· Julai, 2013

Habari kuhusu Asia ya Kusini kutoka Julai, 2013

India: Chakula Chenye Sumu Chaua Watoto 24

  18 Julai 2013

Chakula kilichoua wanafunnzi na kuwaacha wengine katika hali mbaya kinasadikiwa kuwa kilichanganyikana na dawa ya kuulia wadudu. Tukio hili linaibua maswali kuhusiana na ubora wa chakula cha mchana wanachopewa wanafunzi wanaotoka katika familia masikini.

Mama na Watoto Wake Wauawa kwa Kucheza kwenye Mvua

  6 Julai 2013

Mama na watoto wake wawili wa kike waliuawa kwa kufyatuliwa risasi mara baada ya watu watano waliokuwa wamefunika nyuso zao kuvamia nyumba alimokuwa akiishi mama huyu na watoto wake katika mji mdogo wa Chilas nchini Pakistan, tukio linalosadikiwa kuwa ni la mauaji ya kulinda heshima. Video iliyorekodiwa kwa simu inayowaonesha wasichana hao wakicheza kwenye mvua imekuwa ikisambaa kiholela na ambayo imeonekana kama ni kashfa na hivyo kuharibu heshima ya familia.