Habari kuhusu Bangladesh

Mwanamke Aokolewa Kwenye Kifusi Baada ya Siku 17

  15 Mei 2013

Siku ifananayo na ile iliyogharimu maisha ya watu mara baada ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa tisa huko Savar pembezoni mwa mji mkuu wa Banglasesh, Dhaka, idadi ya watu waliofariki imeongezeka hadi 1,055 , idadi inayopelekea tukio hili kuwa tukio lililowahi kuua watu wengi zaidi tokea lile la tarehe 9/11 kulipotokea mashambulizi ya kigaidi, mfanyakazi mwanamke ajulikanaye kwa jina la Reshma Begum amekutwa akiwa hai mara baada ya kuzuiwa na kifusi cha jengo hilo kwa siku 17.

Bangladesh: Waislamu Wadai Wanawake Wabaki Majumbani

  8 Mei 2013

Wanachama wa kikundi chenye msimamo mkali cha Kiislamu nchini kimewashambulia wanahabari wa kike waliokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kiuandishi wakati kikundi hicho kilipokuwa kikifanya maandamano katika jiji la Dakar kudai kutumika kwa sheria kali za kiislamu, ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku wanawake kuchanganyika na wanaume. Mpaka madai yao yatakapotekelezwa, chama hicho kimejiapiza kulitenga jiji la Dhaka na sehemu nyingine za nchi hiyo ifikapo Mei 5, 2013 kwa kuwaweka wanaharakati wake katika maeneo sita ya kuingilia jiji hilo.

Bangladesh: Jengo Laporomoka, Mamia Wauawa kwenye Vifusi

  29 Aprili 2013

Janga jingine tena la kiwanda nchini Bangladesh, safari hii jengo la ghorofa tisa lilianguka na kuua zaidi ya watu 142 na watu wengine karibu elfu moja kujeruhiwa. Watu wengine wengi bado wamenaswa kwenye kifusi na harakati za kuwaokoa bado zinaendelea. tukio hili linatokana na uzembe wa baadhi ya watu kwani utawala wa kiwanda hiki uliwashinikiza watu kuendelea kufanya kazi katika jengo ambalo halikuwa salama.

Serikali ya Bangladeshi Yawafuatilia Wanablogu, Yawatuhumu Kuukashfu Uislam.

  28 Aprili 2013

Kadri mapambano makali kati ya wanaharakati wa Kiislamu na serikali yanavyoendelea kusababisha migongano ya kidini nchini Bangladesh, Mamlaka ya Mawasiliano ya nchi hiyo imechukua hatua ya kuwanyamazisha wanablogu wanaoonekana wapinzani wa Uislamu na serikali. Asif mshindi wa tuzo ya mwanablogu bora amekuwa akilengwa na hatua hizo kwa siku za hivi karibuni.

Bangladeshi: Raia Wakutana Kudai Haki Itendeke

  17 Februari 2013

Kidogo kidogo, makutano ya Shahbag katika mji mkuu wa Bangladesh, Dhaka yamefurika watu wenye lengo la kutaka haki kufuatia ukatili uliofanywa mnamo mwaka 1971 wakati wa harakati za vita vya kutafuta uhuru pamoja na kudai hukumu ya kifo kwa wahalifu wa vita.Drop by drop, the Shahbag intersection in Bangladesh's capital city Dhaka has become an ocean of people, demanding justice for the atrocities committed during the country's 1971 liberation war and death penalty for war criminals.

Bangladeshi: Msichana Mwingine Mzawa Abakwa na Kisha Kuuliwa.

  2 Januari 2013

Kwa mara nyingine msichana mzawa ameuawa nchini Bangladesh baada ya kubakwa kikatili. Mhanga huyo, Khomaching Marma (14) alikuwa mwanafunzi wa darasa la nane. Ubakaji huu wa kikatili uliosababisha mauaji kwa mara nyingine tena umeamsha hasira na ghadhabu nchini kote. Watumiaji wa mtandao pia wanapinga vikali vitendo hivyo.

Watoto wa Mitaani Bangladesh Wakabiliwa na Unyanyasaji

  13 Novemba 2012

Jumla ya watoto wa mitaani nchini Bangladeshi wanakadiriwa kufikia 400,000. Karibu nusu ya idadi hiyo wanaishi katika Jiji la Dhaka. Asilimia kubwa ya watoto hao ni wasichana. Wasichana hao wa mitaani huishi katika mazingira yenye hatari nyingi hasa unyanyasaji na dhuluma nyingine.

Bangladesh: Mahakama Yaamuru Kufungwa kwa Kurasa za Facebook kwa Kukashifu Dini

  23 Aprili 2012

Mnamo tarehe 21 Machi, mahakama moja huko Bangladesh iliziamuru mamlaka zinazohusika kuzifungia kurasa tano za Facebook na tovuti moja kwa kukashifu Mtume Mohamedi, Kuruani na dini nyinginezo. Wanaharakati wa mtandaoni wana hofu kwamba kama amri hiyo itatekelezwa, basi itafungua milango kwa uhuru wa kujieleza kudhibitiwa katika siku za usoni.

Pakistani: Vitendo vya Unyanyasaji Watoto Vyaongezeka

  26 Machi 2010

Msemo 'Unyanyasaji watoto' hutumika kueleza vitendo vya aina mbalimbali vilivyo jinai na vinavyofanywa dhidi ya watoto. Wanablogu wanajadili vitendo hivi vya unyanyasiaji watoto vinavyokera na vinavyozidi kuongezeka nchini Pakistani.