima wa Nigeria?

Soma makala hii. The Future of ICT for Development

Wizara ya KIlimo nchini Naijeria imetangaza mpango wake wa kugawa simu za bure za kiganjani kwa wakulima wa vijijini. Mpango huu umezua mjadala mzito kwenye ulimwengu wa blogu nchini Naijeria.

9 Juni 2013

China Yadaiwa Kuchimba Dhahabu Kinyume cha Sheria Nchini Ghana

Shirika la Habari la Xinhua limeripoti kwamba raia 124 wa Kichina waliodaiwa kushiriki katika uchimbaji wa madini haramu ya dhahabu walikamatwa na kuwekwa kizuizini nchini Ghana. Serikali ya China imetakiwa kulinda na kuwatetea raia wake. Kwa upande mwingine, maoni yaliyotokana na tukio hilo yaliukosoa unyanyasaji unaofanywa dhidi ya watu wa Afrika katika biashara ya madini ya dhahabu inayosimamiwa na China nchini Ghana. Mtandao wa China offbeat unayo maelezo ya kina.

Je, Italia Iko Tayari kwa Waziri Aliyezaliwa Afrika?

“Je, Italia iko tayari kwa Waziri wa Serikalki aliyezaliwa Afrika?,” Donata Columbro anauliza:

Miezi miwili baada ya uchaguzi wa hivi karibuni, Italia ina serikali mpya. Na Cécile Kyenge, mwenye umri wa miaka 48,  daktari wa upasuaji macho na raia wa Italia aliyezaliwa Kongo, ni Waziri mpya wa Ushirikiano katika baraza la mawaziri la Waziri Mkuu Enrico Letta.

7 Juni 2013

Matatizo Makuu ya Raia wa Benin ni Yapi?

Tite Yokossi anafunua matokeo ya kura ya maoni iliyoendeshwa na Mfuko wa Zinsou ambao uliwauliza wananchi wa Benin ni yapi ndiyo matatizo yao makuu leo [fr]. Tatizo la kwanza lililoorodheshwa lilikuwa uwezo mdogo wa kufanya manunuzi miongoni mwa watumishi wa umma. Mengineyo ni uwezekano wa kupata fursa ya elimu, huduma ya maji safi, huduma za afya na umeme, ulinzi wa raia na misaada kwa wakulima.

Gwaride la Kwanza la Mashoga Nchini Lesotho

Leila Hall anablogu kuhusu gwaride la kwanza la mashoga kuwahi fanyika nchini Lesotho:

Tukio hilo limeandaliwa na Kikundi cha Kutoa msaada cha MATRIX- Shirika lisilo la kiserikali la Lesotho- linatetea haki za watu kama wasagaji, mashoga, wenye hisia za mapenzi kwa jinsia zote mbili, Wanaogeuza jinsia nchini humo. Shirika hilo, ambalo lilitambuliwa kisheria mwaka 2010, kama lilivyo gwaride la mwaka huu ni shirika la kwanza la aina yake nchini Lesotho.

5 Juni 2013

Uganda: Hatimaye Magazeti Yaliyofungiwa na Polisi Yafunguliwa

Soma makala hii.

Uganda imeruhusu magazeti mawili kufunguliwa tena baada ya msuguano uliodumu kwa siku 11 kati ya serikali na vyombo vya habari juu ya barua yenye waliyoipata ambayo iliyoonyesha njama ya kumtayarisha mtoto wa kwanza wa Rais Yoweri Museveni kumrithi kiongozi huyo aliyedumu kwa miaka 27.

1 Juni 2013

Photos jumbe Video jumbe
Wafanyakazi wa Sekta ya Afya Nchini Msumbiji Wagoma Kudai Maslahi

Soma makala hii.

Wafanyakazi wa sekta ya afya nchini Msumbiji wamekuwa katika mgomo uliodumu kwa siku kumi na kusababisha kusimama kwa huduma katika vitengo vingi vya kutoa huduma za afya kote nchini humo. Mgogoro wao na serikali umetokana na madai yao ya kuboreshewa maslahi na mazingira ya kazi pamoja na kurekebishwa kwa gharama za chumba cha wagonjwa mahututi katika mahospitali yote nchini humo.

30 Mei 2013

Wafanyakazi Wavamia Majengo ya Serikali Nchini Mauritania

Photo of the clashes, uploaded by Abo Bakr Ahmado on his Facebook

Picha ya mapigano, iliyowekwa na Abo Bakr Ahmado kwenye ukurasa wake wa Facebook

Siku ya Jumanne asubuhi, Mei 28, 2013, maelfu ya vibarua, wanaolipwa ujira wao kwa kufanya kazi kwa siku, walianzisha maandamano makubwa [ar] huko Zouérat, mji mkuu wa jimbo la Tiris Zemmour kasikazini mwa Mauritania, wakidai mikataba inayoeleweka na haki zao nyinginezo ikiwa ni pamoja na kumalizwa kwa ukiritimba wa wafanyabiashara kwenye makampuni ya machimbo ya madini katika nchi za Kiarabu (ARMICO). Wafanyakazii hao waliandamana kuelekea kwenye makao makuu ya utawala wa jimbo hilo, majengo ya mmoja wapo wa makampuni ya wakandarasi, pamoja na majengo ya kituo cha redio ya taifa. Jeshi [ar] liliingilia kati kudhibiti hali hiyo na kuyatawanya maandamano hayo.

Mwanaharakati Magdy Ahmed alitwiti kuhusu kutoroka kwa gavana wa Tiris Zemmour baada ya wafanyakazi kuandamana [ar]:

@mejdmr :والي ولاية زويرات الجنرال ول باهية و الوالي المساعد وشرطة المدينة يفرون أمام غضب عمال الجرنالية الذين اقتحمو مبني الولاية والإذاعة الجهوية

@mejdmr: Gavana, Ould Bahia, naibu gavana na polisi walikimbia baada ya kushuhudia hasira ya wafanyakazi hao kwa siku moja walipovamia ofisi ya gavana na kituo cha redio ya taifa.

28 Mei 2013

Kwa nini Mashirika ya Umma Yameshindwa Nchini Zambia

Elias Munshya, mwanasheria na mchungaji wa Zambia, anaeleza kwa nini mashirika ya umma yamedumaa nchini Zambia tangu uhuru:

Mashirika ya umma hayajawahi kutengeneza faida tangu mwaka 1964. Yamekuwa yakiendeshwa kiholela bila utaalamu wa kibiashara bali kisiasa. Mashirika haya hayajawahi kuwa na wataalamu wanaoendesha bodi husika bali yamejaa wafanyakazi kwa misingi ya mahusiano ya undugu, ubinamu, upwa na ujukuu na wanasiasa

.

Botswana: Kuibwa kwa Kazi ya Sanaa ya “Bushman's Secrets”

MyWeku anaichambua filamu yenye maudhui halisi (documentary) inayoelezea wizi wa kazi ya sanaa ya Sana iitwayo “Bushman's secrets”:

Filamu hii inachora picha inayosikitisha ya namna ambavyo Uniliver, kampuni inayojinadi kama “mzalishaji mkubwa tena nambari moja duniani wa barafu zitengenezwazo kwa maziwa maarufu kama ice cream,” sasa linatumia bila aibu maudhui ya kazi ya sanaa ya Bushman's Secrets kujitangaza kama bidhaa ya kupunguza uzito.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha