GlobalVoices katika

India

Kumbukumbu za nchi · 13 jumbe


Habari mpya Kuhusu India

1 Januari 2013

Kuhusiana na Vuguvugu la Mabadiliko ya Umma

Gaurav Mishra anachambua nguvu ya vuguvugu la mabadiliko linaloanzia kwa watu wa kawaida na namna inavyofanya kazi kuleta mabadiliko chanya katika utendaji wa vyombo vikuu vya habari kwa kutumia vyombo vya habari vya kiraia.

30 Disemba 2012

Video ya Kuomba Ujenzi wa Vyoo vya Umma huko Jharkhand, India

Amit Topno, mwakilishi wa jumuiya ya hiari “inayopiga picha za video” aliripoti kwamba wakati wa kijiji cha Nichitpur katika Jimbo la Jharkhand hawana choo chochote cha umma kinachotumika. Wanavijiji wanaziomba mamlaka za serikali za mitaa kupitia video hii kuhakikisha kuwa vyoo vinavyostahili matumizi ya binadamu vinajengwa.

22 Oktoba 2012

India: Mgogoro wa Mtambo wa Nyuklia wa Kudankulam Waendelea.

Soma makala hii.

Mradi wa Nguvu za Nyuklia mjini Koodankulam katika wilaya ya Tirunelveli iliyo katika Jimbo la kusini la Tamil Nadu nchini India umeanza kufanya kazi mwezi uliopita lakini maandamano ya kuupinga mradi huo umeendelea na kamata kamata inasababisha waandamanaji kuishia jela. Juma hili limeshuhudia maandamano yakienea India yote kwa ushirikiano na watu wanaopinga matumizi ya Mtambo wa Nyuklia.

23 Juni 2012

Pakistani: Buriani Mehdi Hassan; Mfano wa kuigwa wa Ghazal.

Soma makala hii.

Mehdi Hassan Khan ambaye maarufu alijulikana kama ‘Mfalme wa Ghazal’alifariki dunia Jumatano tarehe 13, Juni, 2012 baada ya kuugua kwa muda mrefu, katika hospitali jijini Karachi nchini Pakistan. wananchi wa Mtandaoni wanattoa salamu zao za mwisho.

India: Kipindi cha Runinga cha Aamir Khan Chaweka Wazi Masuala ya Kijamii

Soma makala hii.

Kipindi kipya cha maongezi kwenye televisheni nchi India kinachoitwa Satyamev Jayate (Ni Ukweli tu Utakaoshinda) kinachoendeshwa na muigizaji na mtengeneza filamu wa Bollywood, Aamir Khan kinaleta na kujadili miiko na masuala moto moto ya kijamii ambayo yanawanasa na kuwavutia WaHaindi wengi zaidi na zaidi. Wananchi wa kwenye mtandao wanatoa maoni yao.

26 Septemba 2010

India: Marufuku Kutuma Ujumbe wa Simu za Mkononi wa Jumla

Rajesh Jain kwenye Emergic analaumu kupigwa marufuku utumaji wa jumla wa ujumbe wa simu za mkononi pamoja na ujumbe wa media-anuai ili kuzuia uhamasishaji umma kabla na baada ya hukumu ya Ayodhya.

14 Aprili 2010

India, Pakistani: Hekaheka za Sania-Shoaib Zaendelea

Utata wa harusi ya Shoaib Malik na Sania Mirza unaendelea huku vyombo vya habari vikichochea hekaheka na mamilioni ya watu nchini India na Pakistani wanaendelea kuzama katika habari hiyo. Wakati wapenzi hao wanajiandaa na harusi na kuvishinda vikwazo, sehemu nyingine mashambulizi yanaendelea.

15 Novemba 2009

India: Usawa

“Takriban asilimia 15 ya watu ambao ni viongozi wa siasa na watumishi wa serikali, kwa kupitia vitendo vya kifisadi, wamejilimbikizia asilimia 85 ya utajiri wote wa India, na kuwaachia asilimia 15 tu ya utajiri huo asilimia 85 ya wananchi,” anasema Ram Bansal katika blogu ya India in Peril.

12 Oktoba 2009

Wanablogu Wa Asia Kusini Na Tuzo Ya Nobeli Ya Amani Aliyopewa Obama

Soma makala hii.

Rais wa Marekani Barack Obama amepokea tuzo mashuhuri ya Amani ya Nobeli leo. Wanablogu na wanaoblogu habari fupi fupi huko Asia kusini wanaelezea maoni yao kuhusu habari hiyo.

20 Mei 2009

Uchaguzi wa India 09: India Imepiga Kura, Imeamua kuimarisha Utulivu

Matokeo ya Uchaguzi yanamiminika kutoka kila upande wa nchi na ni dhahiri kwamba India imepiga kura kwa kishindo ili kuchagua serikali imara ya mseto ya UPA, chini ya uongozi wa chama cha Congress. Dr Manmohan Singh atakuwa Waziri Mkuu kwa mara ya pili mfululizo. Hata kabla matokeo hayajatimia, kwa kuangalia tu mwelekeo, kundi la vyama vya mseto la NDA linaloongozwa na chama cha BJP limetangaza rasmi kushindwa kwake katika uchaguzi.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha