· Mei, 2011

Habari kuhusu Asia ya Kusini kutoka Mei, 2011

Nepal: Mwanzo wa Mapinduzi ya Facebook?

  10 Mei 2011

Pradeep Kumar Singh anaweka picha na habari za kampeni ya hivi karibu ni ya Facebook iliyopewa jina la “Jitokeze. Simama. Ongea. Vinginevyo, kaa kimya. Takriban vijana 400 wa Nepali walijitokeza sehemu ya Maitighar Mandala tarehe 8 Mei, 2011 na kudai katiba mpya.

Pakistani: ISI Walikuwa Wanafahamu Nini Kuhusu Laden?

  8 Mei 2011

Faheem Haider katika blogu ya Sera ya Nchi za Nje ya Pakistani anahoji kile ambacho Jeshi na Usalama wa Taifa (shirika la kijasusi) la Pakistani vilikuwa vinafahamu kuhusu gaidi mkuu Osama Bin Laden, ambaye aliingiliwa na kuuwawa huko Abbottabad, karibu na mji mkuu wa Pakistani.