GlobalVoices katika

Tunisia

Kumbukumbu za nchi · 12 jumbe


Habari mpya Kuhusu Tunisia

8 Oktoba 2012

Tunisia: Mgomo Waanza jijini Thala

Kupitia mtandao wa twita, Tounsia Hourra (m-Tunisia huru) anasema [ar] kuna mgomo mkubwa umeanza jijini Thala, kwenye jimbo la Kasserine, leo [Oktoba 8, 2012]. Mgomo huo umekuja kama hatua ya kupinga kukua kwa kasi kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.


@tounisiahourra
: اضراب عام في تالة ( ولاية القصرين ) اليوم احتجاجا على ارتفاع معدلات البطالة واهمال صيانة المدينة

@tounisiahourra: Mgomo mkubwa jijini Thala (jimbo la Kasserine) leo kupinga kuongezeka kwa ukosefu wa ajira na kuzorota kwa maendeleo ya jiji hilo.

30 Aprili 2012

Video jumbe
Tunisia: Miitikio Tofauti Kufuatia Kuingiliwa kwa Barua Pepe za Waziri Mkuu

Soma makala hii.

Mnamo Aprili 8 “Anonymous Tunisia” kikundi kisichotambulisha majina ya wanachama wao nchini Tunisia (ambacho kinadai kuwa na uhusiano na kikundi cha watu “wasiojitambulisha” ) waingiliao mawasiliano ya watu kiliingilia mawasiliano the ya barua pepe ya waziri mkuu wa Tunisia Hamadi Jebali. Vuguvugu hilo lilipewa jina la utani la (“Achana na Tunisia yangu”) ambayo ni sehemu ya kampeni kuu iitwayo “Operesheni Rejeza Tunisia”.

25 Januari 2012

Photos jumbe
Tunisia: Mwaka 2011 katika Picha za Mitandao ya Kijamii

Soma makala hii.

Mwaka 2011 ulikuwa wa mabadiliko nchini Tunisia. Yote yalianza kwa kuanguka utawala wa Zeine El Abidine Ben Ali, na kuhitimishwa kwa waislamu wenye msimamo mkali kutwaa madaraka kwa kura. Tazama makala hii ya picha kuona matukio makubwa yaliyotokea Tunisia mwaka huu.

Makala za Global Voices Zilizosomwa Zaidi mwaka 2011

Soma makala hii.

Global Voices haijabaki kuwa sauti pweke ya vyombo vya habari vya kiraia linapokuja suala la twita zinazotuma taarifa na posti za kwenye blogu. Bado, hata hivyo pale ambapo shauku kwa vyombo vikuu vya habari ikindelea kupungua, sisi ndio tunaojibidiisha kuendelea kuweka kumbukumbu ya kile ambacho wanablogu wadogo popote pale waliko wanahitaji dunia ikifahamu. Fahamu orodha ya makala zetu 20 zilizosomwa zaidi kwa mwaka 2011

16 Disemba 2011

Uarabuni: Hongera Tunisia!

Soma makala hii.

Human rights activist Moncef Marzouki, 66, has been elected as Tunisia's new interim president today. His appointment, which was followed by a moving acceptance speech, was noted by netizens from across the Arab world, who cheered on Tunisia's progress towards democracy, wishing the same for their countries.

28 Januari 2011

Syria: Propaganda ya Vyombo vya Habari vya Serikali Kuhusu Maandamano ya Tunisia na Misri

Mwanablogu wa ki-Syria Maurice Aaek amegundua[ar] kwamba vyombo vya habari vinavyoendeshwa na serikali nchini Syria vinachapisha habari za uongo na nusu-kweli kuhusu maandamano ya upinzani nchini Tunisia na Misri. Amegundua kwamba gazeti la Tishreen daily halikuweka sababu ambazo zilimfanya Ben Ali aondoke na kuwaachia watu wajitafsirie wenyewe, na kuwa gazeti la Al-Baath daily lilisema kwamba maandamano ya upinzani nchini Misri yana nia ya kutaka balozi wa Izraeli afukuzwe, na kutoyaweka kabisa madai ya kutaka Mubarak ang'atuke.

24 Januari 2011

Tunisia: Anonymous Dhidi ya Ammar – Nani Atashinda Vita ya Kuchuja Habari?

Soma makala hii.

Kichuja habari cha Tunisia, kinachojulikana kama Ammar, kinaeendelea kutishia kuziharibu na kuzifunga anuani za wanaharakati wa mtandaoni, katika nchi hiyo ambayo imekuwa ikishuhudia wimbi la maandamano tangu katikati ya mwezi Desemba. Ni leo tu, wanaharakati wamedai kwamba serikali imeingilia anuani zao za barua pepe,na kuziingilia blogu na mitandao yao ya kijamii, na kuzizuia zisifanye kazi. Hatua hii inaonekana kuja kama kulipiza kisasi kwa shambulio lililofanywa na kikundi cha wanaharakati wa mtanda0ni wanaojulikana kama Anonymous, ambalo lililenga njia na mitandao ya muhimu ya Serikali ya Tunisia.

25 Agosti 2010

Photos jumbe
Tunisia: Picha ‘Zilizochakachuliwa’ ni Dalili ya Hali Halisi katika Vyombo vya Habari vya Kitaifa

Soma makala hii.

Utumiaji vyombo vya habari vya kitaifa nchini Tunisia kama chombo vya kupigia propaganda ni jambo ambalo limeripotiwa vya kutosha. Ushahidi wa hivi karibuni kabisa wa utumiaji mbaya wa vyombo vya habari umewekwa bayana na wanablogu wa nchi hiyo mnamo tarehe 20 Agosti baada ya magazeti ya Le Temps na Assabah kuchapisha ripoti kuhusu taasisi ya hisani ya Zeitouna kutuma msaada wa kibinadamu wa chakula kwa waathirika wa mafuriko nchini Pakistani.

7 Aprili 2010

Tunisia: Wanablogu wa Tunisia Wazungumza Kiingereza

Wanablogu wa Tunisia walizoea kuepuka kutumia Kiingereza (lugha ya tatu nchini mwao), na badala yake waliandika kwa Kiarabu (na wakati mwingine kwa lahaja za Tunisia) au Kifaransa. Lina Ben Mhenni anazitupia macho baadhi ya blogu zinazoandikwa kwa lugha ya Kiingereza.

15 Disemba 2009

Tunisia: Mwanafunzi Atupwa Gerezani kwa Kuhojiwa na Chombo cha Habari

Wanaharakati nchini Tunisia wamezindua ukurasa wa Facebook na blogu ili kumuunga mkono Mohamed Soudani, 24, aliyetoweka mnamo tarehe 22 Oktoba 2009 nchini humo mara baada ya kufanya mahojiano na Redio Monte Carlo International na vilevile Redio France International. Tangia hapo marafiki walipata fununu kwamba alikamatwa na kutupwa korokoroni na kuteswa vibaya.

Sehemu za Dunia

Nchi

Lugha