· Disemba, 2011

Habari kuhusu Syria kutoka Disemba, 2011

Syria: Mwanablogu Razan Ghazzawi Ameachiwa HURU!

  19 Disemba 2011

Habari zinasambaa mtandaoni kwamba mwanablogu wa Syria aliyekuwa gerezani anaweza kuachiwa huru wakati wowote kuanzia sasa. Ghazzawi, anayeblogu akiwa Syria kwa kutumia jina lake halisi, aliwekwa kizuizini akiwa njiani kuhudhuria warsha ya uhuru wa Vyombo vya habari iliyokuwa ikifanyika mjini Amman. Kuwekwa kwake kizuizini kulikosolewa na watumiaji wa mtandao, ambao sasa wanasubiri kwa hamu kuachiwa kwake. Amekuwa ndani kwa siku 15 sasa.