<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?>
<rss version="2.0"
	xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/"
	xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/"
	xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/"
	xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom"
	xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/"
	xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/"
	>

<channel>
	<title>Global Voices in Swahili &#187; Pakistan</title>
	<atom:link href="http://sw.globalvoicesonline.org/category/world/south-asia/pakistan/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
	<link>http://sw.globalvoicesonline.org</link>
	<description>Dunia inaongea, je unasikiliza?</description>
	<lastBuildDate>Wed, 02 Dec 2009 12:35:07 +0000</lastBuildDate>
	<generator>http://wordpress.org/?v=2.8.4</generator>
	<language>en</language>
	<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
	<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
			<item>
		<title>Pakistani: Katika Vita</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/pakistani-katika-vita/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/pakistani-katika-vita/#comments</comments>
		<pubDate>Wed, 04 Nov 2009 09:27:36 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Human Rights]]></category>
		<category><![CDATA[Law]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[Roundups]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=511</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naRezwan  &#183; Imetafsiriwa na j nambiza tungaraza &#183;  Angalia ujumbe mama 
Mohammad Malick anatoa maoni juu ya shambulizi la kigaidi la hivi karibuni kwenye soko la watu wa tabaka chini na la kati huko Peshawar: “limeonyesha kuwa hii ni vita ambyo magaidi wanasimama upande mmoja wa mstari wa damu, na sisi [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rezwan/">Rezwan</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/11/03/pakistan-at-war/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><em>Mohammad Malick</em> <a href="http://ahraza.wordpress.com/2009/11/02/we-must-declare-state-of-war/">anatoa maoni</a> juu ya shambulizi la kigaidi la hivi karibuni kwenye soko la watu wa tabaka chini na la kati huko Peshawar: “limeonyesha kuwa hii ni vita ambyo magaidi wanasimama upande mmoja wa mstari wa damu, na sisi wananchi upande mwingine.”</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/11/pakistani-katika-vita/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Wanablogu Wa Asia Kusini Na Tuzo Ya Nobeli Ya Amani Aliyopewa Obama</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 12 Oct 2009 12:31:53 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[Bangladesh]]></category>
		<category><![CDATA[Breaking News]]></category>
		<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[India]]></category>
		<category><![CDATA[International Relations]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Sri Lanka]]></category>
		<category><![CDATA[War & Conflict]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=368</guid>
		<description><![CDATA[Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Amani ya Nobeli leo. Wanablogu na wanaoblogu habari fupi fupi huko Asia kusini wanaelezea maoni yao kuhusu habari hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/rezwan/">Rezwan</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/10/09/south-asian-bloggers-on-obama%E2%80%99s-nobel-peace-prize/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p><div class="wp-caption aligncenter" style="width: 430px"><img alt="Picha kwa hisani ya http://www.flickr.com/photos/marcn/2174935053/ na imetumika chini ya hati miliki huria " src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/10/barack-Obama-640x480.jpg" title="Barack Obama" width="420" height="282" /><p class="wp-caption-text">Picha kwa hisani ya http://www.flickr.com/photos/marcn/2174935053/ na imetumika chini ya hati miliki huria </p></div><br />
Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Nobeli ya Amani leo. <a href="http://news.bbc.co.uk/2/hi/europe/8298580.stm">Kwa mujibu wa kamati ya Nobeli</a> (Obama) amestahili kupokea tuzo hiyo kutokana na “juhudi zake za kuimarisha diplomasia ya kimataifa na ushirikiano baina ya watu”.</p>
<p>Hili limekuwa ni jambo la kushangaza kwa watu wengi duniani. Kwa nadharia tuzo hii inapaswa kutolewa kwa mtu au shirika lililojihusisha katika kupata ufumbuzi wa mgogoro mrefu wa kijeshi. Lakini kumeshawahi kuwepo na utofauti huko nyuma na Obama ni mmoja wa hali hizo tofauti kwani alianza kazi ya urais baada ya kupendekezwa mwezi Februari.</p>
<p>Gazeti la The New york Times <a href="http://thelede.blogs.nytimes.com/2009/10/09/world-reaction-to-a-nobel-surprise/">limetoa muhtasari</a> wa baadhi ya marejeo ya maoni kutoka duniani kote. Sasa hebu na tuangalie jinsi wanablogu na wale wanaoblogu makala fupi fupi kutokea Asia Kusini wanavyoelezea maoni yao kuhusu habari hii.</p>
<p>Kutokea Bangladeshi, <em><a href="http://bdoza.wordpress.com/2009/10/09/obama-own-nobel-peace-prize-2009-is-it-premature/">An Ordinary Citizen</a></em> haamini na anasema kuwa tuzo hiyo imetolewa kabla ya wakati wake.</p>
<blockquote><p>
Tunazienzi juhudi zake za kuleta amani ambazo huwa anazianzisha tu na bado tunasubiri matokeo.<br />
Je si kweli kwamba muda bado haujafika kwake kuipokea tuzo hiyo? Hatuna hakika ni kwa jinsi gani (tuzo hii) itaathiri mtazamo wake.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa India <a href="http://churumuri.wordpress.com/2009/10/09/churumuri-poll-does-obama-deserve-nobel/">Churumuri</a> anayo maswali kadhaa rahisi:</p>
<blockquote><p>Je Obama anastahili tuzo hii? Je amefanya jambo lolote linaloihalalisha? Je kwa kumpa kijana mbichi kama huyu, wakati wa uchanga wa urais wake, kunawashusha hadhi wale wote waliofanya kazi ngumu na kwa muda mrefu ili kuipokea? Au haidhuru chochote, kwani tuzo ya Nobeli ni tuzo ya kisiasa aliyopewa Yasser Arafat na Menanchem Begin? (kama vile ambavyo yeyote aliyewahi kusoma The Prize kilichoandikwa na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Irving_Wallace">Irvin Wallace</a> anaweza kufahamu)</p></blockquote>
<p>Na bado kutokea India, <a href="http://zoooni.blogspot.com/2009/10/obama-n-his-nobel-win.html">Zooni </a>ni mshabiki wa Obama, lakini ameshangazwa pia:</p>
<blockquote><p>Ok kabla haujafikiria vibaya mimi si kati ya wale wanaomchukia Obama… ninampenda vilivyo, nimeandika makala ya kumpongeza kwa ushindi wake wa urais, je ameshinda nini na kwa sababu ipi, alikuwa kazini kwa wiki 2 tu wakati alipopendekezwa (mapendekezo yalikoma tarehe 1 Februari). Nadhani Obama alishinda tuzo kutokana na kampeni yake kabambe!</p></blockquote>
<p>Kutokea Pakistan, <em>Temporal</em> wa blogu ya <em>Baithak</em> <a href="http://baithak.blogspot.com/2009/10/nobel-peace-prize-2009-obama-gets-what.html">amekuwa mkali kidogo katika maoni yake</a>:</p>
<blockquote><p>Mwaka huu unaweza ukawa ndio mwaka ambao utaashiria kuanza kushuka kwa tuzo ya Nobeli. Wanakamati walikuwa wanakula au kuvuta kitu gani?</p>
<p>Rais Obama anaweza kustahili tuzo hii katika miaka ijayo. Lakini sio katika wakati huu. Ndio kwanza  ameanza jitihada na  ado hajaacha alama yake kwenye amani ya dunia.</p></blockquote>
<p>Mwanablogu wa Ki-Sri Lanka <em>Indi.ca</em> <a href="http://globalvoicesonline.org/2009/10/09/south-asian-bloggers-on-obama%E2%80%99s-nobel-peace-prize/Indi.ca%20http://indi.ca/2009/10/obamas-nobel-peace-prize/">anafikiri kuwa</a> tuzo hii itamuumiza Obama nyumbani (Marekani):</p>
<blockquote><p>Nafikiri kuwa Obama ni mtu muungwana zaidi anayetembea katika uso wa dunia hii leo. Hata hivyo, sidhani kama ameshafanya kile ambacho anataka kukifanya. Nobeli inaweza kumsaidia kinadharia, lakini inaweza kumuumiza nyumbani (Marekani). </p></blockquote>
<p>Wanaondika blogu fupi fupi duniani kote walikuwa wametingwa leo kwa kuelezea mshangao na kutoamini baada ya kuzisikia habari. Yafuatayo ni baadhi ya maoni kutoka kwa watumiaji wa Twita wa Asia Kusini:</p>
<blockquote><p><a href="http://twitter.com/vijaysankaran">@vijaysankaran</a>: Tuzo ya nobeli sasa imekuwa kama <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Bharat_ratna">Bharat Ratna</a>… inahusu wewe ni nani, na siyo ulichokifanya-)</p>
<p><a href="http://twitter.com/tantanoo">@tantanoo</a>: kwa hiyo Bush alitangaza vita, Obama anaomba amani na kushinda tuzo ya Nobeli. Mahesabu mazuri.</p>
<p><a href="http://twitter.com/santhemant">santhemant</a>: “rais wa Marekani Obama apokea tuzo ya Amani kwa kuendesha VITA sehemu nyingi.. kwa kuiunga mkono Pakistani na kupuuza nchi za kidemokrasia kama vile India.</p>
<p><a href="http://twitter.com/saniakhan">saniakhan</a>: sijui kama naweza kuunga mkono ushindi wa Rais Obama wa Tuzo ya Nobeli huku kukiwa na ndege za kivita za drones huko Pakistan bado zikiendelea kupiga.</p>
<p><a href="http://twitter.com/YusufKhan">YusufKhan:</a> Guantanamo bado iko wazi, ndege za drone bado zinaangusha mabomu huko Pakistani, vita bado vinaendelea huko Iraq/Afghanistan, na bado Obama anashinda tuzo ya Amani ya Nobeli. Yay.</p>
<p><a href="http://twitter.com/TinyToots">@TinyToots</a>: mimi pia ninahitaji Tuzo ya Amani ya Nobeli. Kila siku ninajiepusha na kuwafanyia fujo watu wengi. Kwa nini hakuna mtu anayenipendekeza?</p>
<p><a href="http://twitter.com/OldmonkMGM">@OldmonkMGM</a>: mchague mtu asiyefanana na wengine: Dalai Lama, Mother Teresa, Martin Luther King, Barack Obama.</p></blockquote>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/10/wanablogu-wa-asia-kusini-na-tuzo-ya-nobeli-ya-amani-aliyopewa-obama/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Pakistani: Tatizo La Sukari Limeifanya Ramadhani Kuwa Chungu</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/pakistani-tatizo-la-sukari-limeifanya-ramadhani-kuwa-chungu/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/pakistani-tatizo-la-sukari-limeifanya-ramadhani-kuwa-chungu/#comments</comments>
		<pubDate>Mon, 31 Aug 2009 14:15:10 +0000</pubDate>
		<dc:creator>j nambiza tungaraza</dc:creator>
				<category><![CDATA[English]]></category>
		<category><![CDATA[Food]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Humanitarian]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=315</guid>
		<description><![CDATA[Upungufu wa sukari pamoja na kupanda kwa bei nchini Pakistani mwaka huu kumewaathiri walaji na kumesitisha ongezeko la matumizi wakati wa mwezi wa ramadhani. Wanablogu wa kipakistani wanaichambua hali hiyo.]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/faisal-kapadia/">Faisal Kapadia</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/j-nambiza-tungaraza/'>j nambiza tungaraza</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2009/08/28/pakistan-sugar-crisis-turns-ramadan-bitter/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Kila mwaka wakati wa mwezi wa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Ramadan">Ramadhani</a> huwa kuna upungufu kwenye masoko ya bidhaa za chakula nchini Pakistani kutokana na kuongezeka kwa mahitaji. Mwaka huu upungufu umetokea hasa kwenye <a href="http://www.nation.com.pk/pakistan-news-newspaper-daily-english-online/Regional/Lahore/18-Aug-2009/Sugar-vanishes-from-retail-market">soko la sukari</a>. Ili kudhibiti serikali inapanga kuongeza ukubwa wa mauzo ya sukari kwa kupitia <a href="http://www.geo.tv/8-26-2009/48279.htm">maduka ya vifaa</a> (yaliyopewa ruzuku na serikali) kutoka tani 40,000 mpaka tani 100,000. hata hivyo, unapoendesha nje ya maduka hayo kuna ushahidi mkubwa kuweza kushawishi mtu yeyote kuwa hakuna mgawo wa kutosha wa sukari.</p>
<p>Kwa mujibu wa ripoti katika gazeti la <a href="http://www.dawn.com/wps/wcm/connect/dawn-content-library/dawn/the-newspaper/local/karachi-sugar-shortage-at-utility-stores-persists-689">The Dawn</a>, ambalo linaelezea hali ya ugavi mjini Karachi, maduka yanapata mgawo mdogo zaidi ya kawaida na hayana uwezo wa kuhudumia mahitaji ya walaji. Bei ya sukari katika soko la wazi ilipanda kufikia Rupia 55-58 kwa kilo (kama ikipatikana) ambapo bei rasmi ya mauzo kwa sukari ni Rupia 38 kwa kilo.</p>
<p><em>Hassan Khan</em> anaelezea <a href="http://hassaankhan.blogspot.com/2009/08/sugarphobia.html">upande wa kisiasa</a> wa tatizo hili katika blogu yake:</p>
<blockquote><p>Pakistani ina viwanda vya sukari vipatavyo 80. Vingi ya viwanda hivyo vinamilikiwa na wawekezaji pamoja na wanasiasa. Upeo wa unafiki ni kwamba kabla ya ramadhani, walianza kuhodhi sukari na bei yake ikaruka kutoka Rupia 38 mapaka Rupia 54. Kila unapowasha idhaa ya habari ya televisheni ya Pakistani mambo huonekana kuwa mabaya na yanaonekana mabaya zaidi wakati mgogoro umefikia upeo na waziri akivipasha habari vyombo vya habari kwamba kutokana na ongezeko la bei katika soko la kimataifa la sukari, bei ya sukari inaongezeka nchini Pakistani.</p></blockquote>
<div class="wp-caption alignnone" style="width: 430px"><img alt="Uzalishaji wa miwa nchini Pakistani. Picha na mtumiaji wa Flickr Omer Wazir" src="http://globalvoicesonline.org/wp-content/uploads/2009/08/sugarcane-Pakistan-640x480.jpg" title="sugarcane Pakistan [640x480]" width="420" height="280" /><p class="wp-caption-text">Uzalishaji wa miwa nchini Pakistani. Picha na mtumiaji wa Flickr Omer Wazir</p></div>
<p><a rel="cc:attributionURL" href="http://www.flickr.com/photos/thewazir/">http://www.flickr.com/photos/thewazir/</a> / <a rel="license" href="http://creativecommons.org/licenses/by-sa/2.0/">CC BY-SA 2.0</a></p>
<p><em>Sana Saleem</em> <a href="http://sanasaleem.com/2009/08/25/pakistan-sugar-crisis-a-farce/">anasema</a> kuwa upungufu wa sukari umetokana na uzalishaji mdogo wa mazao mwaka huu:</p>
<blockquote><p>Imedaiwa kwamba wakulima wanawalaumu wamiliki wa viwanda vya sukari kwa kutolipa vizuri. Takwimu zinaonyesha kuwa malipo kwa wazalishaji yalicheleweshwa kwa zaidi ya miezi minane mpaka kumi. Hii iliwavunja mioyo wakulima na kuacha kuzalisha miwa na kuchagua kuzalisha ngano badala yake ili kupata vivutio vilivyokuwepo. Na sasa imefika wakati wa visa vya wenye viwanda. Siyo tu kwamba wenye viwanda wanalaumiwa kwa kuchelewesha malipo na kusababisha upungufu wa aslimia 15 mpaka 20 ikilinganishwa na mwaka jana, pia wamehodhi kiwango kikubwa cha mazao. Maza ohayo yamehifadhiwa ili kutengeneza upungufu kidanganyifu kwenye soko. </p></blockquote>
<p><em>Bilquis</em>, mtaalamu-mshauri kutoka Lahore, anatoa uchambuzi wa kitaalamu juu ya suala hili katika <a href="http://changinguppakistan.wordpress.com/">CHUP</a>:</p>
<blockquote><p>Mwaka huu ulishuhudia upungufu wa kawaida  katika uzalishaji wa sukari. Kwa ujumla, wakulima, sawa na wengine, huzalisha mazao ambayo yatawapatia faida zaidi. Katika mwaka 2008-09, serikali ya sasa iliongeza bei ya (kununua) ngano kufikia <strong>Rupia 950</strong> (kwa bei ya chini zaidi) ili kuwahamasisha wakulima wazalishe ngano. Hiki kilikuwa ni kivutio na kilipelekea kuwavutia wakulima wengine kuzalisha ngano (kwa sababu ina faida). Na matokeo yake, wakulima wa miwa walihamia kwenye uzalishaji wa ngano ambko kulisababisha upungufu wa uzalishaji wa miwa.</p>
<p>Zaidi, katika muongo uliopita, uzalishaji wa miwa umepungua kutokana na ugumu ulipo kwenye soko la sukari. Wataalamu mbalimbali wanasema kuwa wakulima wamepunguza maeneo yaliyotengwa kwa uzalishaji kutokana na upungufu wa maji, tabia za utawala za wenye viwanda vya sukari, uchelevu wa malipo, ongezeko la gharama za uzalishaji, magonjwa na mashambulizi ya panya. Na hasa wanawalaumu wamiliki wa viwanda na uchelevu au ukosefu wa malipo kwa wakulima na upungufu wa maji kwa ajili ya kumwagilia, vitu ambavyo vinawafanya wakulima wasite  kuzalisha zao hilo. Na hivyo, sababu hizo mbili zimepunguza mgawo wa sukari kwa asilimia <strong>15</strong> mpaka <strong>20</strong> ikilinganishwa na mwaka jana.</p></blockquote>
<p>Hivi sasa, serikali ya Pakistani inafikiria kuagiza sukari kutoka ng’ambo ili kukabili upungufu. Hata hivyo, wafanyabiashara wan je wa sukari kama vile Brazil na India pia wameongeza bei zao. Kwa hiyo bei haitashuka katika muda wowote hivi karibuni. Kitakachotokea katika siku chache zijazo ni muhimu kwani watu wako tayari kutoka mitaani na kufanya maandamano kupinga tatizo hili la sukari.</p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2009/08/pakistani-tatizo-la-sukari-limeifanya-ramadhani-kuwa-chungu/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
		<item>
		<title>Pakistani: Musharraf Aondoka Jengoni</title>
		<link>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/</link>
		<comments>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/#comments</comments>
		<pubDate>Fri, 22 Aug 2008 14:29:29 +0000</pubDate>
		<dc:creator>Deogratias Simba</dc:creator>
				<category><![CDATA[Feature]]></category>
		<category><![CDATA[General]]></category>
		<category><![CDATA[Governance]]></category>
		<category><![CDATA[Pakistan]]></category>
		<category><![CDATA[Politics]]></category>
		<category><![CDATA[South Asia]]></category>
		<category><![CDATA[Swahili]]></category>
		<category><![CDATA[Weblog]]></category>

		<guid isPermaLink="false">http://sw.globalvoicesonline.org/?p=12</guid>
		<description><![CDATA[Ilichapwa kwanza naAwab Alvi  &#183; Imetafsiriwa na Deogratias Simba &#183;  Angalia ujumbe mama 
Imepita miaka nane, siku mia tatu na ushee tangu mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu yaliyoongozwa na Jenerali wa Jeshi la Pakistani yalipofanyika na hivyo kumpokonya madaraka kiongozi fisadi Nawaz Sharif. Wakati huo kulikuwa na matumaini ya kesho mpya, ilikuwa ni [...]]]></description>
			<content:encoded><![CDATA[<em>Ilichapwa kwanza na<a href="http://globalvoicesonline.org/author/awab-alvi/">Awab Alvi</a>  &middot; Imetafsiriwa na <a href='http://sw.globalvoicesonline.org/author/simbadeo/'>Deogratias Simba</a> &middot;  <a href='http://globalvoicesonline.org/2008/08/19/pakistan-musharraf-has-left-the-building/'>Angalia ujumbe mama</a></em> 
<br /><p>Imepita miaka nane, siku mia tatu na ushee tangu <a href="http://kadnan.com/blog/2008/08/18/17th-august-1988-18th-august-2008/">mapinduzi yasiyo ya kumwaga damu</a> yaliyoongozwa na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Pervez_Musharraf">Jenerali wa Jeshi la Pakistani</a> yalipofanyika na hivyo kumpokonya madaraka kiongozi fisadi Nawaz Sharif. Wakati huo kulikuwa na matumaini ya kesho mpya, ilikuwa ni mwendo wa madaha kuelekea kwenye dira iliyofifia iliyopachikwa jina la ‘mwamko wa wastani wenye kuongozwa na fikra pevu’ na ama kwa hakika hatua muhimu katika kuiondolea jamii gonjwa lililogeuka kuwa janga, yaani, rushwa. Wakati huo raia wa Pakistani walisherehekea, lakini haikupita muda mrefu kabla watu hawajang’amua kuwa walikuwa tena kwenye janga wasilotaka, na kwa bahati mbaya ujaji huo polepole uligeuka kuwa utawala wa kidikteta usiotakikana. Baada ya miezi mingi ya utawala wa mabavu, hivi majuzi kulitokea tukio la kumaliza utawala uliodumu muda wa miaka tisa kasoro siku sitini, na hapa Pakistani inafungua ukurasa mpya. </p>
<p>Ilionekana kama siku nyingine nchini Pakistani lakini mara iligeuka kuwa inayojijaza munkari na mara minong’ono ilianza kusambaa miongoni mwa raia wakati habari zilipoanza kusambaa. Watu hao waligubikwa na <a href="http://www.teeth.com.pk/blog/2008/08/18/safe-exit-today-safe-entry-for-future-dictators-tomorrow">mnong’ono mmoja baada ya mwingine</a> kutoka katika taarifa zilizorushwa na vituo vya televisheni kwenda kwenye ujumbe mfupi wa maneno na hata barua pepe; ilikuwa kana kwamba majaaliwa ilikuwa yaamuliwe na kila mmoja wao. Gazeti tando moja linalokwenda kwa jina la linatupa muhtasari makini kuhusu msukumo wa minong’ono hiyo katika sentenso moja: &#8216;<a href="http://www.deadpanthoughts.com/?p=509">Simu inaita – Mushy anaondolewa madarakani kwa manufaa ya umma … tazama GEO (kituo kimoja cha televisheni) … SASA hivi&#39; </a>Wapo waliotuaminisha kwamba huyu jamaa anayekwenda zake angejaribu kujitetea ili abaki madarakani, wapo waliotabiri kwamba huenda angerejesha mfumo wa mahakama kama njia yake pekee ya kujinusuru na kulipiza kisasi; kinyume chake hali imegeuka kuwa hotuba ya kuagia, akiachia mambo mbele ya watu wake wa karibu waliokuwa wakilengwalengwa na machozi, hali ambayo tunahabarishwa kupitia kwamba ‘<a href="http://saim-baig.blogspot.com/2008/08/no-last-punch-musharraf-resigns.html">akiwa amevaa uso usio na tabasamu Musharraf, huku akipepewa na bendera za Pakistani nyuma yake na picha ya ‘mwanzilishi’ wa taifa hili</a> aliishia kusema “<strong>Naweka hatma yangu mikononi mwa umma</strong>.”</p>
<p><img src='http://farm1.static.flickr.com/153/345600341_bf03e54162.jpg?v=0' alt='' class='alignnone' /></p>
<p><strong>Pervez Musharraf</strong> - Picha kwa hisani ya: <a href="http://www.flickr.com/photos/worldeconomicforum/345600341/">Mtiririko wa picha za Flickr wa Mkutano wa Uchumi Duniani</a> zilizo chini ya <a href="http://creativecommons.org/licenses/by-sa/2.0/deed.en">haki miliki huria kwa umma</a>.</p>
<p>Kuaga huku kulikotawaliwa na machozi kulikofanya na Musharraf mnamo tarehe 18 Agosti mwaka huu kulikuja zikiwa zimepita siku nne tu tangu Taifa liadhimishe sherehe za miaka 61 ya Uhuru. Ni katika hali ya tahadhari kubwa kwamba Pakistani inaadhimisha mwisho huu wa miaka tisa ya utawala wa familia hii. Hotuba yake ya mwisho ilijaa hasa <a href="http://www.pakspectator.com/look-back-at-musharrafs-era/">kurejelea historia</a> na hii ni kama ilivyonukuliwa na <em>The Pakistani Spectator</em>, yaani hasa kuelezea ni kwa namna gani <a href="http://changinguppakistan.wordpress.com/2008/08/18/its-official-musharraf-resigns/">alitumikia nchi na watu wake</a>.  </p>
<p>Wanablogu wa KiPakistani walipokea taarifa hizi kwa hisia tofauti, wapo waliomshabikia kwa miluzi yenye kuashiria kwamba alikuwa ‘<a href="http://pitafi.com/2008/08/18/for-he-is-a-jolly-good-fellow/">a Jolly Good Fellow’ </a>(mtu mwema na mchangamfu), wakati huohuo washabiki wake waaminifu hawakukawia <a href="http://pak1stanfirst.com/2008/08/18/support-for-president-musharraf/">kumpigia mbija za kumpongeza</a>, hata hivyo wapo waliochukua hali hii kwa tahadhari huku wakisherehekea kumalizika kwa utawala wa kidikteta. Katika namna ya kukejeli, <em>Yeah That Too</em> alishirikisha <a href="http://think-islam.blogspot.com/2008/08/he-came-he-saw-poof.html">maneno machache</a>, <em>Ammar</em> kwa upande wake aliandika kuhusu namna ‘<a href="http://ammar360.com/2008/08/18/the-cat-fight-now-begins/">Mpambano mpya wa manyau’ unavyokaribia kuanza</a>, <em>Chowrangi</em> anazungumizia <a href="http://www.chowrangi.com/pervez-musharrafs-resignation-and-the-way-forward.html">mustakabali wa nchi ya Pakistani baada ya Musharraf</a>, <em>Psychotic Discourses </em>anatupatia mwanga juu ya <a href="http://blog.anasimtiaz.com/2008/08/18/welcome-to-demon-cracy/">muundo mpya wa ‘Utawala wa Kishetani’ </a>(Demon-cracy), wakati ambapo <em>MB</em> anatuchanganya zaidi kwa kuzungumizia hali hii kama moja ya <a href="http://publicmb.wordpress.com/2008/08/18/the-circle-in-the-circus-completes-again/">mizunguko ya kisarakasi</a>. </p>
<p>Swali kubwa kwa sasa linabaki kuwa endapo Musharraf anaruhusiwa kutafuta ukimbizi nje ya Pakistani au endapo <a href="http://kadnan.com/blog/2008/08/18/17th-august-1988-18th-august-2008/">atafikishwa mbele ya sheria</a> ili kujibu <a href="http://www.teeth.com.pk/blog/2008/08/11/reference-against-pervaiz-draft">tuhuma mbalimbali zinazomkabili</a>. Ama kwa hakika ni changamoto kubwa kwa Taifa la Pakistani na ambayo inaweza kuwa na matokeo mengi.</p>
<p>Mtu anabaki kujiuliza, <a href="http://pakistanpolicy.com/2008/08/18/after-musharraf-the-next-president/">hivi nini kinafuata</a>, hasa katika kipindi hiki ambapo kuna wanasiasa wenye matumaini ya kunyakua cheo hicho cha juu zaidi katika taifa hili, ambapo hata hivyo jukumu la kuiondoa nchi katika mkanganyiko huu mkubwa liko zaidi mabegani mwa <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Asif_Ali_Zardari">Asif Zardari</a> na <a href="http://en.wikipedia.org/wiki/Nawaz_Sharif">Nawaz Sharif</a>, ambapo wote wawili ni wanasiasa ambao hawakuchaguliwa lakini ambao wengi wanawawekea matumaini makubwa ya kuiondoa nchi hii kutoka katika lindi la vurugu ambamo imo kwa sasa. </p>
]]></content:encoded>
			<wfw:commentRss>http://sw.globalvoicesonline.org/2008/08/pakistani-musharraf-aondoka-jengoni/feed/</wfw:commentRss>
		<slash:comments>0</slash:comments>
		</item>
	</channel>
</rss>
