The Global Voices Lingua project hopes to bring GV content to new linguistic audiences - Details

Also in:

Sub-Saharan Africa Kumbukumbu za sehemu

Kiungo cha RSS kwa Sub-Saharan Africa

2009-11-16

Senegal ,
Haiti

Wiki hii, waandishi wawili wenye asili ya Kiafrika wanaoandika kwa Kifaransa walipewa tuzo mbili zenye kuheshimika sana katika fasihi ya Kifaransa: Ulimwengu wa blogu za wanaozungumza Kifaransa katika Karibea umekuwa ukinguruma juu ya kutosheka kwao mara mbili kwa mpigo, katika makala hii kutoka Haiti, na hii kutoka Guadeloupe na hii kutoka Martinique [Fr].

2009-11-13

Uganda

Wanasiasa wa Uganda wanakuwa kama panzi: “kufuatia hali ya kufikia kikomo kwa tawala nyingi za kiimla, Museveni na washirika wake katika ukaliaji wa mabavu wa Buganda kwa kutumia silaha wanaanza kuwa kama panzi.”

2009-11-11

South Africa

Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini kwa wanaoongea Kiingereza: Ni njia kuu iliyoje ya kufafanua kwa kuonyesha Wimbo wa taifa wa Afrika Kusini kwa wale kati yetu ambao kwanza hatuufahamu mpaka sasa, pili tunaoufahamu lakini pengine hatujui jinsi ya kutamka maneno yake na tatu ambao hatuongei lugha iliyo kwenye wimbo huo.

Naijeria: Wanablogu Wajadili Sifa Mbaya ya Naijeria

Inajulikana vyema kuwa Naijeria ina tatizo la muonekano – utapeli wa 419 kwenye intaneti, rushwa, uharamia wa mafuta katika jimbo la Delata – kwa watu wengi, huu ndio uhusiano unaokuja akilini wakati nchi yenye watu wengi zaidi Afrika inapotajwa.

2009-11-10

Angola: Gharama za Juu za Maisha Mjini Luanda

Gharama kubwa ya maisha nchini haieleweki: viashiria vya maendeleo vya hali ya juu havishabihiani na hali ya kifedha ya Waangola wengi na havitafsiriki katika viwango vya maisha vya wasio na hali nzuri kiuchumi.

Nigeria

Chidi Opara anamkumbuka Ken Saro-Wiwa, Mwandishi wa Kinaijeria, mwanaharakati wa mazingira na haki za walio wachache ambaye aliuwawa na watawala wa kijeshi wa Naijeria tarehe 10 Novemba, 1995.

Kenya

Ubia wa Kuleta Mabadiliko umetoa tamko linalowataka mwai kibaki na raila odinga kushirikiana na mahakama ya kimataifa ya Jinai na kuhakikisha muswada wa Tume Maalum unapitishwa nchini kenya na kurasimishwa kama sheria ndani ya wiki mbili.

2009-11-07

Ghana

Sehemu ya kwanza ya vionjo vya Ghana iliyotayarishwa na Gayle: Nchini Ghana, kila kanda ina kitu cha kutoa. Utamaduni, historia, pwani, wanyama na mimea, unaweza ukavivinjari nchini kote, kutokea kwenye mitisitu ya kitropiki kule kusini mpaka mbuga za savana za kaskazini. kama ni mpenzi wa pwani au historia, utaburudika na ziara hii ya sehemu za pwani.

2009-11-05

Kenya ,
Nigeria

Marvin anaandika kuhusu Afripot, tovuti ya habari inayotilia makini habari za Afrika: “Hivi sasa anatambulisha chungu cha kuyeyushia Afrika – Afripot. Tayari nimo ndani ninayeyuka na ninatumaini kukuona pale na wewe pia kwani mazungumzo kuhusu Afrika na Waafrika yanachukua kasi na kupamba moto. Ni nani ajuaye, inaweza kutengeneza joto la kutosha na kulazimisha mabadiliko tuayoyahitaji sana.”